Kama kweli hii kamati imeundwa na watu watakuwa serious Tanzania itakuwa imekombolewa,
Kwa kuwa huu ndio utakuwa Mwisho wa Mafisadi na serikali inayowatetea,
Source: IPP Media
Wapinzani kuwafikisha Kortini mafisadi wa EPA
2008-06-27 11:06:53
Na Simon Mhina
Wapinzani wameunda kamati maalum itakayohakikisha kwamba watu wanaodaiwa kuchukua fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) Sh. bilioni 133 wanafikishwa mahakamani.
Hatua hiyo imekuja kufuatia mvutano ulioibuka upya ndani ya Bunge kuhusu waliopora fedha hizo, ambapo sasa serikali inadai kuwa fedha hizo hazikuwa za umma isipokuwa za wafanyabiashara.
Tayari wapinzani wameunda kamati maalum ya kupambana na waporaji wa nchi ijulikanayo kama Public Interest Litigation Commitee (PILCOM) kwa ajili ya kuwaburuza mahakamani waliopora fedha hizo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jana, Mwenyekiti wa kamati hiyo, ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha Democratic, Mchungaji Christopher Mtikila, alisema lengo la kuwafikisha mahakamani watuhumiwa hao ni kulinda hadhi ya Bunge, ambayo inachezewa na kuhakikisha matrilioni ya wavuja jasho yaliyochukuliwa kijanja yanarejeshwa.
``Kazi ya kamati hii ni kuwafikisha mbele ya sheria watu wote walioshiriki katika wizi wa matrilioni ya mapesa ya nchi yetu katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na katika Hazina ya taifa letu, ili wazirejeshe fedha hizo pamoja na riba, gharama pamoja na zile walizoziweka nje ya nchi, ``alisema.
Alisema wajumbe wa kamati ya PILCOM, ni pamoja na mawakili 26, wabunge wa upinzani na wale wa CCM wenye mrengo wa kuwatetea wananchi, maaskofu pamoja na masheikh.
Hata hivyo, alisema amekubaliana na hoja zilizotolewa na wajumbe hasa wale wa dini na wabunge wa CCM kwamba kwa sasa wasitajwe kwanza.
Alisema kilichotoa msukumo wa watu wanaoipenda nchi hii kufungua kesi hiyo, ni hatua ya kujitokeza kwa kikundi kidogo cha wabunge ambao wamediriki`kuwasafisha` mafisadi bila aibu.
Alisema fedha zilizoporwa lazima zirudishwe, hivyo kwa vile Bunge limeanza kusuasua, lazima mahakama iingilie kati ili sheria ifuate mkondo wake.
Kuhusu Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Mustapha Mkulo, Mchungaji Mtikila alisema waziri huyo amekwenda kinyume na kauli ya Rais Kikwete na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda pale aliposema fedha za EPA sio za serikali.
``Kwa maneno mengine Mkulo anataka kusema Kikwete alikosea kumfukuza marehemu Balali, kama fedha sio za serikali, kwanini Rais ameunda chombo cha kiserikali kuchunguza?
Mkulo anataka kutunyamazisha au mapesa ya EPA ndiye yanazidi kutoa jeuri kwa watu kiasi hicho,``alihoji.
Aliwataka wananchi kuiunga mkono kamati hiyo, ambaye inapambana na magenge ya mafisadi, ambayo yanaogopwa hata na serikali yenyewe.
Kwa kuwa huu ndio utakuwa Mwisho wa Mafisadi na serikali inayowatetea,
Source: IPP Media
Wapinzani kuwafikisha Kortini mafisadi wa EPA
2008-06-27 11:06:53
Na Simon Mhina
Wapinzani wameunda kamati maalum itakayohakikisha kwamba watu wanaodaiwa kuchukua fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) Sh. bilioni 133 wanafikishwa mahakamani.
Hatua hiyo imekuja kufuatia mvutano ulioibuka upya ndani ya Bunge kuhusu waliopora fedha hizo, ambapo sasa serikali inadai kuwa fedha hizo hazikuwa za umma isipokuwa za wafanyabiashara.
Tayari wapinzani wameunda kamati maalum ya kupambana na waporaji wa nchi ijulikanayo kama Public Interest Litigation Commitee (PILCOM) kwa ajili ya kuwaburuza mahakamani waliopora fedha hizo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jana, Mwenyekiti wa kamati hiyo, ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha Democratic, Mchungaji Christopher Mtikila, alisema lengo la kuwafikisha mahakamani watuhumiwa hao ni kulinda hadhi ya Bunge, ambayo inachezewa na kuhakikisha matrilioni ya wavuja jasho yaliyochukuliwa kijanja yanarejeshwa.
``Kazi ya kamati hii ni kuwafikisha mbele ya sheria watu wote walioshiriki katika wizi wa matrilioni ya mapesa ya nchi yetu katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na katika Hazina ya taifa letu, ili wazirejeshe fedha hizo pamoja na riba, gharama pamoja na zile walizoziweka nje ya nchi, ``alisema.
Alisema wajumbe wa kamati ya PILCOM, ni pamoja na mawakili 26, wabunge wa upinzani na wale wa CCM wenye mrengo wa kuwatetea wananchi, maaskofu pamoja na masheikh.
Hata hivyo, alisema amekubaliana na hoja zilizotolewa na wajumbe hasa wale wa dini na wabunge wa CCM kwamba kwa sasa wasitajwe kwanza.
Alisema kilichotoa msukumo wa watu wanaoipenda nchi hii kufungua kesi hiyo, ni hatua ya kujitokeza kwa kikundi kidogo cha wabunge ambao wamediriki`kuwasafisha` mafisadi bila aibu.
Alisema fedha zilizoporwa lazima zirudishwe, hivyo kwa vile Bunge limeanza kusuasua, lazima mahakama iingilie kati ili sheria ifuate mkondo wake.
Kuhusu Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Mustapha Mkulo, Mchungaji Mtikila alisema waziri huyo amekwenda kinyume na kauli ya Rais Kikwete na Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda pale aliposema fedha za EPA sio za serikali.
``Kwa maneno mengine Mkulo anataka kusema Kikwete alikosea kumfukuza marehemu Balali, kama fedha sio za serikali, kwanini Rais ameunda chombo cha kiserikali kuchunguza?
Mkulo anataka kutunyamazisha au mapesa ya EPA ndiye yanazidi kutoa jeuri kwa watu kiasi hicho,``alihoji.
Aliwataka wananchi kuiunga mkono kamati hiyo, ambaye inapambana na magenge ya mafisadi, ambayo yanaogopwa hata na serikali yenyewe.