Kamati kuu CHADEMA yatoa karipio kali kwa viongozi wake waliomsema Lowassa hadharani

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,445
7,810
Baadhi ya wajumbe walimtaka Lowassa aombe radhi hadharani kutokana na tukio hilo(Kwenda Ikulu) lakini busara ilitumika kwa kutaka jambo hilo liishe kwa Lowassa kutoa taarifa hadharani.

Raia Mwema liliambiwa pia kwamba wajumbe wa kikao hicho walielezwa kuwa Lowassa kwa sasa amekumbwa na changamoto kadhaa katika maisha yake binafsi na si busara kumuongezea mambo mengine mazito.

Miongoni mwa changamoto za Lowassa ambazo zimetajwa kwenye kikao cha kamati kuu ni pamoja na suala la familia yake(Mtoto wake kuhamishwa benki kuu na mkwewe kuwa mahabusu).

"Kamati kuu imemkubalia Lowassa abaki ndani ya chama hicho kutokana na kwamba kama ni changamoto hata mwenyekiti wetu pia amekumbana nazo na bado anakabiliana nazo.

Lakini pia chama kimeonya wale wote waliotoa matamko baada ya uamuzi ule wa Lowassa". Alisema ofisa mmoja wa CHADEMA kwa sharti la kutotajwa jina.

Mbali na makubaliano hayo, kamati kuu pia ilitoa karipio kwa viongozi wake ambao walionekana kumsema Lowassa hadharani mara baada ya kutokea kwa tukio hilo na kuwakumbusha kuwa chama kina wasemaji wake rasmi ambao ni mwenyekiti, katibu mkuu na msemaji wa chama(Makao Makuu).

Mara baada ya taarifa za mkutano huo wa Lowassa na DK. Magufuli kuwekwa hadharani, baadhi ya vigogo wa chama hicho walitumia mitandao ya kijamii kumshutumu mbunge huyo wa zamani wa Monduli.
 
ametolea ufafanuzi wapi au na wewe umesoma udaku wa mitandaoni kwamba kamati kuu imemuhoji wakati siku hiyo walikuwa moro kwenye mazishi na kutangaza kuhailisha kikao chao.
huelewi na wewe mkuu nimekwambia ya kwamba yeye mwenyewe ndie alieandika kwenye twitter yake.
 
Mimi ni CHADEMA pure ila viongozi walikosea sana kuanza kutofautiana kwenye public.... Ilibidi wayamalize kisiri siri bila sisi kuona kabisa kuwa hawana mawasiliano.... Yaani lowassa alichokiongea bado hawajakijua wanaanza kumkosoa hadharani ilibidi wawe watulivu wakutane wayamalize watoke na kauli moja

Pamoja na madhaifu lukuki ya CCM ila kwenye hili huwa wanajitahidi sana kumaliza matatizo yao kwa usiri na busara nyingi bila madhara kuonekana nje kwa wananchama wa kawaida

Kwa hili uongozi wa CHADEMA mlikosea kuwepo na mawasiliano kabla hamjatoa matamko
 
Baadhi ya wajumbe walimtaka Lowassa aombe radhi hadharani kutokana na tukio hilo(Kwenda Ikulu) lakini busara ilitumika kwa kutaka jambo hilo liishe kwa Lowassa kutoa taarifa hadharani.

Raia Mwema liliambiwa pia kwamba wajumbe wa kikao hicho walielezwa kuwa Lowassa kwa sasa amekumbwa na changamoto kadhaa katika maisha yake binafsi na si busara kumuongezea mambo mengine mazito.

Miongoni mwa changamoto za Lowassa ambazo zimetajwa kwenye kikao cha kamati kuu ni pamoja na suala la familia yako(Mtoto wake kuhamishwa benki kuu na mkwewe kuwa mahabusu).

"Kamati kuu imemkubalia Lowassa abaki ndani ya chama hicho kutokana na kwamba kama ni changamoto hata mwenyekiti wetu pia amekumbana nazo na bado anakabiliana nazo.

Lakini pia chama kimeonya wale wote waliotoa matamko baada ya uamuzi ule wa Lowassa". Alisema ofisa mmoja wa CHADEMA kwa sharti la kutotajwa jina.

Mbali na makubaliano hayo, kamati kuu pia ilitoa karipio kwa viongozi wake ambao walionekana kumsema Lowassa hadharani mara baada ya kutokea kwa tukio hilo na kuwakumbusha kuwa chama kina wasemaji wake rasmi ambao ni mwenyekiti, katibu mkuu na msemaji wa chama(Makao Makuu).

Mara baada ya taarifa za mkutano huo wa Lowassa na DK. Magufuli kuwekwa hadharani, baadhi ya vigogo wa chama hicho walitumia mitandao ya kijamii kumshutumu mbunge huyo wa zamani wa Monduli.
Ni jeuri na dharau kubwa sana kumsema mwenye mali hadharani
 
Back
Top Bottom