Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,891
- 939
MHE. NDAISABA RUHORO ATEMBELEWA BUNGENI NA KAMATI YA SIASA WILAYA YA NGARA
Mbunge wa Jimbo la Ngara Mhe. Ndaisaba George Ruhoro wiki hii aliialika Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Ngara chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Mwl. Vitalis Ndailagije na Mkuu wa Wilaya ya Ngara Kanali Mathias Julius Kahabi kuhudhuria Mkutano wa 11 wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kikao cha 14
Baada ya ziara ya Bungeni Mhe. Ndaisaba aliipeleka Kamati hiyo kwenda kuuona Mji wa Kiserikali Mtumba (Magufuli City) na kupokelewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utumishi na Utawala Bora Ndugu Xavier Daudi
Kamati ilipata nafasi ya kuzungukia Miradi ya Ujenzi wa Miundombinu mbalimbali kuona namna Serikali ya awamu ya sita ya chini ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan inavyotekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi
Kamati ilipata wasaa wa kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi TAMISEMI Mhe. Angellah Kairuki huku ujumbe wa Kamati ukiwa ni kutoa salamu za Shukrani kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuelekeza fedha zinazoendelea kukamilisha miradi mbali mbali ya Maendeleo Jimboni
Mhe. Waziri alifurahi sana na kuwakaribisha tena wajumbe wa Kamati, na kuwaahidi kuwa Serikali itaendelea kutenga fedha kwaajili ya kukamilisha Miradi ya Maendeleo, ili Wananchi wake waendelee kupata nafuu ya maisha.
Attachments
-
WhatsApp Image 2023-04-29 at 20.38.00.jpeg54.5 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-04-29 at 20.37.58(1).jpeg48.1 KB · Views: 4
-
WhatsApp Image 2023-04-29 at 20.37.59(1).jpeg46.7 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-04-29 at 20.37.57.jpeg59.9 KB · Views: 4
-
WhatsApp Image 2023-04-29 at 20.38.00(1).jpeg59.4 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-04-29 at 20.38.01.jpeg36.7 KB · Views: 4