Naomba kuuliza. Ninavyojua , kamati kuu inatoa mapendekezo na siyo maamuzi. NEC ndiyo inaamua nani apewe hiyo nafasi baada ya kupitia mapendekezo ya kamati kuu na hivyo hivyo kamati kuu ina toa mapendekezo baada ya kupitia maoni na mapendekezo ya kamati ya maadili, kamati za siasa za mkoa na wilaya.