Kamati Kuu CHADEMA yawavua Uanachama Madiwani 5 walioingia muafaka Arusha

Mungi

JF Gold Member
Sep 23, 2010
16,975
9,566
Mkutano wa cc ya CHADEMA ndio umeisha muda huu, wamewafukuza kwenye chama madiwani watano waliokaidi agizo la chama.

Na kadi wamenyang'anywa

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA).TAARIFA KUHUSU MAAMUZI YA KAMATI KUU YA CHADEMA YALIYOFIKIWA KATIKA MKUTANO WA DHARURA ULIOFANYIKA SIKU YA JUMAMOSI/JUMAPILI TAREHE 06-07 AGOSTI 2011 KATIKA HOTELI YA IMAGI MJINI DODOMA.
Kamati Kuu ya CHADEMA ilikutana katika Mkutano wa Dharura uliofanyika siku ya Jumamosi na Jumapili tarehe 06 Agosti 2011 katika Hoteli ya Imagi Mjini Dodoma. Pamoja na mambo mengine Ilifikia maamuzi yafuatayo :

1.
Kamati Kuu ilipokea taarifa ya utekelezaji wa maagizo iliyoyatoa katika Mkutano wake wa tarehe 17 Julai 2011 iliyowataka madiwani wa CHADEMA Arusha kujiuzulu nafasi walizozipata pamoja na kuomba radhi kwa makosa waliyoyafanya kutokana na mwafaka uliofikiwa baina yao na madiwani wenzao wa TLP na CCM kwa kuwa chama hakikuridhia wala kuutambua mwafaka huo.


2.
Kamati Kuu imezingatia kuwa, kati ya madiwani 10 waliopewa maelekezo na Kamati Kuu, madiwani watano (5) ndio wametekeleza maelekezo kikamilifu wakati madiwani wengine watano (5) wamekataa kuyatekeleza maelekezo hayo.

3. Baada ya kutafakari kwa kina taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya Kamati Kuu, na kuwapa nafasi ya kujieleza mbele ya Kamati Kuu Madiwani ambao walikuwa hawajatekeleza maelekezo,Kamati Kuu imezingatia kuwa madiwani wamekataa kutekeleza maagizo ya Kamati Kuu.

Aidha, Kamati Kuu imezingatia kuwa kitendo cha madiwani kukataa kutekeleza maagizo halali ya Kamati Kuu ni utovu mkubwa wa nidhamu na ni kuvunja maadili na kanuni za chama, na kinaenda kinyume na msingi mama wa CHADEMA wa uwajibikaji.

Hivyo basi, kwa kutumia mamlaka ya Kikatiba Kamati Kuu imewafukuza uanachama madiwani watano wafuatao kwa kosa la kukataa kutekeleza maagizo ya Kamati Kuu:


i)
Ndugu Estomih Mallah


ii)
Ndugu John Bayo


iii)
Ndugu Charles Mpanda

iv) Ndugu Rehema Mohamed

v)
Ndugu Reuben Ngowi
Watajwa hapo juu wamejulishwa maamuzi ya Kamati Kuu ndani ya Mkutano tarehe 07 Agosti 2011 saa 7:57 usiku, Aidha, kila mmoja wao atakabidhiwa barua yenye kueleza maamuzi ya Kamati Kuu.

4. Aidha, Kamati Kuu imepokea taarifa ya mazungumzo baina ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe Freeman Mbowe, na Waziri Mkuu, Mhe Mizengo Pinda, juu ya nia na azima ya kumaliza tatizo la mgogoro wa umeya Arusha, waliyoyafanya asubuhi ya siku ya Jumamosi, Tarehe 06 Agosti 2011 nyumbani kwa Waziri Mkuu Mjini Dodoma.

Kamati imezingatia kuwa:

a. Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa na Waziri Mkuu wamekubaliana kuunda Kamati ya Kitaifa ya kushughulikia mgogoro wa umeya wa Arusha itakayojumuisha wajumbe kutoka sehemu mbili zinazohusika katika mgogoro huu ambazo ni CCM na CHADEMA

b.
Kamati ya Kitaifa ya Maridhiano itaundwa haraka iwezekanavyo, na kwa vyovyote mgogoro wa u meya Manispa ya Arusha ulikubalika uishe ndani ya mwezi mmoja tangu tarehe ya mazungumzo ya Mwenyekiti wa Taifa na Waziri Mkuu


c.
Uenyekiti wa Kamati ya Kitaifa utakuwa chini ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Ndugu John Tendwa, na kwamba Msajili wa Vyama vya Siasa ataratibu uundwaji wa Kamati hiyo ya Kitaifa.


