Kamati ya Bunge yaijia juu serikali kuhusu kampuni ya mizigo

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
803
Kamati ya Bunge yaijia juu serikali kuhusu kampuni ya mizigo

Andrew Msechu na Glory Kimathi


KAMATI ya Bunge ya Miundombinu imeitaka serikali kusitisha mara moja mkataba na Kampuni inayosimamia Kitengo cha Makontena katika Bandari ya Dar es Salaam (TICTS) ulioongezwa kabla ya kumalizika kwa mkataba wa kwanza wa miaka kumi utakaomalizika mwaka 2010.

Wajumbe wa kamti hiyo ambao ni wabunge pia wameitaka serikali kuweka wazi wamiliki wa na kujitetea iwapo haihusiki na kuongezwa kwa mkataba wa kampuni hiyo kinyume cha utaratibu.

Katika kikao cha kamati hiyo na viongozi wa Wizara ya Miundombinu na TICTS kilichofanyika Ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam jana, wabunge hao walitaka mkataba wa miaka 15 ulioongezwa kabla ya kumalizika kwa mkataba wa awali na kwamba wapewe maelezo ya kina kabla hawajaamua kupeleka hoja binafsi bungeni kuhusu utata wa mkataba huo.

Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango alisema mkataba huo uliolazimishwa kuongezewa muda wakati chama chake kikiwa katika harakati za kampeni za uchaguzi mwaka 2005 unaonyesha kukiukwa kwa taratibu na kuleta mashaka juu ya walioamua kusimamia kuongeza muda wa mkataba huo.

Alisema mkataba wa awali uliosainiwa mwaka 2000 ulishaonekana kuwa na matatizo makubwa ya kiutendaji hata kabla ya kumaliza nusu ya muda wake wa awali, uliongezwa kwa muda wa miaka mingine 15 kinyume na utaratibu na kuufanya ufikie miaka 25.

"Suala ninalogundua hapa ni ubovu wa mkataba huu, leo tuko hapa utendaji wake hauridhishi, kinachoniuma zaidi na hatua ya PSRC kutueleza wazi hapa kuwa si wao walioongeza muda wa mkataba huo kabla ya wakati, bali ni amri iliyotoka juu. Tunataka serikali iuangalie upya mkataba huu na iondoe miaka15 iliyoongezwa," aliema Kilango.

Aliongeza kuwa hadaa nyingine iliyowekwa katika mkataba huo ni hatua ya kuitaka TICTS kuendelea kuendesha kitengo hicho cha makasha hadi watakapohakikisha kuwa kinakuwa na uwezo wa kupitisha makontena 600,000 ndipo makampuni mengine yaweze kuruhusiwa kuingia kwenye ushindani.

"Tunaitegemea bandari hasa ya Dar es Salaam kuwa chanzo kikuu cha mapato ya nchi, lakini katika kipindi hiki cha utandawazi, tunaona wazi kuwa makampuni mengine yanabanwa kwa makusudi na TICTS imepewa nafasi ya kuhodhi shughuli hizi kwa kipindi kisichojulikana na zaidi kuna mianya wa mapato ya ziada, kila kontena linatozwa dola 80 za kimarekani kwa siku 19, lakini serikali hapa inapata dola 15 tu" alisema Kilango.

Mbunge wa Rorya Profesa Philemon Sarungi aliungana na Kilango akidai kuwa TICTS imepuuza kauli ya Waziri Mkuu kutaka kuondolewa kwa msongamano wa makontena kwa kufanya kazi kwa masaa 24 kwa siku zote saba za wiki, lakini pamoja na Wizara kueleza kuwa zoezi hilo limeshindikana bado wananchi hawajaelezwa.

"Sisi tunajua kuwa kauli yoyote ya kiongozi ni amri inayotakiwa kuingia kwenye utekelezaji, lakini suala la muhimu hapa tukubalaiane, tuelezwe kuwa ni lini serikali inatarajia kuupitia na kuuboresha mkataba huu wa TICTS," alisema Sarungi.

Mbunge wa Mbozi Mashariki Godfrey Zambi alisema kufuatia mazingira ya kuharakishwa kuongezwa kwa mkataba huo, mazingira yanayonyesha kuwa ni mradi wa wakubwa fulani walioamua kuhakikisha kuwa wanafanya kila linalowezekana ili uendelee kuwepo kwa muda huo, hasa baada ya kuhisi kuwa huenda wasiendelee kuwepo serikalini baada ya mwaka 2005.

"Iwapo hatutapewa maelezo mazuri na wizara hii, mimi nitakuwa wa kwanza kuikataa bajeti yake, lakini suala la msingi ni kuondolewa kwa miaka hii 15 iliyoongezwa kinyemela na tupitie upya utendaji wa TICTS, kama unaturidhisha si tutaongeza tu mkataba wana wasiwasi gani?" alisema.

Katika kikao hicho chini ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, mbunge wa Singida Kusini Mohamed Misanga, Mbunge wa Ruangwa Gogfrid Ng'itu alibainisha kuwa mkataba huo wa TICTS ni moja ya mikataba yenye utata mkubwa na kuitaka wizara kukiri kupokea barua ya kuongeza mkataba huo.

"Mkataba huu ni Richmond na Buzwagi nyingine, hili liko wazi, tumetaka sana kama wabunge tuonyeshwe mkataba huu lakini tunaambiwa kwua tutakuwa tumeingia jikoni, sasa tusipouona sisi wawakilishi wa wananchi wanataka wauone akina nani, hapo ndipo uoza unapoanzia hivyo ni lazima mikataba ya aina hii iwe wazi na sisi wabunge tuweze kuipitia na kuithibitisha katika hatua za mwanzo," alisisitiza.

Awali, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Batholomew Lufunjo aliwaeleza wabunge hao kuwa pamoja na seriali kuamua kuiongezea kampuni hiyo mkataba huo bado ipo kwenye mchakato wa namna ya kuboresha mkataba huo wa TICTS ili uwe na vigezo vingi zaidi vya utendaji ili kuongeza ufanisi.

Alipotakiwa kujibu hoja hizo alisema dhumuni la kuongeza muda huo lilitokana na utendaji mzuri wa TICTS, jibu ambalo lililopingwa na wabunge hao wakidai kuwa hakukuwa na sababu ya kuharakisha utekelezaji wa suala hilo.

Hata hivyo Naibu Katibu Mkuu huyo alisema yeye hana majibu ya uhakika atakayowaridhisha wabunge hao, na kudai kuwa Waziri wa Miundombinu ndiye anayeweza kuwapa majibu sahihi.

Mkataba huo ulioanza mwaka 2000 ulitakiwa kumalizika mwaka 2010 lakini uliongezewa miaka 15 mwaka 2005, hivyo kuufanya umalizike mwaka 2025, pia kuongezewa sehemu ya kuhifadhi makontena pamoja na kupewa yadi Ubungo.


Source: Mwananchi
 
I love you Anne Kilango Malecela maana una busara mno na uchungu na Nchi . Si katika hili pekee nakutambua hata Bungeni na ulikuwa mmoja wa wabunge wa CCM walio kataa dhuluma ya Zitto kupewa fukuzo la kijinga kwa hoja yake. I love you mama when it come on serious issues za Nchi unamzidi mumeo mbali kabisa .
 
Napenda kumpongeza Huyo Mbunge kwa kuuliza maswali ya msingi, sasa asiishie kupewa kitu kidogo au cheo yakaisha. kuna ile post ya Marehemu Salome Mbatia, Ni vizuri aangalie long term investment nayo ni kuwatumikia watu wake. Sio Pesa?
 
I can bet on this Mama . She is real na siamini kwamba anaamini katika kuzimwa .No she has a very outspoken zaidi hata ya Malecela .Ndani ya CCM sisi wenyewe tuna wasi wasi kwamba ni Mpinzani lakini tukitulia tunaona ana nia njema zaidi ya Rais wetu wa CCM yetu .
 
Sidhani kuna haja ya kumpongeza at all, hawa wabunge ni kazi yao ambayo imekuwa overdue.Tukumbuke kuwa hayo ni majukumu yao ya kikatiba, siku zote wametakiwa kufanya hivyo na kuweka kando mambo ya kulindana ki-CCM, nani hajui wanamwogopa Karamagi ambaye kila kukicha anahusika na kashfa ya kurudisha nyuma jitihada za watanzania kimaendeleo?.

Sababu ya ku-discourage kumpongeza Mama Kilango ni moja, ataongea na yataishia hapo hapo bandarini wakati efficiency ikishuka kila wakati, bunge tunalo, kwanini haliweki msimamo na kudhibiti hii hali isitokee tena.Imagine majibu ya huyo katibu mkuu wa wizara husika alichokisema, eti wanaboresha mkataba....hapo hoja ni equipment, expertise na performance.Mambo ya kupongezana kwa maneno matupu hayatufikishi kokote..

Tanzania kwa nafasi iliyonayo, wakati huu wa matatizo ya Kenya ilitakiwa kuchukua biashara ya mizigo yote iliyokuwa inapita bandari ya Mombasa, inayokwenda na kutoka landlocked countries kama Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Hatuwaombei matatizo jirani zetu Kenya, lakini katika biashara hizi Kenya wametumia matatizo yetu kujijenga zaidi.

Haya mambo yote yapo ndani ya uwezo wa bunge letu, iwasilishwe hoja ndani ya bunge mkataba wa hiyo kampuni ya Karamagi ufutwe zipewe kampuni zenye vifaa na uwezo wa kufanya kazi - pamoja na rekodi ya miaka zaidi ya 10 katika kuendesha kitengo cha makontena bandarini.

Lakini kwa kuwa na uendeshaji mdogo wa bandari zetu, tunashindwa hata kupitisha mizigo yetu wenyewe kwa ufanisi.
 
"Suala ninalogundua hapa ni ubovu wa mkataba huu, leo tuko hapa utendaji wake hauridhishi, kinachoniuma zaidi na hatua ya PSRC kutueleza wazi hapa kuwa si wao walioongeza muda wa mkataba huo kabla ya wakati, bali ni amri iliyotoka juu. Tunataka serikali iuangalie upya mkataba huu na iondoe miaka15 iliyoongezwa," aliema Kilango.


Hii nayo ni Source moja ya Fedha haramu ya SISIEMU mwaka 2005 ilo vunwa kiharamu ili kukidhi hamu yake chafu ya kushinda uchaguzi kwa hila za Mbweha mwenye njaa na hasira.

Huyo mtu aliye juu aliyetoa amri ya kuongeza mkataba atajwe. Ni nani huyo kama siyo SISIEMU chenyewe na Rais wa nchi?

Sisi Wananchi tutendelea kusitsista kuchukua hatua madhubuti dhidi ya Mharamia hawa wa SISIEMU mpaka lini?

Mungu humsaidia ajisaidiaye.
Kila Mtanzania Yuko BIZE kufukuza shilingi huku akiacha shilingi zilizo halali yake za kufaidi bila kuzifukuza zikiibiwa na na SISIEMU.

Hicho kilio cha ajira ni vema tukililie ndani ya sanduku la kura.Pia tusisahau kulilinda sanduku la kura kwa nguvu zetu zotezisiibiwe na nduli SISIEMU.
 
Mhmm!! naona kila mtu anaruka kupitia dirishani. JK jiangalie usije ukabaki peke yako kwenye gari. Hivi ule utaratibu wa collective responsibility ulishakufa?
 
Acheni wale! nani hapendi kula? Hata wewe ukipewa sii utakula? Leo JF mko hapa kulalamika kwa vile mko out of System! Mwai Kibaki alikuwa analilia hivi tangu zamani ilipofika 2002 akaanza naye kula- leo Kenya iko wapi?

Msiwaonee wivu- if you can not fight them join them!

Acheni wivu- wivu kitu mbaya!
 
Acheni wale! nani hapendi kula? Hata wewe ukipewa sii utakula? Leo JF mko hapa kulalamika kwa vile mko out of System! Mwai Kibaki alikuwa analilia hivi tangu zamani ilipofika 2002 akaanza naye kula- leo Kenya iko wapi?

Msiwaonee wivu- if you can not fight them join them!

Acheni wivu- wivu kitu mbaya!

Kigeu geu are you serious??? unadhani ukila tu bila kufikilia kesho si hata unachokula kitafikia mahali kiishe??? C'on man, you can do better tha this!
 
Kigeu geu are you serious??? unadhani ukila tu bila kufikilia kesho si hata unachokula kitafikia mahali kiishe??? C'on man, you can do better tha this!


Rwabingiri,

Mimi nimekuwa mkweli kama binadamu taabu ya wengi wetu hapa tuu wanaafiki! Sii mawaziri wengi tu vijana walikuwa wanapinga sana ulaji siku za nyuma sasa wamepewa nafasi na JK na wapo kimya na sasa nao wanakula? Kama ni vibaya wanavyofanya ni swala lingine. Ukweli ni huo watu wanatesa kwa zamu!

Kila mtu anapenda kula kusidanyanyane!
 
wabunge hao walitaka mkataba wa miaka 15 ulioongezwa kabla ya kumalizika kwa mkataba wa awali na kwamba wapewe maelezo ya kina kabla hawajaamua kupeleka hoja binafsi bungeni kuhusu utata wa mkataba huo. mkataba huo uliolazimishwa kuongezewa muda wakati chama chake kikiwa katika harakati za kampeni za uchaguzi mwaka 2005 unaonyesha kukiukwa kwa taratibu na kuleta mashaka juu ya walioamua kusimamia kuongeza muda wa mkataba huo. Alisema mkataba wa awali uliosainiwa mwaka 2000 ulishaonekana kuwa na matatizo makubwa ya kiutendaji hata kabla ya kumaliza nusu ya muda wake wa awali, uliongezwa kwa muda wa miaka mingine 15 kinyume na utaratibu na kuufanya ufikie miaka 25. "Suala ninalogundua hapa ni ubovu wa mkataba huu, leo tuko hapa utendaji wake hauridhishi, kinachoniuma zaidi na hatua ya PSRC kutueleza wazi hapa kuwa si wao walioongeza muda wa mkataba huo kabla ya wakati, bali ni amri iliyotoka juu.

Amri ilitoka kwa Mkapa niliyasema haya wiki tatu zilizopita, akiwa rais aliamuru kumuongezea muda Karamagi na kampuni yake for 25 years, halafu kuna wanaosema kuwa Balali anahitaji kinga, hivi huu sio ushahidi wa kutosha kumfikisha Mkapa kortini?
 
Naona hata wabunge wa CCM 'uzalendo" unawashinda.Aliposema Zitto na Slaa walisema watovu wa nidhamu.Sasa unapoona mpaka mtu kama Sarungi aliyewahi kuwa waziri wa mawasiliano na uchukuzi anasema hivyo na huyu mama K anakuja juu ujue kazi ipo.
 
..damn miaka 25 ya contract,this is more than ufisadi yaani katika dola 80 sisi tunaambuia 15,na Field marshal kama nimekupata vizuri una maana hiyo ni kampuni ya Karamagi au? aiseeh sasa nimeanza kuamini kuna watu wame jiposition kula ile nchi milele,na mkapa kama hili nalo ni kweli ndugu yetu wewe ni mtu mbaya sana na huna huruma na nchi yetu na sisi hatutakuwa na huruma na wewe...subirini watu walivalie njuga hili muone watu watakavyoaibika.
 
Rwabingiri,

Mimi nimekuwa mkweli kama binadamu taabu ya wengi wetu hapa tuu wanaafiki! Sii mawaziri wengi tu vijana walikuwa wanapinga sana ulaji siku za nyuma sasa wamepewa nafasi na JK na wapo kimya na sasa nao wanakula? Kama ni vibaya wanavyofanya ni swala lingine. Ukweli ni huo watu wanatesa kwa zamu!

Kila mtu anapenda kula kusidanyanyane!

Subiri saa ya Kuteswa Kwa Zamu ikifika.
 
Rwabingiri,

Mimi nimekuwa mkweli kama binadamu taabu ya wengi wetu hapa tuu wanaafiki! Sii mawaziri wengi tu vijana walikuwa wanapinga sana ulaji siku za nyuma sasa wamepewa nafasi na JK na wapo kimya na sasa nao wanakula? Kama ni vibaya wanavyofanya ni swala lingine. Ukweli ni huo watu wanatesa kwa zamu!

Kila mtu anapenda kula kusidanyanyane!

Si mkweli kwenye hili. Si KILA mtu anapenda kula. Wengi, ndio lakini si kila mtu. Amini usiamini hata Nigeria kuna watu wangepewa nafasi wasingekula. Nchi iliyomtoa Abacha ilimtoa Murtala. Hapo kwetu wako wengi tu waliofanya na wengine wanaendelea kazi zao kiadilifu bila KULA. Bahati mbaya watu wengi katika jamii wanawaona wajinga na hawaenziwi. Wapo.ndugu yangu. Wapo. Tusikate tamaa.
 
Huyu mama akikumbuka maandalizi yake ya kuwa "FirstLady" na pindua ya CCM anaishiwa hamu hivyo kuamua kuwa upande wa akina yakhe. Ingawa anasema ukweli.
 
Kigeugeu!! Wahaya wana msemo ati jina baya humharibu mwenye jina. Yaani matendo ya mtu hufuata jina lake. Kigeugeu ameonyesha hivyo, naye ni fisadi maana amesema if you can't fight them, join them. Aibu.
 
Huyu mama akikumbuka maandalizi yake ya kuwa "FirstLady" na pindua ya CCM anaishiwa hamu hivyo kuamua kuwa upande wa akina yakhe. Ingawa anasema ukweli.

Inafurahisha sana statement yako!
Inasemekana Mama Malecela alikuwa anataka kuwa na "EOTF" yake na yeye mara mumewe akiingia ikulu. Mumewe kabanwa mbavu na Mkapa, nahani ndio ikawa mwisho wa ndoto zake!
Hata hivyo nampa big up kwa utetezi aliofanya katika maelezo ya thread hii hapo juu!
 
Back
Top Bottom