Kamati hii ya Uteuzi inaweza kweli kutupatia Tume Huru ya Uchaguzi?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,986
144,313
Leo hii nimeamua kupitia baadhi ya Ibara za katiba Inayopendekezwa na mojawapo ni Ibara ya 218(1) inayohusu Kamati ya Uteuzi ambayo itakuwa na wajibu wa kupokea na kuchambua maombi ya watu wanaomba kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

Kamati hii ya uteuzi,kwa mujibu wa Katiba Inayopendekezwa,itakuwa na wajibu ya kuteua Mwenyekit wa Tume Huru ya Uchaguzi,Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wengine saba wa Tume hii ya uchaguzi.

Wafuatao ndio watu watakuwa wajumbe wa Kamati hiyo ya uteuzi
na ambao ndio watachambua maombi ya watu wanaotaka kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi na kisha kuwasilisha majina ya wajumbe watakaochaguliwa kwa Raisi kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.

1.Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ndie atakuwa mwenyekiti wa kamati ya uteuzi

2 Jaji Mkuu wa Zanzibar ambae atakuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi.

3.Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano

4.Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi

5.Jaji Kiongozi

6.Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Na pia kutakuwa na katibu wa kamati hii ya uteuzi ambae atakuwa ni Mkurugenzi wa Tume ya Huru ya Uchaguzi(mteule wa Raisi).

Sasa wadau hata kama leo hii Raisi ataamua kura ya maoni iitishwe kupitisha Katiba Inayopendekezwa na Katiba hiyo ikapita,Katiba Mpya itakayopatikana itaweza kutupatia Tume Huru ya Uchaguzi iwapo hao waheshimiwa hapo juu ndio watahusika kutupatia wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi?

Sitashangaa siku moja tukawa na katiba Mpya na kisha tukawa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba Mpya, lakini mwisho wa siku tukafuata nyayo za jirani zetu Kenya.

Africa ni shiida kwakweli!!
 
Leo hii nimeamua kupitia baadhi ya Ibara za katiba Inayopendekezwa na mojawapo ni Ibara ya 218(1) inayohusu Kamati ya Uteuzi ambayo itakuwa na wajibu wa kupokea na kuchambua maombi ya watu wanaomba kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

Kamati hii ya uteuzi,kwa mujibu wa Katiba Inayopendekezwa,itakuwa na wajibu ya kuteua Mwenyekit wa Tume Huru ya Uchaguzi,Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wengine saba wa Tume hii ya uchaguzi.

Wafuatao ndio watu watakuwa wajumbe wa Kamati hiyo ya uteuzi
na ambao ndio watachambua maombi ya watu wanaotaka kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi na kisha kuwasilisha majina ya wajumbe watakaochaguliwa kwa Raisi kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.

1.Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ndie atakuwa mwenyekiti wa kamati ya uteuzi

2 Jaji Mkuu wa Zanzibar ambae atakuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi.

3.Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano

4.Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi

5.Jaji Kiongozi

6.Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Na pia kutakuwa na katibu wa kamati hii ya uteuzi ambae atakuwa ni Mkurugenzi wa Tume ya Huru ya Uchaguzi(mteule wa Raisi).

Sasa wadau hata kama leo hii Raisi ataamua kura ya maoni iitishwe kupitisha Katiba Inayopendekezwa na Katiba hiyo ikapita,Katiba Mpya itakayopatikana itaweza kutupatia Tume Huru ya Uchaguzi iwapo hao waheshimiwa hapo juu ndio watahusika kutupatia wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi?

Sitashangaa siku moja tukawa na katiba Mpya na kisha tukawa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba Mpya, lakini mwisho wa siku tukafuata nyayo za jirani zetu Kenya.

Africa ni shiida kwakweli!!
Mkuu Salary Slip, kwanza asante sana kwa kuibua hoja hii, ambayo kwa maoni yangu, hii ndio ilipaswa kuwa hoja kipaumbele no. 1 kwa vyama vyote vya upinzani nchini, hata kama sio kusubiri hadi katiba mpya, wanaweza ku pressure sheria ya uchaguzi ifanyiwe marekebisho ili tupate Tume inayoitwa Tume Huru.

Kwenye hili la tume huru, kiukweli kabisa, hoja za wapinzani ni zile za hoja za mbaazi ikikosa maua, kwa sababu determinant ya uhuru wa Tume haupimwi na ni nani ameiteua, bali ni the electoral process, free, fair na maximum transparency.

