Uchaguzi 2020 Kamati Kuu ya ACT-Wazalendo inafanya kikao leo 02 Agosti 2020

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
605
1,536
IMG-20200802-WA0011.jpg


Kamati Kuu ya ACT Wazalendo inafanya kikao leo 02 Agosti 2020. Kikao hichi ni maandalizi ya Mkutano Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 05 Agosti 2020.

Kikao kinafanyika Lamada Hoteli jijini Dar-es-salaam.

Pamoja na mambo mengine. Kamati Kuu leo inategemea kupendekeza majina ya wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar na kupitisha Rasimu za Ilani ya Uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ya Uchaguzi wa Zanzibar.

IMG-20200802-WA0014.jpg


Katibu Mkuu wa Chama, Ndugu Ado Shaibu, akitafakari jambo na baadhi ya wajumbe kabla ya kuanza kikao.


IMG-20200802-WA0004.jpg


Naibu Katibu wa Idara ya Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma ndugu, Janeth Rithe akizungumza na waandishi wa habari mapema leo kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya chama.

IMG-20200802-WA0021.jpg
IMG-20200802-WA0008.jpg
IMG-20200802-WA0006.jpg
IMG-20200802-WA0009.jpg

Taswira mbalimbali za wajumbe wa Kamati Kuu wakijadiliana kabla ya kuanza Kikao chao.

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
 
Sasa Kamati Kuu Chama inapitia Rasimu ya Ilani ya Uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
IMG-20200802-WA0031.jpg
IMG-20200802-WA0033.jpg
IMG-20200802-WA0032.jpg
 
Leo Mwenyekiti wa Chama Taifa, Ndugu Maalim @SeifSharifHamad anaongoza Kikao cha Kamati Kuu ya chama chetu cha @ACTwazalendo

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
IMG-20200802-WA0045.jpg
 
Katibu Mkuu wa Chama na Katibu Mkuu wa kikao cha Kamati Kuu, Ndugu Ado Shaibu akiwa tayari kuongoza Kikao cha Kamati Kuu.

#KaziNaBata #TheFutureIsPurple
IMG-20200802-WA0065.jpg
IMG-20200802-WA0069.jpg
 
Ina maana membe amekosa 7bl za kuinunua CHADEMA apewe nafasi ya kugombea urais? Au atoe 1bl ampe lissu ili akagombee na Membe nafasi ya makamu wa rais.
 
Sasa Kamati Kuu Chama inapitia Rasimu ya Ilani ya Uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

#KaziNaBata #TheFutureIsPurpleView attachment 1524839View attachment 1524841View attachment 1524842
Membe hataleta faida yoyote kubwa kwa upinzani katika uchaguzi huu. Hana mvuto, na ukweli mvuto wake umeporomoka sana ikilinganishwa na alipokuwa akishiriki katika kinyang'anyiro cha kutafuta kupitishwa na CCM kuwa mgombea urais 2015.

Kitu pekee ambacho Membe anaweza kusaidia upinzani, na hasa ACT Wazalendo ni kuchangia kupata mbunge mmoja au wawili kule kusini. Vinginevyo, kama Membe atagombea urais kura zake chache atakazopata atasaidia kidogo kupunguza kura za CCM kwa kuwa zaidi atapigiwa kura na wanaCCM wasiofurahishwa na mwenendo wa uongozi wa chama hicho.

Wapinzani wengi, ambao wamechoshwa kabisa na mfumo wa utawala huu watampigia kura mtu wanayeamini ni mpinzani kweli kweli. Membe amekuja upinzani wakati mbaya ambao wapinzani hawana imani kabisa na watu wanaotoka CCM. Kilichofanywa na Lowasa na Sumaye hakiwezi kuwaondoka kwa urahisi hata kama ACT-Wazalendo watakesha wakiimba mapambio. Najua ACT-Wazalendo wanamng'ang'ania Membe ili pamoja na kuwasaidia kupata wabunge awasaidie pia kufuta image ya Uislamu ndani ya chama hicho, lakini Membe mwenyewe ni bahati mbaya ukristo wake ni wa jina zaidi!

ACT-Wazalendo wasitumie nguvu kubwa kushawishi Membe kuwa mgombea urais wa kuwakilisha upinzani kwa kuwa hili haliwezekani kupata kibali kwa wapiga kura wenyewe kwanza hata kabla ya Chadema. Wakilazimisha watazidi kupunguza imani yao kwa wapiga kura ambao wanakitilia mashaka pia chama hicho kuwa ni pandikizi la TISS. Zaidi ile Pr au communication strategy yao iwe kuji-brand kujiondoa katika kutizamwa zaidi katika maeneo haya mawili-la udini na kutumika na TISS. Hili litahitaji sasa wenye akili nyingi kwenye media strategy. Kuna media ambazo hazijatumika kabisa lakini ni fursa kubwa ya kujiondoa katika image hiyo.
 
Ina maana membe amekosa 7bl za kuinunua CHADEMA apewe nafasi ya kugombea urais? Au atoe 1bl ampe lissu ili akagombee na Membe nafasi ya makamu wa rais.
Mijitu kama hii sijui kwanini inakuwa kwenye majukwaa kama hili!
 
ACT Wazalendo ndio chama pekee cha upinzani kinachoweza kumtoa CCM madarakani, hakina kashfa wala jambo lolote la kujisafisha, CHADEMA wana mambo mengi sana ya kujisafisha katika uchaguzi oktoba.
 
ACT Wazalendo ndio chama pekee cha upinzani kinachoweza kumtoa CCM madarakani, hakina kashfa wala jambo lolote la kujisafisha, CHADEMA wana mambo mengi sana ya kujisafisha katika uchaguzi oktoba.
Hebu taja moja tu ambalo Chadema watapaswa kujisafisha nalo!
 
Hebu taja moja tu ambalo Chadema watapaswa kujisafisha nalo!
Ishue ya kumchukua lowassa na kumpa kijiti cha kugombea, ishue za wabunge/madiwani walionunuliwa na CCM kutoka Chadema wanazovujisha (Hii haina madhara sana kwasasa, kwasababu wengi wao wamepigwa chini kwenye kura za maoni - wanawaza kurudi kuomba msamaha). Ishue za ubaguzi ndani ya chama kwenye uchaguzi wa viongozi wa chama.
 
Ishue ya kumchukua lowassa na kumpa kijiti cha kugombea, ishue za wabunge/madiwani walionunuliwa na CCM kutoka Chadema wanazovujisha (Hii haina madhara sana kwasasa, kwasababu wengi wao wamepigwa chini kwenye kura za maoni - wanawaza kurudi kuomba msamaha). Ishue za ubaguzi ndani ya chama kwenye uchaguzi wa viongozi wa chama.
Duh! kuna kashfa gani hapo sasa?
 
Membe hataleta faida yoyote kubwa kwa upinzani katika uchaguzi huu. Hana mvuto, na ukweli mvuto wake umeporomoka sana ikilinganishwa na alipokuwa akishiriki katika kinyang'anyiro cha kutafuta kupitishwa na CCM kuwa mgombea urais 2015.

Kitu pekee ambacho Membe anaweza kusaidia upinzani, na hasa ACT Wazalendo ni kuchangia kupata mbunge mmoja au wawili kule kusini. Vinginevyo, kama Membe atagombea urais kura zake chache atakazopata atasaidia kidogo kupunguza kura za CCM kwa kuwa zaidi atapigiwa kura na wanaCCM wasiofurahishwa na mwenendo wa uongozi wa chama hicho.

Wapinzani wengi, ambao wamechoshwa kabisa na mfumo wa utawala huu watampigia kura mtu wanayeamini ni mpinzani kweli kweli. Membe amekuja upinzani wakati mbaya ambao wapinzani hawana imani kabisa na watu wanaotoka CCM. Kilichofanywa na Lowasa na Sumaye hakiwezi kuwaondoka kwa urahisi hata kama ACT-Wazalendo watakesha wakiimba mapambio. Najua ACT-Wazalendo wanamng'ang'ania Membe ili pamoja na kuwasaidia kupata wabunge awasaidie pia kufuta image ya Uislamu ndani ya chama hicho, lakini Membe mwenyewe ni bahati mbaya ukristo wake ni wa jina zaidi!

ACT-Wazalendo wasitumie nguvu kubwa kushawishi Membe kuwa mgombea urais wa kuwakilisha upinzani kwa kuwa hili haliwezekani kupata kibali kwa wapiga kura wenyewe kwanza hata kabla ya Chadema. Wakilazimisha watazidi kupunguza imani yao kwa wapiga kura ambao wanakitilia mashaka pia chama hicho kuwa ni pandikizi la TISS. Zaidi ile Pr au communication strategy yao iwe kuji-brand kujiondoa katika kutizamwa zaidi katika maeneo haya mawili-la udini na kutumika na TISS. Hili litahitaji sasa wenye akili nyingi kwenye media strategy. Kuna media ambazo hazijatumika kabisa lakini ni fursa kubwa ya kujiondoa katika image hiyo.
Acha zako 2020 sisi upinzani 2020 tunaenda na Mbobezi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom