Kamati Kuu ya CCM - Mtego unasao?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Wiki chache zijazo, Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi itakutana katika kikao chake cha Kawaida huko Butiama. Kikao hicho ambacho kitatangulia kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM bila ya shaka kati ya mambo mengi ambayo itajikuta inakabiliwa nayo ni mgongano wa wazi ndani ya Chama hicho ambao umetokea baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa na malumbano kati ya baadhi ya viongozi wa chama hicho na chombo cha Bunge ambacho chama hicho hicho kinaongoza.

Kwa mujibu wa Katiba ya CCM Kamati Kuu ya CCM ina jukumu la "Kutoa uongozi wa siasa nchini" na hivyo bila ya shaka wajumbe wa Kamati hiyo wanaangalia kwa ukaribu maendeleo ya wanachama wake na hasa mpasuko wa wazi na ushindani wa wazi ambapo siyo tu unamuweka kwenye shabaha Rais (ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa) bali pia unagusa maslahi ya watu wengi ambao wana maslahi tofauti kupitia chama hicho.

Kwa kuangalia historia ya Kamati Kuu ni wazi kuwa chombo hicho bado kina nguvu ya kuweza kuingilia jambo lolote na wana uwezo wa kumchukulia hatua mwanachama wao yeyote yule ambaye siyo tu anatishia maslahi ya chama hicho bali pia anatishia hali ya mwelekeo wa kisiasa nchini.

Ni kwa sababu hiyo sitoshangaa kabisa endapo Mbunge wa Monduli Bw. Edward Lowassa akapewa karipio kali na akileta "zake" kuvuliwa uanachama kwa mujibu wa Ibara ya 110:7.

Historia ya CCM inaonesha kuwa hawakusita kuwachukulia hatua watu kama Aboud Jumbe, Seif Sharrif Hamad na wenzake, Horace Kolimba na viongozi kadha wa kadha pale inapobidi. Kwa mtu anafikiri kuwa ni popular kama Lowassa atafanya makosa makubwa sana kudhani kuwa mashabiki wake wa chini watasimama mbele ya Kamati hiyo. Kama nilivyosema miezi michache iliyopita, shoka limekwisha inuliwa; na Lowassa kwa makusudi amejilengesha kama shina la mti; Endapo Lowassa hatafyata mapema (sitarajii) kuna uwezekano mkubwa wa kuchukuliwa hatua kali na lile jinamizi liitwalo "nidhamu ya chama" na sitoshangaa akachukuliwa hata hatua ya kuvuliwa uanachama!!

You heard it first... !!

Lakini swali ambalo ni la kujibiwa kabla ya kufika huko ni je JK anaweza kuleta mizengwe ya kiCCM na kutumia fimbo yake ya Uenyekiti wa CCM kuvunja daima urafiki wake na Lowassa? Kwa upande wa Lowassa swali analohitaji kujibu kabla ya kugongana na KK ni je anakubalika kiasi gani kwa wananchi wa kawaida kiasi cha kuweza kumrudisha Bungeni kwa tiketi ya chama kingine chochote kile?

Ndugu zangu, naogopa yawezekana tunashuhudia kuanguka na kufutika kwa Lowassa katika uongozi wa Tanzania. Tunasubiri kuona nani ata mcheck mate mwenzie!!
 
Lowassa anaelekea kwenye kapu la historia. Sidhani kama anao ujasiri wa kujiunga na chama cha upinzani (most likely CHADEMA). Lakini akifanya hivyo kuna kila dalili akakisumbua sana CCM kule Monduli kama ilivyo kwa Slaa hivi sasa. Je CHADEMA wako tayari kumpokea? Watawaeleza nini wananchi?

Ni jambo la kusubiri na kuona!
 
As I noted in one of my posts,one of EL's chronic problems is putting emotions infront of common sense.Huyu jamaa kwa "kuwaka" hajambo.Ni kama anam-underestaimate kila mtu.Pengine ni jeuri ya fedha,pengine ni obsession yake na kumrithi JK.

Only way to control this unguided missile ni kwa JK kuweka urafiki (kama bado upo) kando,na kumvaa mshkaji wake kwamba spidi yake ya 240 kwenye wrong lane itapelekea ajali.Nadhani kuna kila dalili ya EL kuja na "mtandao mpya" utakaojumuisha RA,Karamagi na mafisadi wengine.

JK,you have been warned!
 
Lowassa, ninaamini ni kama enzi zile Kitine, bado haelewi vizuri bongo na siasa zake, lakini very soon ataelewa manaa na Salmin naye wakati fulani alidhani ana nguvu sana na anaweza kujipa term ya tatu, mpaka siku moja alipoitwa cc na kuambiwa ajitoe na ujinga,

Lowassa, ameharibu jina lake kwa kujiuzulu kutokana na ripoti mbaya dhidi yake, kama kweli angekuwa na akili kubwa ya siasa, basi angeizuia ripoti mapema kwa ku-negotiate surrender hata kabla kamati ya Mwakyembe, haijaundwa au hata ilipoundwa angetumia nafasi yake kisiasa na kiserikali, kumuomba muungwana amuondoe kistaarabu mapema kabla ya kufikia mwisho wa ripoti, ripoti isingekuwa na nguvu sana as long as Lowassa, angekuwa ametoka mapema, huenda hata isingepelekwa bungeni, kwa sababu marafiki zake wangeweza ku-negotiate isitolewe kabisa since alishajiuzulu au kutolewa na rais mapema, lakini kusubiri mpaka mwisho halafu ndio aanze kampeni za kujisafisha anapoteza hela zake bure masikini ya Mungu, na wabongo they are very good at playing na watu wenye hela za mchezo kama huyu, huku wakijua kuwa wanachomfanyia ni impossible,

Hawezi kurudi tena kwenye power haitakuja kutokea, hata akiingia upinzani hakuna wa kumfuata huko kati ya mawaziri walioko kwenye power sasa, kosa lingine kubwa sana alilolifanya ni kukosa umakamu wa ccm, maana angekuwa nao, sasa hivi asingekuwa na tatizo la kurudi kwenye power ccm, ukweli ni kwamba he is done maana kina Pinda watampa vipi hiyo nafasi? cc haingii tena sasa unakuwaje powerful bongo kama huingii cc? Six naye sasa nasikia anataka urais pia, na mkuu pale nje naye nasikia yumo njiani, wenziwe wote bado wako kwenye power, yeye tu ndiye yuko nje halafu wampe nafasi ya kurudi?

Mimi ningemshauri,apumzike kwanza ili siasa zimfuate na sio yeye kuzifukuzia kiasi hiki, mbona kina Diallo wametulia kimyaaa!
 
Lowassa anaelekea kwenye kapu la historia. Sidhani kama anao ujasiri wa kujiunga na chama cha upinzani (most likely CHADEMA). Lakini akifanya hivyo kuna kila dalili akakisumbua sana CCM kule Monduli kama ilivyo kwa Slaa hivi sasa. Je CHADEMA wako tayari kumpokea? Watawaeleza nini wananchi?
Ni jambo la kusubiri na kuona!

Duh! yaani imefikia Chadema kuwa mfano bora wa kula matapishi?...Hiyo siku Lowassa atakapo ingia/jiunga na Chadema ndio siku Chadema watakuwa kama chama cha Mrema baada ya mwaka 1995!....
 
As I noted in one of my posts,one of EL's chronic problems is putting emotions infront of common sense.Huyu jamaa kwa "kuwaka" hajambo.Ni kama anam-underestaimate kila mtu.Pengine ni jeuri ya fedha,pengine ni obsession yake na kumrithi JK.

Only way to control this unguided missile ni kwa JK kuweka urafiki (kama bado upo) kando,na kumvaa mshkaji wake kwamba spidi yake ya 240 kwenye wrong lane itapelekea ajali.Nadhani kuna kila dalili ya EL kuja na "mtandao mpya" utakaojumuisha RA,Karamagi na mafisadi wengine.

JK,you have been warned!

This seem to be exactly na ninachoona!!

EL kukaa kimya ni miujiza...na obsession ya madaraka? haitamuacha bila kuwa na Kundilake..lets wait and see na hii itakuwa encouraged na kilema chake kushindwa ku_control emotions.. Hisia zikiwaka zinamfikirisha mtu kutenda mambo ambayo basicaly ni kumpotosha hata kama haoni hivyo kwa wakati ule.
 
Lowassa anaelekea kwenye kapu la historia. Sidhani kama anao ujasiri wa kujiunga na chama cha upinzani (most likely CHADEMA). Lakini akifanya hivyo kuna kila dalili akakisumbua sana CCM kule Monduli kama ilivyo kwa Slaa hivi sasa. Je CHADEMA wako tayari kumpokea? Watawaeleza nini wananchi?

Ni jambo la kusubiri na kuona!

Chadema, kwa maoni yangu haistahili kabisa kumchukua Lowassa. Wamchukue kwa lipi hasa atakaloweza kuwasaidia Chadema? Makombo ya CCM yakubaliwe na Chadema?, NO WAY! watakuwa wamefanya kosa kubwa sana. Anaweza akaacha historia nzuri kama atakuwa mkweli na kusema ufisadi wote anaoufahamu kuhusu kashfa mbali mbali za ndani ya serikali
 
seems he's not a smart politician na hizi stunts anazofanya sasa za kujisafisha/propaganda kwenye TV,Magazeti na kupokelewa na wapambe 10,000or whatever number it is will come back to haunt him na history will not look kindly on this.
 
hata mtu awe kilaza wa aina gani, hujifunza kutokana na makosa yake yaliyopita.....sitegemei kama Lowassa atakuwa mjinga kiasi cha kwamba kuweka emotions mbele kiasi cha kuwa asijue anafanya nini.
safari hii Kikwete ana kazi kubwa zaidi ya walivyokuwa na Marais wengine waliowatimua kina Jumbe na Hamadi.

kwanza kuna urafiki baina yao, na pia Lowassa ameshajifunza historia.

sitegemei kama Lowassa atampa Kikwete njia rahisi ya Kumfukuza chama.....lakini na tukae tusubiri
 
Jinsi EL alivyopoteza nafasi yake hadi akaaunguka Dodoma nitawasimulia siku nyingi. Alichezewa mchezo ambao siku moja utaandikwa kwenye vitabu vya rekodi! Na hicho ndicho kilichomfanya achanganyikiwe.
 
Jinsi EL alivyopoteza nafasi yake hadi akaaunguka Dodoma nitawasimulia siku nyingi. Alichezewa mchezo ambao siku moja utaandikwa kwenye vitabu vya rekodi! Na hicho ndicho kilichomfanya achanganyikiwe.

Jazba aliyokuwa nayo siku analitangazia Bunge kwamba ameamua kuachia ngazi ni uthibitisho tosha kabisa kwamba alikuwa amechananyikiwa na hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali kuachia ngazi huku akiwa bado anatamani kuendelea kuwa PM. Siku ya kufa nyani miti yote hupakwa utelezi!
 
Jinsi EL alivyopoteza nafasi yake hadi akaaunguka Dodoma nitawasimulia siku nyingine. Alichezewa mchezo ambao siku moja utaandikwa kwenye vitabu vya rekodi! Na hicho ndicho kilichomfanya achanganyikiwe.

MKJJ
Tupo kwenye vigoda na popcorn zetu tukisubiria fully story kuanguka kwa Lowassa...inasemekana yeye mwenyewe hakutegemea kabisa, naona anajipanga upya...ingawa upinzani uliopo mbele anaweza potea kabisa asahaulike kwenye historia...
 
Jinsi EL alivyopoteza nafasi yake hadi akaaunguka Dodoma nitawasimulia siku nyingi. Alichezewa mchezo ambao siku moja utaandikwa kwenye vitabu vya rekodi! Na hicho ndicho kilichomfanya achanganyikiwe.

...kuna kilichomwangusha kweli zaidi ya ufisadi wake?
 
sitegemei kama Lowassa atampa Kikwete njia rahisi ya Kumfukuza chama .....lakini na tukae tusubiri

Mbona tayari ameishampa hiyo opportunity na siyo swala la JK peke yake bali ni swala la CC nzima.

Kosa la EL ni kuendelea kubwabwaja badala ya kukaa kimya huku akiangalia afanye nini ili kuweza ku-bounce back.

Wapambe wake kama akina Ole Naiko wanazidi kuongeza mafuta kwenye moto unaowaka tayari. Hakuna mtu asiyejua uhusiano wa EL na Naiko. Kitendo cha Naiko kuleta swala la ukabila kwenye Richmond ni kosa kubwa sana na asubir hukumu yake kutoka serikalini ama Bungeni.

Mpaka hapo tayari JK na CC wana kila sababu ya kumshughulikia kama watataka kufanya hivyo kutokana na series ya mambo jinsi yanavyokwenda. EL kama angekuwa smart angekaa kimya kabisa na wala asionyeshe jazba. The way anavyozidi kujitetea ndivyo anavyozidi kujiongezea maadui na kuonyesha udhaifu wake ama kiburi chake kwa serikali na CCM.
 
Masaa machache kabla ya ripoti kugawiwa kwa wabunge.. Lowassa alikuwa na uhakika kuwa angeweza kupangua. Usiku ule walipopewa ripoti in advance yeye na Kiongozi wa Upinzani.. ndio ulikuwa usiku wa balaa!! kisirisiri yeye na mkewe wakawa wanajiuliza "tutarudi na roho zetu?".

Na siku iliyofuata wakati ripoti inasomwa na Dr. Mwakyembe Lowassa alimuona Dr. Mwakyembe kama vile ni "Malaika wa Shetani" na ndipo wabunge wa CCM walipocharuka na kuanza kumkomelea Lowassa utadhani wamepewa amri ya "kamlete akibisha mlipue".

Lowassa na timu yake wakajikuta wamepewa kazi, kazi ambayo hata "Kuli" asingeiweza. Ndipo ile asubuhi yake yeye na mkewe wakajikuta wameshikilia "roho mkononi". Alikuwa amekasirika, na alikuwa hana njia yoyote isipokuwa kujiuzulu Uwaziri Mkuu.

Hakuondoka hivi hivi bali alidai kilichofanyika ni "Njama" tena njama kama ile iliyosimuliwa kwenye "maajabu ya mlima Kolelo".Ilikuwa ni njama ambayo kutisha kwake kulikuwa kama hadithi za "Mizimu ya Watu wa Kale". Ni Njama hii iliyomuudhi Lowassa na kuamua kuanza kuandaa "Kikosi cha Kisasi".

Ni Kikosi hicho ambacho leo hii kimeanza mapambano kwa kuapa "Liwalo na Liwe".
 
Jinsi EL alivyopoteza nafasi yake hadi akaaunguka Dodoma nitawasimulia siku nyingi. Alichezewa mchezo ambao siku moja utaandikwa kwenye vitabu vya rekodi! Na hicho ndicho kilichomfanya achanganyikiwe.

i hope tunapoamka kesho utakuwa umeshaweka hii issue at least kwa abstract level.

ngoja nikusaidie kuanza kidogo:::::


uchaguzi ccm nov 2007:::: chairman jk aleta sheria mpya kuwa prime minister anaingia cc moja kwa moja. why ///////

nov 2007 speaker sitta anapewa mwongozo weka kamati ya kuchunguza richmond na waweke hawa. why nov 2007 on this issue which was hot since 2006////////

nov 2007 epa issue ni kubwa sana na mweka hazina wa ccm anatolewa.

sasa nakupa ile heart of the city yenyewe ambayo imecheza chess yote, but lazima niweke riddle lindi/rukwa/tabora na mtoto wa mjini braza.

goodnight.
 
