Kamati ya Ngwilizi haijakidhi haja bali imeleta mswali yasiyo na majibu

DR. MWAKABANJE

JF-Expert Member
Nov 7, 2012
1,976
3,122
Kwanza kabisa napenda kuwaomba radhi wana jf, wa thread hii kuipost leo, ni hii ni kwa sababu ya kukosa umeme ambapo hapa mwanza baadhi ya maeneo tunapata umeme kwa saa 10 tu, na ni mgao wa kimyakimya.Hoja yangu leo, Ni muda mchache tu baada ya Mbunge wa kigoma kaskazini Mh. Zitto Kabwe (CHADEMA) kupeleka hoja binafsi bungeni juu ya kuundwa kwa kamati teule ya bunge pamoja na mambo mengine kuchunguza uwepo wa fedha chafu za watanzania nchini Uswisi, pia ikumbukwe kwamba kuna mkutano wa wanachama wa jumuiya ya Afrika mashariki juu ya kupambana na rushwa ndani ya nchi hizo unaoendelea mjini mwanza (malaika hotel).Ni katika mkutano huo basi tumepata kumsikia mkurugenzi wa taasisi yetu inyojiita taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini bwana Dr. Edward Hosea akiongea na vyombo mbalimbali vya habari hasa katika hoja ya fedha za uswis ikionekana kama majibu kwa Mh. Zitto na watu tunaounga mkono hoja hiyo.Naomba nimnukuu kidogo japo inaweza isiwe neno kwa neno," watu wanaongea kuhusu fedha za uswisi bila kutuletea majina, sisi ni taasisi inayofuata sheria hivyo hatuwezi kufanya kazi bila kufuata sheria tunataka watu watuletee majina vinginevyo tutawakamata watu halafu baadaye tuliingize taifa kwenye matatizo""huwezi ukaendelea kupiga kelele tu mwizi mwizi wakati ushahidi umeuweka mfukoni""Huwezi ukapiga kelele tu bila kutaja majina hata uswisi wamesema tupeleke majina, leta majina sasa tuyashughulikie we si unauchungu sana na nchi hii" mwisho wa kumnukuu japo aliongea mengi sana!Binafsi tatizo nililonalo kwa huyu bwana ni kwamba nashindwa kumuelewa kwamba inamaana kwenye taasisi yake amepewa kazi halafu anasubiri watu wamuonyesha wala rushwa, wamtajie majina halafu wampelekee ushahidi kazi yao sasa ni nini naomba atueleze?Pili, kauli hii imeniumiza sana sana, leta majina sasa tuyashughulikie we si unauchungu sana na nchi hii" kwani anatuonyesha kuwa kikwete kampa kazi mtu asiye mzalendo, anayemuona zito kama mwenye kihelehele, mtaka umaarufu kama wao wanavyosema nk.Sasa kama anaonyesha wazi wazi kushindwa kazi, kama tulivyoona hata kwenye uchaguzi wa ndani ya CCM, anahaki gani ya kuendelea kutanua na magari ya wananchi, fedha na ofisi nzuri za watanzania ?
 
Kwanza kabisa napenda kuwaomba radhi wana jf, wa thread hii kuipost leo, ni hii ni kwa sababu ya kukosa umeme ambapo hapa mwanza baadhi ya maeneo tunapata umeme kwa saa 10 tu, na ni mgao wa kimyakimya.

Sijakuelewa, title ni kama haiendani na contents, kamati ya Ngwilizi ina uhusuiano wowote na fedha za uswisi?

Na hapo kwenye red ni kama umejichanganya, mnakosa halafu mnapata kwa masaa 10, hayo masaa 10 hayatoshi kupost uzi?
 
Nimekupata mkuu, nimeedit title yangu kwani nilishaiona kulikuwa na tatizo la mtandao nilipopost mara ya kwanza iligoma niliporudia kama mara tatu ikakubali na nikashangaa title imeweka ya uzi niliopost kitambo

Kuhusu swala la umeme, inatokea umeme unakata kuanzia saa 1 asubh. kurudi saa 1 jion, na ukiirudi unakuta kunamabo yametinga so sometimes it becomes difficulty.
 
Kwanza kabisa napenda kuwaomba radhi wana jf, wa thread hii kuipost leo, ni hii ni kwa sababu ya kukosa umeme ambapo hapa mwanza baadhi ya maeneo tunapata umeme kwa saa 10 tu, na ni mgao wa kimyakimya.Hoja yangu leo, Ni muda mchache tu baada ya Mbunge wa kigoma kaskazini Mh. Zitto Kabwe (CHADEMA) kupeleka hoja binafsi bungeni juu ya kuundwa kwa kamati teule ya bunge pamoja na mambo mengine kuchunguza uwepo wa fedha chafu za watanzania nchini Uswisi, pia ikumbukwe kwamba kuna mkutano wa wanachama wa jumuiya ya Afrika mashariki juu ya kupambana na rushwa ndani ya nchi hizo unaoendelea mjini mwanza (malaika hotel).Ni katika mkutano huo basi tumepata kumsikia mkurugenzi wa taasisi yetu inyojiita taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini bwana Dr. Edward Hosea akiongea na vyombo mbalimbali vya habari hasa katika hoja ya fedha za uswis ikionekana kama majibu kwa Mh. Zitto na watu tunaounga mkono hoja hiyo.Naomba nimnukuu kidogo japo inaweza isiwe neno kwa neno," watu wanaongea kuhusu fedha za uswisi bila kutuletea majina, sisi ni taasisi inayofuata sheria hivyo hatuwezi kufanya kazi bila kufuata sheria tunataka watu watuletee majina vinginevyo tutawakamata watu halafu baadaye tuliingize taifa kwenye matatizo""huwezi ukaendelea kupiga kelele tu mwizi mwizi wakati ushahidi umeuweka mfukoni""Huwezi ukapiga kelele tu bila kutaja majina hata uswisi wamesema tupeleke majina, leta majina sasa tuyashughulikie we si unauchungu sana na nchi hii" mwisho wa kumnukuu japo aliongea mengi sana!Binafsi tatizo nililonalo kwa huyu bwana ni kwamba nashindwa kumuelewa kwamba inamaana kwenye taasisi yake amepewa kazi halafu anasubiri watu wamuonyesha wala rushwa, wamtajie majina halafu wampelekee ushahidi kazi yao sasa ni nini naomba atueleze?Pili, kauli hii imeniumiza sana sana, leta majina sasa tuyashughulikie we si unauchungu sana na nchi hii" kwani anatuonyesha kuwa kikwete kampa kazi mtu asiye mzalendo, anayemuona zito kama mwenye kihelehele, mtaka umaarufu kama wao wanavyosema nk.Sasa kama anaonyesha wazi wazi kushindwa kazi, kama tulivyoona hata kwenye uchaguzi wa ndani ya CCM, anahaki gani ya kuendelea kutanua na magari ya wananchi, fedha na ofisi nzuri za watanzania ?

Kwanza nikusahihishe kuwa haya maneno mekundu hayawezi kufuatana. Pili ni imani yangu kuwa TAKUKURU wanafanyia kazi tuhuma na ushahidi ni lazima upatikane toka kwa mtuhumu, ni haki kabisa Dr. Hosea kuwataka akina ZITTO wapeleke majina kama ushahidi ambao hatimaye TAKUKURU watakuja na jibu sahihi. Unafikiri Wataanzia wapi endapo watataka kufanyia kazi tuhuma hizo kama siyo kwa akina ZITTO? lazima wapelekewe majina.
 
Kwanza nikusahihishe kuwa haya maneno mekundu hayawezi kufuatana. Pili ni imani yangu kuwa TAKUKURU wanafanyia kazi tuhuma na ushahidi ni lazima upatikane toka kwa mtuhumu, ni haki kabisa Dr. Hosea kuwataka akina ZITTO wapeleke majina kama ushahidi ambao hatimaye TAKUKURU watakuja na jibu sahihi. Unafikiri Wataanzia wapi endapo watataka kufanyia kazi tuhuma hizo kama siyo kwa akina ZITTO? lazima wapelekewe majina.
mwananchi wa kawaida anaweza kushikiliwa na jeshi la polisi kwa muda mrefu (zaidi ya mwaka) kwa kutuhumiwa tu.(kila kesi inapotajwa mahakamani wanajibu upelelezi haujakamilika).kama hiyo inawezekana,kwa nini ishindikane kwa hao majambazi?
hata wakipewa hawatayafanyia kazi wala hawana uwezo wa kuyafanyia kazi.maswali ya kujiuliza ni je;
1:waliokwapua fedha za EPA walifanywa nini.(ukirudisha ulichoiba unasamehewa au umeleta ushahidi ili uhukumiwe?)
2:mheshimiwa Rais aliwahi kusema kwamba ana orodha ya viongozi wa dini wanaofanya biashara ya madawa ya kulevya.yamefanyiwa kazi.?
 
Nafikiri ni katika nchi yetu tu, ukituhumu rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, njama za kuuawa, kunyweshwa sumu na mengineyo ya jinai, utatakiwa upeleke ushahidi kwa vyombo vyetu vya dolaili vifanye uchunguzi. Lakini ki-ukweli wanatakiwa wakipewa taarifa, wazifanyie uchunguzi wao na si kuwapa ushahidi. Maana unaweza ukawa nao, lakini kimamlaka ukakosa mwingine. Wao kama vyombo vya dola, wana mamlaka ya kuchunguzi zaidi na hata kupata nyaraka zaidi. Hivi nini maana ya intelijensi! Nchini kwetu hii intelijensi inafanya kazi kwenye maandamo na migomo tu?
 
Hivi hii ishu inaendeleaje? Maana nakumbuka tuliishia pale Lissu aliposema wataenda lakini hawatakubali kuhojiwa...
 
Mkuu hata kama umekosea mi binafsi hapo kwenye red pameniuma saana kumbe kuna watu wana madaraka makubwa hawana uchungu na nchi hii kwa cheo kama cha Hosea kutamka maneno haya ujue nchi hii hakna kiongozi. Nayaamini maneno ya chenge hivi ni vijisenti kwa Hosea nchi hii haina viongozi wazalendo. Hongera Hosea sasa tunajua kumbe haupo kwaajili ya kupinga rushwa bali kutetea wala rushwa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom