Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 31,829
- 33,224
Napenda kuishauri Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Morogoro, kuchukua tahadhari na kusimamia viwango vya makanisa yanayojengwa kwa nguzo za miti na mbao bila kuta za matofari.
Jana 16.01.2022 majira ya asubuhi karibia na ibada kuanza Kanisa la Nabii Joshua Lililopo Kihonda Yespa liliporomoka kutokana na either nguzo na mbao za paa lake kuoza au viwango vya ujenzi kuwa hafifu, endapo kungekuwa na waumini ndani ya kanisa hilo basi yaliyotokea Mwanza hivi majuzi (watu 14 kufariki kwa ajali) yangejirudia Morogoro kwa mamia ya waumini kufukiwa na paa la kanisa hilo.
Wito kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa ni kupitia upya viwango vya ujenzi wa makanisa yote yaliyojengwa kama mabanda na kuwataka wenye makanisa kuyaimarisha kwa vyuma badala ya miti na mbao kwakuwa ni hatari sana kwa maisha ya watu, hali iliyovyo kwenye kanisa hilo inatisha hivi sana, nakushauri Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama ya Mkoa ufike kwenye eneo la tukio ili ujionee hali ilivyo hatarishi.
Jana 16.01.2022 majira ya asubuhi karibia na ibada kuanza Kanisa la Nabii Joshua Lililopo Kihonda Yespa liliporomoka kutokana na either nguzo na mbao za paa lake kuoza au viwango vya ujenzi kuwa hafifu, endapo kungekuwa na waumini ndani ya kanisa hilo basi yaliyotokea Mwanza hivi majuzi (watu 14 kufariki kwa ajali) yangejirudia Morogoro kwa mamia ya waumini kufukiwa na paa la kanisa hilo.
Wito kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa ni kupitia upya viwango vya ujenzi wa makanisa yote yaliyojengwa kama mabanda na kuwataka wenye makanisa kuyaimarisha kwa vyuma badala ya miti na mbao kwakuwa ni hatari sana kwa maisha ya watu, hali iliyovyo kwenye kanisa hilo inatisha hivi sana, nakushauri Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama ya Mkoa ufike kwenye eneo la tukio ili ujionee hali ilivyo hatarishi.