Huyu jamaa amechanganyikiwa alijua atakaa madarakani milele as a result imemtokea puani.
Namshauri awe mpole tuu ndio maisha ayo
 
Mzee MKJJ nimekunukuu
"Lowassa na timu yake wakajikuta wamepewa kazi, kazi ambayo hata "Kuli" asingeiweza. Ndipo ile asubuhi yake yeye na mkewe wakajikuta wameshikilia "roho mkononi". Alikuwa amekasirika, na alikuwa hana njia yoyote isipokuwa kujiuzulu Uwaziri Mkuu."

Hivi EL alijiamini kwamba kashfa ya Richmond haita mgusa? kwanini alijiamini hivyo? anasema Mhe. Spika alimdokeza na kumtaka aandae ushahidi utakao mwezesha kujitoa ktk kashfa hiyo. Kwakuwa hakuwa na ushahidi akaamua kuwa 'mbogo' na kudai kudhalilishwa sana na kuutaka uwaziri Mkuu wake.

what i see, EL is not strategic leader but only a strategic thief.
 
Nurujamii anakosea kulinganisha sababu zilizomfanya Slaa kuhamia CHADEMA na ambazo zinaweza kumfanya Lowasa kwenda huko baadaye kama ataamua. Hawa ni watu wawili tofauti kabisa ambao huwezi kuwalinganisha. Wakati Slaa alikimbia ufisadi, huyu mwingine ufisadi wake ndio utakuwa unamtoa.
 
seems he's not a smart politician na hizi stunts anazofanya sasa za kujisafisha/propaganda kwenye TV,Magazeti na kupokelewa na wapambe 10,000or whatever number it is will come back to haunt him na history will not look kindly on this.

Nyingine hii hapa katoa ktk harakati za kujisafisha; Lakini bado hasafishiki na mkutno mkuu utamuumbua.
Yetu macho na masikio.


Lowassa aonya kuna ‘kidudumtu’ CCM
na deodatus balile, monduli

WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, amekitahadharisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa ndani yake na serikalini kuna wafitini wanaotaka kupotosha ajenda ya maendeleo kwa kupiga kelele za ufisadi.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika eneo la Mto wa Mbu jimboni Monduli, Lowassa alisema CCM ina watu ndani yake ambao hawakitakii mema chama hicho. “Naomba nieleweke katika hili. Sisemi tusipambane na ufisadi, tusishughulikie wanaoiba mali ya umma… tupambane nao, ila wapo wenzetu ndani ya chama na serikali watakaojaribu kututoa kwenye hoja yetu.

“Tusimamie Ilani ya uchaguzi kwa mshikamano. Tukiyumba katika hili na tusipofanya hivyo, mwaka 2010 tutakuwa na maswali mengi sana na wapinzani wetu tutawapa fursa,” alisema.

Alisema wakati wa kampeni mwaka 2005, chama kiliwaahidi watu maisha bora na kuonya kuwa ahadi hiyo isipotekelezwa, hatari kubwa inakinyemelea chama; “Tuwajue wasiotutakia mema mapema tusikitengenezee chama bomu mbele ya safari,” alisema Lowassa.

Lowassa aliyepokewa na waendesha baiskeli eneo la Kigongoni, lililopo wastani wa kilomita tatu kutoka Mto wa Mbu, alihutubia wakazi wa eneo hilo na kupewa magunia mawili ya mchele, ndizi na mkanda wenye sime.

Aliwambia wananchi hao kuwa yeye bado ana nguvu zake, akili na uwezo, na akafafanua kilichotokea kuhusiana na kashfa ya Richmond hadi kujiuzulu katika alichoeleza kuwa ni uwajibikaji wa pamoja.

Baadhi ya wananchi waliozungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema ufafanuzi alioutoa Lowassa ni kiashirio na maelezo tosha kuwa hakushiriki katika kashfa hiyo.

Mwananchi aliyejitambulisha kama Peter Longidai, alisema: “Juzi aliwataja kina (Dk. Ibrahim) Msabaha, (Johnson) Mwanyika na (Grey) Mgonja. Si na wao wanayo midomo? Kama alihusika si waseme? Yeye kasema wao wanajua kila kitu, mbona wako kimya sasa? Ukweli unazidi kufahamika,” alisema.


Source: Magazeti ya rafiki yake (Mtanzania)
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom