Kamati ya Bashe UVCCM kupasua jipu leo Dodoma, ripoti yasakwa ihujumiwe...

Mwana Mpotevu

Platinum Member
Sep 7, 2011
3,295
2,500
Vigogo CCM wahaha kupata Ripoti Kamati ya Bashe

BAADHI ya vigogo wa CCM na wale wa Umoja wa Vijana wa chama hicho, (UVCCM) jana walikuwa wakihaha kupata ripoti ya kamati iliyoundwa Machi mwaka jana kutathmini namna ya kuuhuisha umoja huo inayotarajiwa kuwasilishwa leo katika kikao cha Baraza Kuu la UVCCM.

Taarifa kutoka ndani ya kikao ambazo zilithibitishwa na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo maarufu kama ‘Kamati ya Bashe', zilieleza kuwa vijana na vigogo wa chama hicho walikuwa na shauku ya kuiona ripoti hiyo ambayo inasemekana imesheheni mambo mazito kabla haijawasilishwa ili wajue namna ya kuizuia au kujipanga kwa kutoa maoni yao.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vililidokeza Mwananchi Jumapili kuwa ripoti hiyo inatarajiwa kuja na mageuzi makubwa ndani ya Jumuiya ya Vijana pamoja na CCM kwa ujumla na kwamba kutovuja kwa kilichopendekezwa humo, kumeibua maswali mengi kwa wajumbe.

Hata hivyo, chanzo chetu kutoka ndani ya chama hicho kimedokeza kuwa moja ya mapendekezo ya kamati hiyo ni pamoja na kuutaka Umoja huo kujisimamia na kuondokana na kuwa ‘Jumuiya ya kuimba Iyena iyena.'
Mengine ni pamoja na kuwa katika mageuzi makubwa ambapo wanataka Jumuiya ambayo italeta mabadiliko ya kiuchumi pamoja na mikakati na misimamo ya ndani ya chama ambayo kwa sehemu inawagusa vigogo.

Pia kamati hiyo inapendekeza uchumi wa nchi kumilikiwa na wazawa yaani wananchi washiriki katika kumiliki raslimali na kwamba kazi hiyo isiachwe kwa wawekezaji wa kigeni pekee.

Kwa mujibu wa msemaji wetu, hadi jana mchana kulikuwa na mgawanyiko wa makundi matatu katika Baraza hilo.
Kundi moja liliongozwa na mtoto wa kigogo ambaye ni mjumbe kutoka Mkoa wa Pwani huku kundi lingine likiwa ni vijana waliotumwa na uongozi kwa ajili ya kuhakikisha wanaunasa waraka huo kabla ya kuingizwa mkutanoni leo hii.
Kundi la tatu ni lile linalojiita ‘Wapenda haki' ambalo ndilo linalojua nini kilichopendekezwa na Kamati ya Bashe na ndilo hasa lililoonekana kuwa na furaha kubwa huku likiapa kutotolewa taarifa hiyo hadi itakapowasilishwa leo ukumbini.

"Tumeapa na tuko tayari kuifia imani yetu, hawa jamaa hawawezi kuiona ripoti hiyo maana kuna ujanja wanataka kuufanya na kurubuni wajumbe, hivyo lazima tuwe makini na mambo hayo,'' alisema mmoja wa wajumbe.

Kauli ya msemaji huyo haikuwa na tofauti na kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bashe ambaye jana alisema kuwa hakuwa na la kusema, lakini akakiri kuwa kuna usiri mkubwa katika kamati yake.

"Kimsingi sisi tutaiwasilisha kesho (leo) saa 9 alasiri, kwa hiyo naomba msubiri wala msiwe na haraka, ndiyo maana unaona wajumbe wa kamati yangu hawaonekani sana pale ukumbini,'' alisema Bashe.

Bila ya kutaja nini kilichomo ndani ya ripoti yao, alisema kuwa wanaCCM na vijana watarajie kuona mambo makubwa ambayo kimsingi yatakuwa na lengo kamili la kuujenga UVCCM pamoja na CCM kwa jumla.

