habari za kusadikika zimetoka bungeni, huku waziri mkuu Mizengo Pinda akithibitisha kuwa Wizara ya Nishati na Madini inayoongozwa na mjukuu wa wa Mapcha wa magamba Ndugu Ngeleja, ikiwa imewahaonga wajumbe wa kamati ya Nishati na Madini ya bunge la JMT. Kamati hii inasadikika kula mlungula ili kuwadhulumu watanzania haki yao ya msingi ya kuibana serikali ili umeme uwake.
Maswali.
Kwanini wizara itoe rushwa kwa wabunge inaficha nini?
Je kwanini tuwe na wabunge kama wao kazi yao ni kula rushwa na kuacha kufanya kazi ya kuiwajibisha serikali.
Je takukuru walikuwa wapi?
Usalama wa taifa/CCM walikuwa wapi?
Kwanini hawa wabunge bado wapo bungeni?
Kwanini Ngeleja bado ni waziri?
Ninafikiri inabidi nguvu ya umma iingilie kati kumwajibisha ngeleja na kurugenzi yote ya wizara ya Nishati na madini. Vilele kama wajumbe wa hiyo kamati hawatajitakasa, nao wakimbizwe wote kwani ni wezi na wasioitendea nchi mema. Ni wahujumu wakubwa wa uchumi.