Kamati ya Olimpiki (TOC) wamuita Alphonce Simbu MUASI, kisa Mavazi ya mbio za Olimpiki Paris, Ufaransa

Melubo Letema

JF-Expert Member
Apr 1, 2020
416
413
IMG_3278.jpeg


Wakati Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa mstari wa mbele kuhamasisha na kukuza Michezo Tanzania ukiwemo wa riadha ,

ila kuna Vizee vilivyopo kwenye Kamati ya Olimpiki Tanzania (Tanzania Olimpic Committee ~ TOC) vinaendekeza hila na uzandiki wa kufikia kumuita mwanariadha wa kimataifa Alphonce Simbu MUASI , hiyo haitoshi alikuwa anagombe Uenyekiti wa Kamisheni ya wachezaji ila hao wazee wakakata jina lake wazee hao ni Henry Tandau (makamu wa rais TOC) na Ghulam (Rais wa TOC) sambamba na Filbert Bayi (Katibu wa TOC) , kisa eti alikataa kukimbia akiwa amevaa mavazi ya kampuni ya ASICS kutumia kampuni ya XTEP

SOMA WALICHOANDIKA WADAU WA RIADHA:

Shida ya kwanza ameenguliwa kwa kwa kutuhumiwa kua kahamasisha mgomo wa kuvaa Xtep wakat ukweli ni kwamba Tandau aliwadanganya watanzania kua amesajili Asics wakati RT iliishasajili Xtep. Simbu kama mchezaji hakua na uwezo wa kukubali au kukataa vifaa wakati aneishaambiwa vifaa gani vimesajiliwa.

Hata tukiachana na kumkata kwanini Tandau amdhalilishe Simbu kwa kumwita Muasi? Simbu ameipambania sana hii nchi kwenye mashindano mbali mbali ya IOC, Common Wealth Games Commitee, Ya Shirikisho, Ya Majeshi kote amepeperusha bendera ya nchi kwa miaka mingi tangu alipoanza kwenda kimataifa.

Leo mtu anaamua kumwita Muasi mbele ya hadhara ya wanamichezo mbalimbali. Hii sio haki kabisa. Nafikiri Wanamichezo wote tuna deni kwa Simbu na tunapaswa kumpigania kwa nguvu zote katika hili kama
Ambavyo yeye amekua akitupigania kimataifa.

Simbu kashiriki mashindano ya kuibeba nchi kwa miaka ya mfululizo bila kuchoka. Hivi karibuni amelazimika kucheza marathon mbili ndani ya siku saba kwajili ya nchi yake. Amecheza Majeshi Naijeria jumapili moja na akapata Gold, na jumapili
Iliofuata kaenda kucheza Valencia na akapata Shaba. Tutakua tumemsaliti kama
Tutakaa kimya na kuacha lipite hivi hivi.

UDHALILISHAJI WA MWANARIADHA:

Simbu ni mwanajeshi, Simbu ni mwanariadha wa kimataifa, Simbu ni Kapteni wa timu ya Taifa ya Riadha, 2022 alikua kapteni wa timu ya Taifa ya Tanzania ilioshiriki Birmingham Common Wealth Games na akaleta medali ya fedha, Simbu ni icon ya Taifa katika michezo.

Huyo Henry Tandau August 2021 baada ya Tokyo Olympic alienda Ikulu kwaajili ya Simbu, leo hawezi kumwita Simbu Muasi alafu ikaisha hivi hivi, lazima pafanyike jambo.
 
Yawezekana ni kweli muasi. Wao wameweka hoja, na wewe ungeweka hoja kuwa kwa kufanya vile haitoshi kuitwa muasi. Iwapo Taifa Stars iliadhibiwa na CAF kulipa zaidi ya sh. 100M kwa mchezaji mmoja tu kukosea kuvaa jezi yenye namba yake, why ajabu kuadhibiwa kwa kuvaa ya brand tofauti?
 
BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE ALITUTAJIA MAADUI.

1. UMASIKINI
2.UJINGA.
3. MARADHI.

Akasema Hawa ni maadui wa kweli kweli katika hili Taifa.

LEO 2024 BAADA YA MIAKA 60 TUMEKUWA NA MAADUI WENGI ZAIDI.

