jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,053
- 28,245
Naona Rais Magufuli anafanyia kazi ushauri wa kamati ya kudumu ya bunge ya nishati na madini.
Katika bunge mwaka 2015/16 Ripoti ya kamati hii inaitaja acacia na a.k.a zake zote kuwa ni kampuni ya madini iliyokataa kulipia kodi zilizowekwa kisheria na kimkataba...hii ni pamoja na kufuatiliwa na kutakiwa kufanya hivyo.
Hii ina maana ni kiburi chao wenyewe kilichopelekea kuliamshi Dubwana Magufuli.
Lakini pia ina maana ni kampuni isiyo na uadilifu linapokuja suala la ulipaji kodi hivyo ni sahihi kabisa mtu akisema kuwa wanatumia mbinu chafu kutuibia.
Katika bunge mwaka 2015/16 Ripoti ya kamati hii inaitaja acacia na a.k.a zake zote kuwa ni kampuni ya madini iliyokataa kulipia kodi zilizowekwa kisheria na kimkataba...hii ni pamoja na kufuatiliwa na kutakiwa kufanya hivyo.
Hii ina maana ni kiburi chao wenyewe kilichopelekea kuliamshi Dubwana Magufuli.
Lakini pia ina maana ni kampuni isiyo na uadilifu linapokuja suala la ulipaji kodi hivyo ni sahihi kabisa mtu akisema kuwa wanatumia mbinu chafu kutuibia.
Madini ya Dhahabu
Mheshimiwa Spika,uchambuzi wa Kamati umebaini kuwa migodi mikubwa ya dhahabu nchini hailipi kodi ya mapato (Corporate tax) kwa kisingizio cha kupata hasara endelevu katika uzalishaji. Hata hivyo kamati haikubaliani na sababu hiyo kwani taarifa zinaonesha kwamba makapuni yanayomiliki migodi hiyo yamekuwa yakipata faida kwenye masoko ya hisa ambako kampuni hizi zimesajiliwa.
Aidha, Ripoti ya TMAA ya mwaka 2015 inaonesha kwamba makapuni ya madini ya dhahabu hayakulipa jumla ya shilingi bilioni 10.27 kwaajili ya ushuru wa Huduma (Service Levy), na Mrabaha (Royalty) kwenye Halmashauri husika. Kamati inaitaka Serikali ifuatilie malipo ya tozo hizo.
Mheshimiwa Spika, Kamati inasikitishwa na ulipaji mbovu wa kodi kwa mgodi wa ACACIA (zamani Baarick gold na African Barrick Gold) kwa kutolipa kodi ya zuio (Withholding Tax) na kodi ya mapato(Corporate Tax) kwa miaka minne hata baada ya kuamriwa na mahakama ya usuluhishi kulipa kodi hiyo inayofikia jumla ya shilingi bilioni 89.
Kamati inaitaka Serikali kuchukua hatua madhubutu juu ya mwenendo huo. Ili iweze kudhibiti ukosefu wa mapato kama ilivyotokea kwenye migodi ya Resoultena Tulawaka ambayo ilifunga shughuli za uchimbaji bila kulipa kodi stahiki[QUOTE/]
TAARIFA YA KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI 20 May, 2016 - Bukombe sasa