Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amevunja Kamati Kuu pamoja na sekretarieti ya chama hicho inayoongozwa na Katibu Mkuu, Yusuf Makamba.
Hatua hiyo imechukuliwa usiku huu na Mwenyekiti wa chama hicho,Rais Jakaya Kikwete kutokana na hali ya chama hicho kuwa mbaya katika swala zima la utendaji.
Hali bado ni tete mjini Dodoma ambako ndiko kunakoendelea kufanyika vikao vya chama hicho vilivyotanguliw a na sekretarieti na baadae Kamati Kuu.
Uamuzi huo mzito uliotolewa na Mwenyekiti wa chama hicho,Rais Jakaya Kikwete usiku huu kutokana na kufanyika kwa mambo ambayo hayakinufaishi chama zaidi zaidi yanakididimiza chama.
Hivyo ili kuhakikisha chama kinatakiwa kusimama imara na kuwa na watendaji wazuri katika chama hicho,imebidi Mwenyekiti wa chama achukue uamuzi huo ili kuhakikisha mambo yanakwenda kama yanavyostahiki kwenda.
Alipotafutwa Katibu Mkuu wa chama hicho,Yussuf Makamba hakutaka kuzungumzia lolote zaidi ya kusema kwamba "Huu ni wakati wa kulala na si wa kuzungumzia swala lolote".
Hivyo Globu ya Jamii inaendelea kutega sikio lake huko Dodoma na itaendelea kukujuza kila kitakachokuwa kinajiri toka mkoani humo.
Source: Issa Michuzi Blog
Hatua hiyo imechukuliwa usiku huu na Mwenyekiti wa chama hicho,Rais Jakaya Kikwete kutokana na hali ya chama hicho kuwa mbaya katika swala zima la utendaji.
Hali bado ni tete mjini Dodoma ambako ndiko kunakoendelea kufanyika vikao vya chama hicho vilivyotanguliw a na sekretarieti na baadae Kamati Kuu.
Uamuzi huo mzito uliotolewa na Mwenyekiti wa chama hicho,Rais Jakaya Kikwete usiku huu kutokana na kufanyika kwa mambo ambayo hayakinufaishi chama zaidi zaidi yanakididimiza chama.
Hivyo ili kuhakikisha chama kinatakiwa kusimama imara na kuwa na watendaji wazuri katika chama hicho,imebidi Mwenyekiti wa chama achukue uamuzi huo ili kuhakikisha mambo yanakwenda kama yanavyostahiki kwenda.
Alipotafutwa Katibu Mkuu wa chama hicho,Yussuf Makamba hakutaka kuzungumzia lolote zaidi ya kusema kwamba "Huu ni wakati wa kulala na si wa kuzungumzia swala lolote".
Hivyo Globu ya Jamii inaendelea kutega sikio lake huko Dodoma na itaendelea kukujuza kila kitakachokuwa kinajiri toka mkoani humo.
Source: Issa Michuzi Blog