Kamati ya Nidhamu ya Bunge ivunjwe/kuwajibishwa kwa kuliingiza taifa katika mgogoro wa kikatiba. Ndugai awajibishwe

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Baada ya tamko toka Ikulu (sijui kama ni la kweli au fake) kwamba inasikitishwa na azimio la Bunge la kukataa kufanya kazi na CAG, azimio ambalo si tu linaleta mgogoro wa kikatiba, bali pia linamshushia hadhi raisi kwa namna ya kumwambia Bunge linaweza kuingilia mamlaka yake. Bunge limetoa tamko la kumgomea raisi! Labda tujiulize kama Bunge linafanya hivyo kwa kuwa mara kadhaa raisi ameonekana akiingilia mamlaka ya Bunge.

Jambo la pili, inafikia mahali ijulikane wazi kwamba Ndugai amekuwa mkubwa kuliko viatu vyake. Ndugai amekuwa na silka ya kujipa mamlaka kupita kiasi, pamoja na kuwadhalilisha wabunge. Tunakumbuka jinsi alivyotoa mwito wa kumwita CAG kwa namna ya dharau. Tunakumbuka kauli yake ya kebehi kwa Lema.Ndugai amekuwa akiwachukulia wabunge kama mwalimu mkuu na watoto wa shule ya msingi.

Kwa hiyo basi, lazima kamati ya nidhamu ya Bunge, na spika Ndugai, kwa namna moja au nyingine, wawajibishwe kwa walilofanya. Wao wamezoea sana kuwawajibisha watu kwa vitu vidogo visivyo na msingi, na imefika mahali wanyweshwe dawa waliyotengeneza wenyewe!

Ni wazi Bunge lina udhaifu mkubwa, katika utendaji na uongozi.
 
Dunia hii na ulimwengu kwa ujumla,lazima maadui wawepo,na watakao kupenda wawepo,kwa matendo yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Tuache ukweli uwe ukweli. Kama ambavyo hatupendi Ndugai afanye kazi kwa maagizo ya Magufuli, hatupendi Kamati ya Nidhamu ya Bunge ifanye kazi kwa maagizo ya Ndugai.

Tungependa kuona pia maamuzi yeyote au hukumu zilizofanywa kuhusiana na Bunge kuwa dhaifu zipitiwe upya. NI wazi zilikuwa na shinikizo la spika ambaye hakuwa anafikiria kwa busara.
 
Hii kamati ya maadili ya bunge inaongozwa kimihemko sana na adhabu zao zinawakomesha wananchi sio mbunge, na pia Job Nfugai ifike mahala akomae ki uweledi namna ya kuliongoza bunge na sio vinginevyo, sasa kutoshirikiana na CAG je bunge ni nyumba yake ama muhimili na chombo cha kitaifa, apeleke jaziba zake nyumbani kwake
 
Pamoja na mapungufu ya kamati ya maadili bado wabunge wanaoimba kila kitu ndiyoooooo ! ni tatizo.Wabunge tuangalie zaidi maslahi mapana ya taifa.Wabunge wangekuwa wanazingatia hilo maazimio ya kamati mengi yangekuwa yanapigwa chini, na kamati isingekuwa inakuja na maazimio dhaifu.
 
Hii inaweza kufanyika tu kama wabunge wetu watakuwa na uzalendo na kusahau njaa. Uzalendo na kuwa na ufahamu katika maamuzi ni kufikia mafanikio
 
Hii inaweza kufanyika tu kama wabunge wetu watakuwa na uzalendo na kusahau njaa. Uzalendo na kuwa na ufahamu katika maamuzi ni kufikia mafanikio
Mkuu wabunge walio wengi wa chama tawala si ndio wanaongoza kwa uzalendo, au?
 
Kwa hiyo Mkuu hadi sasa unaona hakuna tatizo hapo Bungeni, kwa Ndugai na hiyo Kamati yake?
Mkuu tatizo lipo,kwa wabunge wote,wakiwemo na wa upinzani kwa kuendekeza utovu wa nidhamu ili kupata kiki ,CAG, na sisi masapota wao.

Tunatoa tafsiri tukitanguliza mitizamo ya kisiasa ya vyama tunavyoshabikia.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya tamko toka Ikulu kwamba inasikitishwa na azimio la Bunge la kukataa kufanya kazi na CAG, azimio ambalo si tu linaleta mgogoro wa kikatiba, bali pia linamshushia hadhi raisi kwa namna ya kumwambia Bunge linaweza kuingilia mamlaka yake. Bunge limetoa tamko la kumgomea raisi! Labda tujiulize kama Bunge linafanya hivyo kwa kuwa mara kadhaa raisi ameonekana akiingilia mamlaka ya Bunge.

Jambo la pili, inafikia mahali ijulikane wazi kwamba Ndugai amekuwa mkubwa kuliko viatu vyake. Ndugai amekuwa na silka ya kujipa mamlaka kupita kiasi, pamoja na kuwadhalilisha wabunge. Tunakumbuka jinsi alivyotoa mwito wa kumwita CAG kwa namna ya dharau. Tunakumbuka kauli yake ya kebehi kwa Lema.Ndugai amekuwa akiwachukulia wabunge kama mwalimu mkuu na watoto wa shule ya msingi.

Kwa hiyo basi, lazima kamati ya nidhamu ya Bunge, na spika Ndugai, kwa namna moja au nyingine, wawajibishwe kwa walilofanya. Wao wamezoea sana kuwawajibisha watu kwa vitu vidogo visivyo na msingi, na imefika mahali wanyweshwe dawa waliyotengeneza wenyewe!

Ni wazi Bunge lina udhaifu mkubwa, katika utendaji na uongozi.
Watanzania,
Watanzania,
Watanzania,nani katuloga?Why are we so bogus.
Tunajidharaulisha sana.
 
Inasemekana ni fake
IMG-20190405-WA0001.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom