Uchaguzi 2020 Kamati ya Maadili yatolea ufafanuzi adhabu dhidi ya Lissu kumfungia kampeni. Yasema ameadhibiwa na Kamati ya Vyama 15 vinavyoshiriki Uchaguzi Mkuu

Lissu aendelee na kampeni kama kawaida ya ratiba yake.
 
Tume hii iliyojaa doublestand nani mwenye akili ataiamini?!

Ina maana kwenye hizo form za kugombea wahusika hawajazi ananuani zao?

Na kama hawajazi anuani tofauti na za vyama vyao bali wanajaza za chama,nani alipaswa kuwa addressed kwenye hiyo barua kupitia ananuani ya chama?

Je,si walipaswa kumu-address Lissu kama mgombea kupitia anuani ya chama chake?
Soma maelezo yote utaelewa.
 
Pamoja na kuwa upande wa lissu, lakini kuna sehemu anakosea. Sehemu yenyewe ni; Lissu sio mgombea binafsi hivyo barua haiwezi kupelekwa kwake binafsi bali itapitia chama ambacho ndio anakitumia kugombea.

Ingekuwa jambo la ajabu sana kama NEC wangemplekea lissu barua yeye kama yeye badala ya chama Sasa kuhusu yaliyomo kwenye barua mimi sidhani kama yana mashiko.

Mwisho kabisa, hadi sasa lissu ni kama ashatengeneza mgogoro na NEC, je anategemea kushinda kwenye mazingira gani na je anategemea wagombea wa ubunge na udiwani watashindaje?

Au ndio tutasema kuwa hatutakubali? Hakuna tena jipya chini ya jua, naona kabisa yatatokea yale yaliyotokea uchaguzi wa serikali za mitaa na mwisho wa siku chama ndio kitaathirika.
 
Lisu anafanya makusudi kuvuruga uchaguzi, kwani anajua hawezi kushinda. Taminio lake ni kuleta vurugu ili kuchafua nchi kwa wahisani ionekane tanzania hakuna haki wala demokrasia. Hila zake hazitafanikiwa
Una ushahidi kuwa kafanya makusudi. With evidence tetea hoja yako. Lakin ulete ushahid wa uhakika
 
vyama vya Ada-Tadea, CUF, SAU, UPDP, , CHAUMMA, CCM, NCCR-Mageuzi, DP, UMD, , NRA, Demokrasia Makini, ADC na AAFP .
 
Nmecheka sana hapo waliposema hao mawakili wasomi wa Lisu walisema Lisu na chadema ni vitu viwili tofauti.

Kumbe Lisu kawalisha watu wengi sana umbumbumbu wake
Nimeshindwa kushangaa hili, ni kwamba wanafanya kusudi? Hawajui kuwa lissu sio mgombea binafsi??
Kama kweli viongozi wa juu wa chadema wanasupport hili basi kuna tatizo kubwa sana
 
Back
Top Bottom