Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,500
Vigogo CCM wahaha kupata Ripoti Kamati ya Bashe
BAADHI ya vigogo wa CCM na wale wa Umoja wa Vijana wa chama hicho, (UVCCM) jana walikuwa wakihaha kupata ripoti ya kamati iliyoundwa Machi mwaka jana kutathmini namna ya kuuhuisha umoja huo inayotarajiwa kuwasilishwa leo katika kikao cha Baraza Kuu la UVCCM.
Taarifa kutoka ndani ya kikao ambazo zilithibitishwa na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo maarufu kama ‘Kamati ya Bashe', zilieleza kuwa vijana na vigogo wa chama hicho walikuwa na shauku ya kuiona ripoti hiyo ambayo inasemekana imesheheni mambo mazito kabla haijawasilishwa ili wajue namna ya kuizuia au kujipanga kwa kutoa maoni yao.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vililidokeza Mwananchi Jumapili kuwa ripoti hiyo inatarajiwa kuja na mageuzi makubwa ndani ya Jumuiya ya Vijana pamoja na CCM kwa ujumla na kwamba kutovuja kwa kilichopendekezwa humo, kumeibua maswali mengi kwa wajumbe.
Hata hivyo, chanzo chetu kutoka ndani ya chama hicho kimedokeza kuwa moja ya mapendekezo ya kamati hiyo ni pamoja na kuutaka Umoja huo kujisimamia na kuondokana na kuwa ‘Jumuiya ya kuimba Iyena iyena.'
Mengine ni pamoja na kuwa katika mageuzi makubwa ambapo wanataka Jumuiya ambayo italeta mabadiliko ya kiuchumi pamoja na mikakati na misimamo ya ndani ya chama ambayo kwa sehemu inawagusa vigogo.
Pia kamati hiyo inapendekeza uchumi wa nchi kumilikiwa na wazawa yaani wananchi washiriki katika kumiliki raslimali na kwamba kazi hiyo isiachwe kwa wawekezaji wa kigeni pekee.
Kwa mujibu wa msemaji wetu, hadi jana mchana kulikuwa na mgawanyiko wa makundi matatu katika Baraza hilo.
Kundi moja liliongozwa na mtoto wa kigogo ambaye ni mjumbe kutoka Mkoa wa Pwani huku kundi lingine likiwa ni vijana waliotumwa na uongozi kwa ajili ya kuhakikisha wanaunasa waraka huo kabla ya kuingizwa mkutanoni leo hii.
Kundi la tatu ni lile linalojiita ‘Wapenda haki' ambalo ndilo linalojua nini kilichopendekezwa na Kamati ya Bashe na ndilo hasa lililoonekana kuwa na furaha kubwa huku likiapa kutotolewa taarifa hiyo hadi itakapowasilishwa leo ukumbini.
"Tumeapa na tuko tayari kuifia imani yetu, hawa jamaa hawawezi kuiona ripoti hiyo maana kuna ujanja wanataka kuufanya na kurubuni wajumbe, hivyo lazima tuwe makini na mambo hayo,'' alisema mmoja wa wajumbe.
Kauli ya msemaji huyo haikuwa na tofauti na kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bashe ambaye jana alisema kuwa hakuwa na la kusema, lakini akakiri kuwa kuna usiri mkubwa katika kamati yake.
"Kimsingi sisi tutaiwasilisha kesho (leo) saa 9 alasiri, kwa hiyo naomba msubiri wala msiwe na haraka, ndiyo maana unaona wajumbe wa kamati yangu hawaonekani sana pale ukumbini,'' alisema Bashe.
Bila ya kutaja nini kilichomo ndani ya ripoti yao, alisema kuwa wanaCCM na vijana watarajie kuona mambo makubwa ambayo kimsingi yatakuwa na lengo kamili la kuujenga UVCCM pamoja na CCM kwa jumla.