2024 maadui wameongeseka Zaidi kuliko wale watatu wa 1961.

1.Umasikini na ufukara.
2.Ujinga na upumbavu.
3.Magonjwa na Maradhi.

4.Mmomonyoko wa Maadili.
ushoga, usagaji Kamali, sugar mamy, sugar Dady mashangazi
AJIRA.
5. Rushwa na Upendelo

6. USimba na u yanga.
7. Mitandao ya kijamii Tiktok, x, nk
8. Manabii wa uongo na Mashehe Uchwara.
9. Ajali nyingi mno.
10. Gharama kubwa za maisha, ujenzi holela nk

MAMBO NI MENGI SANA VIJANA WA KITANZANIA WANAWAZA MAMBO YA HOVYO SANA SIMBA NA YANGA ZINATAWALA MIKEKA NK.


OKOENI TAIFA LENU LEO.

IPO SIKU HILI TAIFA LITAZIDIWA NA SOMALIA KIUCHUMI.

MKIFIKA MBINGUNI MTAHOJIWA NA MUNGU MLILIFANYIA NINI TAIFA LENU NIMEMALIZA.
 
UMASIKINI UJINGA NA MARADHI UNALITESA TAIFA TANGU MWAKA 1961 DECEMBER 9

LEO NI KUMBUKIZI YA MIAKA 63 YA UHURU.
 
Yawezekana ni kweli muasi. Wao wameweka hoja, na wewe ungeweka hoja kuwa kwa kufanya vile haitoshi kuitwa muasi. Iwapo Taifa Stars iliadhibiwa na CAF kulipa zaidi ya sh. 100M kwa mchezaji mmoja tu kukosea kuvaa jezi yenye namba yake, why ajabu kuadhibiwa kwa kuvaa ya brand tofauti?
Uwe unafikiria vizuri .
Mleta alichosema kisome vizuri
 
BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE ALITUTAJIA MAADUI.

1. UMASIKINI
2.UJINGA.
3. MARADHI.

Akasema Hawa ni maadui wa kweli kweli katika hili Taifa.

LEO 2024 BAADA YA MIAKA 60 TUMEKUWA NA MAADUI WENGI ZAIDI.

2024 maadui wameongeseka Zaidi kuliko wale watatu wa 1961.

1.Umasikini na ufukara.
2.Ujinga na upumbavu.
3.Magonjwa na Maradhi.

4.Mmomonyoko wa Maadili.
ushoga, usagaji Kamali, sugar mamy, sugar Dady mashangazi
AJIRA.
5. Rushwa na Upendelo

6. USimba na u yanga.
7. Mitandao ya kijamii Tiktok, x, nk
8. Manabii wa uongo na Mashehe Uchwara.
9. Ajali nyingi mno.
10. Gharama kubwa za maisha, ujenzi holela nk

MAMBO NI MENGI SANA VIJANA WA KITANZANIA WANAWAZA MAMBO YA HOVYO SANA SIMBA NA YANGA ZINATAWALA MIKEKA NK.


OKOENI TAIFA LENU LEO.

IPO SIKU HILI TAIFA LITAZIDIWA NA SOMALIA KIUCHUMI.

MKIFIKA MBINGUNI MTAHOJIWA NA MUNGU MLILIFANYIA NINI TAIFA LENU NIMEMALIZA.
Nyie mods mnakula mshahara wa melo bure tu
Sasa huyu mjinga kila mara analeta mashudu yake mnamchekea tu
Nyie wa hovyo na nyie
 
Ila mwamba unahangaika mno na hawa viongozi waliopo w TOC. Hii ni thread kama ya ngapi sijui unapambania jezi za asics.

Anyway inawezekana una hoja ila si mna uchaguzi karibuni kwenye hiki chama chenu, kwanini usigombee urekebishe haya mambo iwapo yana ukweli na wajumbe watakuelewa?
 
Ila mwamba unahangaika mno na hawa viongozi waliopo w TOC. Hii ni thread kama ya ngapi sijui unapambania jezi za asics.

Anyway inawezekana una hoja ila si mna uchaguzi karibuni kwenye hiki chama chenu, kwanini usigombee urekebishe haya mambo iwapo yana ukweli na wajumbe watakuelewa?
Uchaguzi umefutwa na BMT.
 
Back
Top Bottom