5.
Kamati Kuu imetambua juhudi za Waheshimiwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe Freeman Mbowe, kwa hatua yao chanya ya kumaliza mgogoro wa Arusha.


6.
Pamoja na hatua njema kuelekea kumaliza mgogoro wa umeya Arusha, Kamati Kuu ya CHADEMA itaendelea kusitisha kumtambua rasmi Meya wa Arusha hadi pale mazungumzo yaliyoanishwa hapo juu yatakapokamilika na mwafaka bayana kupatikana.
Imetolewa na:
……………….
Mhe. Freeman Aikaeli Mbowe (Mb)
MWENYEKITI WA TAIFA
 
kamati kuu ya chadema imechukua maamzi mazito ya kuwafukuza madiwani watano kati ya sita baada ya mmoja kutokufika mbele ya kamati hiyo kama alivyotakiwa, ambae hajakwambwa la balaa hilo ni Crispian.. nawasilisha
 
Kamati kuu ya chadema imewafukuza madiwani sita waliokaidi agizo la chama kutokana na kuingia muafaka feki wa kumtambua meya wa kichina.
 
Kamati kuu Chadema leo tarehe 7/8/2011 majira ya saa saba usiku imefikia maamuzi magumu baada ya kuwafuta uanachama madiwani wasaliti watano ambao ni kama ifuatvyo , John Bayo kata ya Elirai , Estomih Malah ( Kimandolu ) , Charles Mpanda (Kaloleni) na Rehema Mohamed wa viti maalumu. Hawa ni wale baadhi ya madiwani walioingia kihuni bila kufuata utaratibu wa Chama .

Kutokana na uamuzi huu Tume ya Uchaguzi italazimika kupanga tarehe ya uchaguzi mdogo.
 
Kamati kuu Chadema leo tarehe 7/8/2011 majira ya saa saba usiku imefikia maamuzi magumu baada ya kuwafuta uanachama madiwani wasaliti watano ambao ni kama ifuatvyo , John Bayo kata ya Elirai , Estomih Malah ( Kimandolu ) , Charles Mpanda (Kaloleni) na Rehema Mohamed wa viti maalumu. Hawa ni wale baadhi ya madiwani walioingia kihuni bila kufuata utaratibu wa Chama .

Kutokana na uamuzi huu Tume ya Uchaguzi italazimika kupanga tarehe ya uchaguzi mdogo.

Safi sana CHADEMA safisha uchafu wote, hao madiwani hawana nidhamu kabisa. Potelea mbali bora JESHI DOGO LENYE NIDHAMU KULIKO JESHI KUBWA LISILO NA NIDHAMU.... Mapambano bado yanaendelea.
 
Ni uamuzi wenye busara. Chadema kamwe isisite kuchukua maamuzi magumu pale inapobidi kusafisha uchafu
 
hii inaonyesha ndani ya chadema kuna watu wenye uroho wa pesa na hawana uchungu na nchi hii..,hivyo hata kama chadema itapewa nchi 2015 yatazuka yaleyale tu ya kashfa nyingi..,
 
hii inaonyesha ndani ya chadema kuna watu wenye uroho wa pesa na hawana uchungu na nchi hii..,hivyo hata kama chadema itapewa nchi 2015 yatazuka yaleyale tu ya kashfa nyingi..,

Kool-aid will work better for you!!!!!!!
 
hii inaonyesha ndani ya chadema kuna watu wenye uroho wa pesa na hawana uchungu na nchi hii..,hivyo hata kama chadema itapewa nchi 2015 yatazuka yaleyale tu ya kashfa nyingi..,

Ndio maana wewe ni mtoto wa mama hujui mambo. Subiri. Halafu angalia bado unanuka uvumba. Subiri subiri uwe walau menber ndio uanze kutoa hoja za namna hii.
 
Back
Top Bottom