MY TAKE:
Tusubiri mpasuko mwingine UVCCM baada ya NEC yao kupasuka pia
BAADHI ya vigogo wa CCM na wale wa Umoja wa Vijana wa chama hicho, (UVCCM) jana walikuwa wakihaha kupata ripoti ya kamati iliyoundwa Machi mwaka jana kutathmini namna ya kuuhuisha umoja huo inayotarajiwa kuwasilishwa leo katika kikao cha Baraza Kuu la UVCCM.
Taarifa kutoka ndani ya kikao ambazo zilithibitishwa na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo maarufu kama ‘Kamati ya Bashe', zilieleza kuwa vijana na vigogo wa chama hicho walikuwa na shauku ya kuiona ripoti hiyo ambayo inasemekana imesheheni mambo mazito kabla haijawasilishwa ili wajue namna ya kuizuia au kujipanga kwa kutoa maoni yao.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vililidokeza Mwananchi Jumapili kuwa ripoti hiyo inatarajiwa kuja na mageuzi makubwa ndani ya Jumuiya ya Vijana pamoja na CCM kwa ujumla na kwamba kutovuja kwa kilichopendekezwa humo, kumeibua maswali mengi kwa wajumbe.
Hata hivyo, chanzo chetu kutoka ndani ya chama hicho kimedokeza kuwa moja ya mapendekezo ya kamati hiyo ni pamoja na kuutaka Umoja huo kujisimamia na kuondokana na kuwa ‘Jumuiya ya kuimba Iyena iyena.'
Mengine ni pamoja na kuwa katika mageuzi makubwa ambapo wanataka Jumuiya ambayo italeta mabadiliko ya kiuchumi pamoja na mikakati na misimamo ya ndani ya chama ambayo kwa sehemu inawagusa vigogo.
Pia kamati hiyo inapendekeza uchumi wa nchi kumilikiwa na wazawa yaani wananchi washiriki katika kumiliki raslimali na kwamba kazi hiyo isiachwe kwa wawekezaji wa kigeni pekee.
Kwa mujibu wa msemaji wetu, hadi jana mchana kulikuwa na mgawanyiko wa makundi matatu katika Baraza hilo.
Kundi moja liliongozwa na mtoto wa kigogo ambaye ni mjumbe kutoka Mkoa wa Pwani huku kundi lingine likiwa ni vijana waliotumwa na uongozi kwa ajili ya kuhakikisha wanaunasa waraka huo kabla ya kuingizwa mkutanoni leo hii.
Kundi la tatu ni lile linalojiita ‘Wapenda haki' ambalo ndilo linalojua nini kilichopendekezwa na Kamati ya Bashe na ndilo hasa lililoonekana kuwa na furaha kubwa huku likiapa kutotolewa taarifa hiyo hadi itakapowasilishwa leo ukumbini.
"Tumeapa na tuko tayari kuifia imani yetu, hawa jamaa hawawezi kuiona ripoti hiyo maana kuna ujanja wanataka kuufanya na kurubuni wajumbe, hivyo lazima tuwe makini na mambo hayo,'' alisema mmoja wa wajumbe.
Kauli ya msemaji huyo haikuwa na tofauti na kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Bashe ambaye jana alisema kuwa hakuwa na la kusema, lakini akakiri kuwa kuna usiri mkubwa katika kamati yake.
"Kimsingi sisi tutaiwasilisha kesho (leo) saa 9 alasiri, kwa hiyo naomba msubiri wala msiwe na haraka, ndiyo maana unaona wajumbe wa kamati yangu hawaonekani sana pale ukumbini,'' alisema Bashe.
Bila ya kutaja nini kilichomo ndani ya ripoti yao, alisema kuwa wanaCCM na vijana watarajie kuona mambo makubwa ambayo kimsingi yatakuwa na lengo kamili la kuujenga UVCCM pamoja na CCM kwa jumla.
MY TAKE:
Tusubiri mpasuko mwingine UVCCM baada ya NEC yao kupasuka pia