DR. MWAKABANJE
JF-Expert Member
- Nov 7, 2012
- 1,976
- 3,122
Kwanza kabisa napenda kuwaomba radhi wana jf, wa thread hii kuipost leo, ni hii ni kwa sababu ya kukosa umeme ambapo hapa mwanza baadhi ya maeneo tunapata umeme kwa saa 10 tu, na ni mgao wa kimyakimya.Hoja yangu leo, Ni muda mchache tu baada ya Mbunge wa kigoma kaskazini Mh. Zitto Kabwe (CHADEMA) kupeleka hoja binafsi bungeni juu ya kuundwa kwa kamati teule ya bunge pamoja na mambo mengine kuchunguza uwepo wa fedha chafu za watanzania nchini Uswisi, pia ikumbukwe kwamba kuna mkutano wa wanachama wa jumuiya ya Afrika mashariki juu ya kupambana na rushwa ndani ya nchi hizo unaoendelea mjini mwanza (malaika hotel).Ni katika mkutano huo basi tumepata kumsikia mkurugenzi wa taasisi yetu inyojiita taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini bwana Dr. Edward Hosea akiongea na vyombo mbalimbali vya habari hasa katika hoja ya fedha za uswis ikionekana kama majibu kwa Mh. Zitto na watu tunaounga mkono hoja hiyo.Naomba nimnukuu kidogo japo inaweza isiwe neno kwa neno," watu wanaongea kuhusu fedha za uswisi bila kutuletea majina, sisi ni taasisi inayofuata sheria hivyo hatuwezi kufanya kazi bila kufuata sheria tunataka watu watuletee majina vinginevyo tutawakamata watu halafu baadaye tuliingize taifa kwenye matatizo""huwezi ukaendelea kupiga kelele tu mwizi mwizi wakati ushahidi umeuweka mfukoni""Huwezi ukapiga kelele tu bila kutaja majina hata uswisi wamesema tupeleke majina, leta majina sasa tuyashughulikie we si unauchungu sana na nchi hii" mwisho wa kumnukuu japo aliongea mengi sana!Binafsi tatizo nililonalo kwa huyu bwana ni kwamba nashindwa kumuelewa kwamba inamaana kwenye taasisi yake amepewa kazi halafu anasubiri watu wamuonyesha wala rushwa, wamtajie majina halafu wampelekee ushahidi kazi yao sasa ni nini naomba atueleze?Pili, kauli hii imeniumiza sana sana, leta majina sasa tuyashughulikie we si unauchungu sana na nchi hii" kwani anatuonyesha kuwa kikwete kampa kazi mtu asiye mzalendo, anayemuona zito kama mwenye kihelehele, mtaka umaarufu kama wao wanavyosema nk.Sasa kama anaonyesha wazi wazi kushindwa kazi, kama tulivyoona hata kwenye uchaguzi wa ndani ya CCM, anahaki gani ya kuendelea kutanua na magari ya wananchi, fedha na ofisi nzuri za watanzania ?