MY TAKE:
Tusubiri mpasuko mwingine UVCCM baada ya NEC yao kupasuka pia
 
Malisa amesema kuwa sasa UVCCM itaanza kujibu mapigo yote ya wapinzani maana wamechoka kuvumilia matusi ya wapinzani.
 
malisa hana jeur hiyo na kund laki kujibu mapigo mkuu, watabak tu kupeawa hela na EL, alafu ujue kama viongoz wa kitaifa weng wa uvmagamba hawajui politics hata kidogo alafu n vilaza mno
 
Ndio kwanza namsikia huyo malisa ataanzia wapi? Badala ya kutekeleza yale maisha bora walio ahidi wananchi yeye anasubiri kujibu mapingo kweli CCM inafuga vichaa
 
Malisa amesema kuwa sasa UVCCM itaanza kujibu mapigo yote ya wapinzani maana wamechoka kuvumilia matusi ya wapinzani.

Huyo Malissa kweli fikra na akili zake ni sawa na za wengi ya wana c.c.m walivyo,hv wapinzani wanatukana au wanatoa hoja ambazo zinawagusa moja kwa moja wananchi hasa kutokana na hali halisi ya nchi ilivyo?kama ni matusi basi c.c.m wangeshnda kwa kishindo Arumeru!maisha ni magumu sana,na wananchi are feeling the pinch,inflation inatisha,rasilimali zinaporwa na kugawiwa bure tu,kwa nini wananchi wasiwaamini wapinzani kwa kuona wanawapa mwanga wa matumaini japo hawajashka dola??wananchi hawana mpango wa kusikiliza matusi na porojo,kama U.v.c.c.m wanawaza hivyo kwa nini wasianzishe kundi la taarabu tu?
 
Hawa wasipojipanga wataishia kuwa waimba kwaya wa NEC na CC kwa ujumla!!mwanzo wa mwisho wao unakaribia......hayo mapendekezo kama hawatakubalioana kuungana na kuacha tofauti zao...wana magwanda watawaapasua vichwa hadi 2015 wakiingia ikulu ndio kabisa UVnYnYM itajifia usingizini bila shida
 
Vigogo CCM wahaha kupata Ripoti Kamati ya Bashe

BAADHI ya vigogo wa CCM na wale wa Umoja wa Vijana wa chama hicho, (UVCCM) jana walikuwa wakihaha kupata ripoti ya kamati iliyoundwa Machi mwaka jana kutathmini namna ya kuuhuisha umoja huo inayotarajiwa kuwasilishwa leo katika kikao cha Baraza Kuu la UVCCM.

Taarifa kutoka ndani ya kikao ambazo zilithibitishwa na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo maarufu kama ‘Kamati ya Bashe’, zilieleza kuwa vijana na vigogo wa chama hicho walikuwa na shauku ya kuiona ripoti hiyo ambayo inasemekana imesheheni mambo mazito kabla haijawasilishwa ili wajue namna ya kuizuia au kujipanga kwa kutoa maoni yao.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vililidokeza Mwananchi Jumapili kuwa ripoti hiyo inatarajiwa kuja na mageuzi makubwa ndani ya Jumuiya ya Vijana pamoja na CCM kwa ujumla na kwamba kutovuja kwa kilichopendekezwa humo, kumeibua maswali mengi kwa wajumbe.

Hata hivyo, chanzo chetu kutoka ndani ya chama hicho kimedokeza kuwa moja ya mapendekezo ya kamati hiyo ni pamoja na kuutaka Umoja huo kujisimamia na kuondokana na kuwa ‘Jumuiya ya kuimba Iyena iyena.’
Mengine ni pamoja na kuwa katika mageuzi makubwa ambapo wanataka Jumuiya ambayo italeta mabadiliko ya kiuchumi pamoja na mikakati na misimamo ya ndani ya chama ambayo kwa sehemu inawagusa vigogo.

Pia kamati hiyo inapendekeza uchumi wa nchi kumilikiwa na wazawa yaani wananchi washiriki katika kumiliki raslimali na kwamba kazi hiyo isiachwe kwa wawekezaji wa kigeni pekee.

Kwa mujibu wa msemaji wetu, hadi jana mchana kulikuwa na mgawanyiko wa makundi matatu katika Baraza hilo.
Kundi moja liliongozwa na mtoto wa kigogo ambaye ni mjumbe kutoka Mkoa wa Pwani huku kundi lingine likiwa ni vijana waliotumwa na uongozi kwa ajili ya kuhakikisha wanaunasa waraka huo kabla ya kuingizwa mkutanoni leo hii.
Kundi la tatu ni lile linalojiita ‘Wapenda haki’ ambalo ndilo linalojua nini kilichopendekezwa na Kamati ya Bashe na ndilo hasa lililoonekana kuwa na furaha kubwa huku likiapa kutotolewa taarifa hiyo hadi itakapowasilishwa leo ukumbini.

“Tumeapa na tuko tayari kuifia imani yetu, hawa jamaa hawawezi kuiona ripoti hiyo maana kuna ujanja wanataka kuufanya na kurubuni wajumbe, hivyo lazima tuwe makini na mambo hayo,’’ alisema mmoja wa wajumbe.

Kauli ya msemaji huyo haikuwa na tofauti na kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bashe ambaye jana alisema kuwa hakuwa na la kusema, lakini akakiri kuwa kuna usiri mkubwa katika kamati yake.

“Kimsingi sisi tutaiwasilisha kesho (leo) saa 9 alasiri, kwa hiyo naomba msubiri wala msiwe na haraka, ndiyo maana unaona wajumbe wa kamati yangu hawaonekani sana pale ukumbini,’’ alisema Bashe.

Bila ya kutaja nini kilichomo ndani ya ripoti yao, alisema kuwa wanaCCM na vijana watarajie kuona mambo makubwa ambayo kimsingi yatakuwa na lengo kamili la kuujenga UVCCM pamoja na CCM kwa jumla.

MY TAKE:
Tusubiri mpasuko mwingine UVCCM baada ya NEC yao kupasuka pia

kaaazi kweli kweli,,,kumbe vijana kazi yao ni ndio mzeeeee......
Huyo mtoto wa kigogo ni nani????kutoka pwani????riz-1 nini????
Yaani na sisiem kuna wapigania haki????na walio tayar kufa????nani asojua kuwa rasilimali not 4 us????tume kibao zimeundwa hakuna jipya hapo,,,,
 
kaaazi kweli kweli,,,kumbe vijana kazi yao ni ndio mzeeeee......
Huyo mtoto wa kigogo ni nani????kutoka pwani????riz-1 nini????
Yaani na sisiem kuna wapigania haki????na walio tayar kufa????nani asojua kuwa rasilimali not 4 us????tume kibao zimeundwa hakuna jipya hapo,,,,

wameshasema mtoto wa kigogo na mjumbe toka mkoa wa pwani, wameshindwa nini kumalizia na jina tu maana kila kitu wameshakisema.
 
uvccm ni kama kurugenzi ndani ya wizara flani,sasa kuna kurugenzi inaweza kutoa taarifa kwa vyombo vya habari bila mtendaji mkuu wa wizara kujua?unajua maana ya kuhaha?wakiitaka taarifa wanaipata tu,asikudanganye mtu!
 
Hakuna kitu hapo Bashe bado ana uchungu wa kuumbuliwa uraia.
 
Vigogo CCM wahaha kupata Ripoti Kamati ya Bashe

BAADHI ya vigogo wa CCM na wale wa Umoja wa Vijana wa chama hicho, (UVCCM) jana walikuwa wakihaha kupata ripoti ya kamati iliyoundwa Machi mwaka jana kutathmini namna ya kuuhuisha umoja huo inayotarajiwa kuwasilishwa leo katika kikao cha Baraza Kuu la UVCCM.

Taarifa kutoka ndani ya kikao ambazo zilithibitishwa na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo maarufu kama ‘Kamati ya Bashe', zilieleza kuwa vijana na vigogo wa chama hicho walikuwa na shauku ya kuiona ripoti hiyo ambayo inasemekana imesheheni mambo mazito kabla haijawasilishwa ili wajue namna ya kuizuia au kujipanga kwa kutoa maoni yao.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vililidokeza Mwananchi Jumapili kuwa ripoti hiyo inatarajiwa kuja na mageuzi makubwa ndani ya Jumuiya ya Vijana pamoja na CCM kwa ujumla na kwamba kutovuja kwa kilichopendekezwa humo, kumeibua maswali mengi kwa wajumbe.

Hata hivyo, chanzo chetu kutoka ndani ya chama hicho kimedokeza kuwa moja ya mapendekezo ya kamati hiyo ni pamoja na kuutaka Umoja huo kujisimamia na kuondokana na kuwa ‘Jumuiya ya kuimba Iyena iyena.'
Mengine ni pamoja na kuwa katika mageuzi makubwa ambapo wanataka Jumuiya ambayo italeta mabadiliko ya kiuchumi pamoja na mikakati na misimamo ya ndani ya chama ambayo kwa sehemu inawagusa vigogo.

Pia kamati hiyo inapendekeza uchumi wa nchi kumilikiwa na wazawa yaani wananchi washiriki katika kumiliki raslimali na kwamba kazi hiyo isiachwe kwa wawekezaji wa kigeni pekee.

Kwa mujibu wa msemaji wetu, hadi jana mchana kulikuwa na mgawanyiko wa makundi matatu katika Baraza hilo.
Kundi moja liliongozwa na mtoto wa kigogo ambaye ni mjumbe kutoka Mkoa wa Pwani huku kundi lingine likiwa ni vijana waliotumwa na uongozi kwa ajili ya kuhakikisha wanaunasa waraka huo kabla ya kuingizwa mkutanoni leo hii.
Kundi la tatu ni lile linalojiita ‘Wapenda haki' ambalo ndilo linalojua nini kilichopendekezwa na Kamati ya Bashe na ndilo hasa lililoonekana kuwa na furaha kubwa huku likiapa kutotolewa taarifa hiyo hadi itakapowasilishwa leo ukumbini.

"Tumeapa na tuko tayari kuifia imani yetu, hawa jamaa hawawezi kuiona ripoti hiyo maana kuna ujanja wanataka kuufanya na kurubuni wajumbe, hivyo lazima tuwe makini na mambo hayo,'' alisema mmoja wa wajumbe.

Kauli ya msemaji huyo haikuwa na tofauti na kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bashe ambaye jana alisema kuwa hakuwa na la kusema, lakini akakiri kuwa kuna usiri mkubwa katika kamati yake.

"Kimsingi sisi tutaiwasilisha kesho (leo) saa 9 alasiri, kwa hiyo naomba msubiri wala msiwe na haraka, ndiyo maana unaona wajumbe wa kamati yangu hawaonekani sana pale ukumbini,'' alisema Bashe.

Bila ya kutaja nini kilichomo ndani ya ripoti yao, alisema kuwa wanaCCM na vijana watarajie kuona mambo makubwa ambayo kimsingi yatakuwa na lengo kamili la kuujenga UVCCM pamoja na CCM kwa jumla.

MY TAKE:
Tusubiri mpasuko mwingine UVCCM baada ya NEC yao kupasuka pia

maneno ya kutoa tamko kila siku tumewazoea! hata ambao hatuna vyama tumezidi kujidhatiti na misimamo yetu! HATUNA VYAMA aaa SINA CHAMA NA SITAKI
 
Back
Top Bottom