Hoja kuwa Tume sii huru kwa sababu Mwenyekiti, Mkurugenzi na Makamishna wote wanateuliwa na rais, haina mashiko kwa sababu wajumbe wote wanaopendekezwa na katiba mpya wote pia ni wateule wa rais!.

Juzi kati Mkurugenzi wa NEC Ramadhani Kailima alithibitisha kuwa NEC ni tume huru. Kailima: Uchaguzi Ulikuwa huru na wa haki, CHADEMA imeshindwa kihalali! Hakuna upendeleo kwa CCM, NEC ni Tume huru

Malalamiko kuhusu kuibiwa kura pia NEC iliwahi kuyafafanua
TV Prog. Alert: Tume ya Uchaguzi, NEC, Yajibu Hoja za JF Kuhusu Uchaguzi Huru na Wa Haki!

TV Program Alert: Msidanywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia!
Mimi ni mtazamaji mzuri wa electoral game tangu tumeanza uchaguzi wa vyama vingi, kinachofanya wapinzani hawawezi kuchaguliwa, sio kuwa Tume sio huru, bali the playing field is not level, tunaweza kuwa na hiyo Tume inayoitwa huru, lakini kama the playing field is not level, wapinzani wataendelea kulia.

Paskali
 
Nashukuru sana ndugu kuletà mada hii. Mie tangu mwanzo nilitilià mashakà baadhi ya vipengele vilivyoko kwenye rasimu ya katiba ikiwemo eneo hili la namna ya kupata hii tume itakàyoitwa huru. Kwanza nimeona hakutakuwa na tofauti yoyote na hii ya sasa ya akina kailima. Sijajua nchi zilizoendelea kidemokrasia wao wanafanyaje katika hili labda wajuzi watusaidie. Kwa akili ya kawaida hao wateuaji hawawezi kwenda kinyume na bosi wao maana karibu wote ni wateule wa rais.
 
Leo hii nimeamua kupitia baadhi ya Ibara za katiba Inayopendekezwa na mojawapo ni Ibara ya 218(1) inayohusu Kamati ya Uteuzi ambayo itakuwa na wajibu wa kupokea na kuchambua maombi ya watu wanaomba kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

Kamati hii ya uteuzi,kwa mujibu wa Katiba Inayopendekezwa,itakuwa na wajibu ya kuteua Mwenyekit wa Tume Huru ya Uchaguzi,Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wengine saba wa Tume hii ya uchaguzi.

Wafuatao ndio watu watakuwa wajumbe wa Kamati hiyo ya uteuzi
na ambao ndio watachambua maombi ya watu wanaotaka kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi na kisha kuwasilisha majina ya wajumbe watakaochaguliwa kwa Raisi kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.

1.Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ndie atakuwa mwenyekiti wa kamati ya uteuzi

2 Jaji Mkuu wa Zanzibar ambae atakuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi.

3.Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano

4.Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi

5.Jaji Kiongozi

6.Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Na pia kutakuwa na katibu wa kamati hii ya uteuzi ambae atakuwa ni Mkurugenzi wa Tume ya Huru ya Uchaguzi(mteule wa Raisi).

Sasa wadau hata kama leo hii Raisi ataamua kura ya maoni iitishwe kupitisha Katiba Inayopendekezwa na Katiba hiyo ikapita,Katiba Mpya itakayopatikana itaweza kutupatia Tume Huru ya Uchaguzi iwapo hao waheshimiwa hapo juu ndio watahusika kutupatia wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi?

Sitashangaa siku moja tukawa na katiba Mpya na kisha tukawa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba Mpya, lakini mwisho wa siku tukafuata nyayo za jirani zetu Kenya.

Africa ni shiida kwakweli!!
una hoja ya msingi
 
Nashukuru sana ndugu kuletà mada hii. Mie tangu mwanzo nilitilià mashakà baadhi ya vipengele vilivyoko kwenye rasimu ya katiba ikiwemo eneo hili la namna ya kupata hii tume itakàyoitwa huru. Kwanza nimeona hakutakuwa na tofauti yoyote na hii ya sasa ya akina kailima. Sijajua nchi zilizoendelea kidemokrasia wao wanafanyaje katika hili labda wajuzi watusaidie. Kwa akili ya kawaida hao wateuaji hawawezi kwenda kinyume na bosi wao maana karibu wote ni wateule wa rais.
Tena ni bora Tume hiyo ingeundwa enzi za JK labda angalau ingefanana na kinachoitwa Tume Huru ila kwa awamu hii itakuwa ni mwendo wa maagizo kutoka juu.
 
Swali.nia yako uchaguzi Au Maendeleo. 15 uchaguzi. 16 uchaguzi. 17 uchaguzi. Lini utafanya kazi. Unadhani Tz tatizo uchaguzi. Uvivu. Umbeya. Na kukosa Maadili. Malezi ya kawaida kabisa tumekosa. Mitandao ndo imetuonyesha. Mnadakia technologia mwisho imeshawashinda. Unaamka asubhi Tu. siasa. Upande mwingine unatuambia wewe ndo inayokuandeshea maisha yako Au mwizi.
 
Wakati Tume huru inadaiwa kupitia Katiba Mpya, turekebishe pia Katiba za Vyama vyetu vya Siasa ambazo zinaruhusu Mwenyekiti wa Chama kuwa Mmoja huyo huyo kwa miaka zaidi ya 20 na mgombea Urais kuwa huyo huyo 1995, 2000, 2005, 2010, 2015 na bila shaka 2020 watakuwa hao hao.

Tume Huru mi naona ni Mtazamo tu, Tuangalie sheria, kanuni na Taratibu za chaguzi zetu na muihukumu Tume kupitia Ibara za Katiba na Vifungu na Kanuni za Kisheria zilokiukwa na sio vinginevyo, Kenya IEBC ni TUME huru na ODINGA alishiriki kikamilifu kuhakikisha wajumbe na watendaji wa Tume hiyo ni huru ,Kushindwa tu Uchaguzi tayari Tume sio huru
na hivi niulize kwanza Bunge letu lina Wabunge wa upinzani, hivi hawa Uchaguzi wao wao ulisimamiwa na Tume ipi.
na pia turudi kwenye teuzi za vyama vyetu kwenye Wabunge na Madiwani wanawake Viti Maalumu kuna malalamiko kibao so 'Kamati za Uchaguzi' za vyama vyetu nazo sio huru

kabla hujatoa boriti kwenye jicho la mwenzako angalia kwanza kibanzi kwenye jicho lako
 
Mkuu Salary Slip, kwanza asante sana kwa kuibua hoja hii, ambayo kwa maoni yangu, hii ndio ilipaswa kuwa hoja kipaumbele no. 1 kwa vyama vyote vya upinzani nchini, hata kama sio kusubiri hadi katiba mpya, wanaweza ku pressure sheria ya uchaguzi ifanyiwe marekebisho ili tupate Tume inayoitwa Tume Huru.

Kwenye hili la tume huru, kiukweli kabisa, hoja za wapinzani ni zile za hoja za mbaazi ikikosa maua, kwa sababu determinant ya uhuru wa Tume haupimwi na ni nani ameiteua, bali ni the electoral process, free, fair na maximum transparency.

Hoja kuwa Tume sii huru kwa sababu Mwenyekiti, Mkurugenzi na Makamishna wote wanateuliwa na rais, haina mashiko kwa sababu wajumbe wote wanaopendekezwa na katiba mpya wote pia ni wateule wa rais!.

Juzi kati Mkurugenzi wa NEC Ramadhani Kailima alithibitisha kuwa NEC ni tume huru. Kailima: Uchaguzi Ulikuwa huru na wa haki, CHADEMA imeshindwa kihalali! Hakuna upendeleo kwa CCM, NEC ni Tume huru

Malalamiko kuhusu kuibiwa kura pia NEC iliwahi kuyafafanua
TV Prog. Alert: Tume ya Uchaguzi, NEC, Yajibu Hoja za JF Kuhusu Uchaguzi Huru na Wa Haki!

TV Program Alert: Msidanywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia!
Mimi ni mtazamaji mzuri wa electoral game tangu tumeanza uchaguzi wa vyama vingi, kinachofanya wapinzani hawawezi kuchaguliwa, sio kuwa Tume sio huru, bali the playing field is not level, tunaweza kuwa na hiyo Tume inayoitwa huru, lakini kama the playing field is not level, wapinzani wataendelea kulia.

Paskali
Asante sana Pascal.

Sometimes huwa nafika mahali nashindwa hata niseme nini kuhusu siasa za nchi hii maana naona huko mbele naona ni giza tupu huku juhudi za kututoa kwenye hili giza zikiwa hazionekani.

Wapinzani, hasa wabunge wa upinzani, anzeni ku-raise hii issue huko Bungeni na nina hakika baada ya hapo hoja hii itapata msukumo mpya hata nje ya Bunge.

CC: Godbless J Lema Tumaini Makene
 
Swali.nia yako uchaguzi Au Maendeleo. 15 uchaguzi. 16 uchaguzi. 17 uchaguzi. Lini utafanya kazi. Unadhani Tz tatizo uchaguzi. Uvivu. Umbeya. Na kukosa Maadili. Malezi ya kawaida kabisa tumekosa. Mitandao ndo imetuonyesha. Mnadakia technologia mwisho imeshawashinda. Unaamka asubhi Tu. siasa. Upande mwingine unatuambia wewe ndo inayokuandeshea maisha yako Au mwizi.
Kwenye msafara wa mamba,hata kenge wamo.
 
Leo hii nimeamua kupitia baadhi ya Ibara za katiba Inayopendekezwa na mojawapo ni Ibara ya 218(1) inayohusu Kamati ya Uteuzi ambayo itakuwa na wajibu wa kupokea na kuchambua maombi ya watu wanaomba kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

Kamati hii ya uteuzi,kwa mujibu wa Katiba Inayopendekezwa,itakuwa na wajibu ya kuteua Mwenyekit wa Tume Huru ya Uchaguzi,Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wengine saba wa Tume hii ya uchaguzi.

Wafuatao ndio watu watakuwa wajumbe wa Kamati hiyo ya uteuzi
na ambao ndio watachambua maombi ya watu wanaotaka kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi na kisha kuwasilisha majina ya wajumbe watakaochaguliwa kwa Raisi kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.

1.Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ndie atakuwa mwenyekiti wa kamati ya uteuzi

2 Jaji Mkuu wa Zanzibar ambae atakuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi.

3.Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano

4.Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi

5.Jaji Kiongozi

6.Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Na pia kutakuwa na katibu wa kamati hii ya uteuzi ambae atakuwa ni Mkurugenzi wa Tume ya Huru ya Uchaguzi(mteule wa Raisi).

Sasa wadau hata kama leo hii Raisi ataamua kura ya maoni iitishwe kupitisha Katiba Inayopendekezwa na Katiba hiyo ikapita,Katiba Mpya itakayopatikana itaweza kutupatia Tume Huru ya Uchaguzi iwapo hao waheshimiwa hapo juu ndio watahusika kutupatia wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi?

Sitashangaa siku moja tukawa na katiba Mpya na kisha tukawa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba Mpya, lakini mwisho wa siku tukafuata nyayo za jirani zetu Kenya.

Africa ni shiida kwakweli!!
Ile katina ya sita ni bomu
 
Wananchi wanahitaji maendeleo hawahitaji TUME HURU, KATIBA MPYA wala sijui ujinga gani. Nyie mnapigania katiba mkiamini itawasaidia akina Lowassa ,Mbowe na genge lao la wanyang'anyi kuingia ikulu. Na mtasubiri mpaka Yesu arudi labda kije kizazi kingine cha upinzani ndo kipewe kuongoza nchi hii vinginevyo ni ndoto kumuona mamvi IKULU. Na unavyohangaika na SIASA mwaka 2020 utakuja kuwa kichaa na kuokota makopo utakapofanyika uchaguzi mkaibuka na wabunge 7 na madiwani 4 nchi nzima ndo utajua mziki wa JPM sio wa kitoto.
 
TV Program Alert: Msidanywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia!
Mimi ni mtazamaji mzuri wa electoral game tangu tumeanza uchaguzi wa vyama vingi, kinachofanya wapinzani hawawezi kuchaguliwa, sio kuwa Tume sio huru, bali the playing field is not level, tunaweza kuwa na hiyo Tume inayoitwa huru, lakini kama the playing field is not level, wapinzani wataendelea kulia.

Paskali

Mkuu nakubaliana na wewe nusu kuwa tume ipi huru, in reality uchaguzi wa 2015, process yote kupiga mnpaka kuhasabu na kujumlisha kura vituoni ilikuwa huru tena huru sana.changamoto ilikuw ainaanzia kwenye majumuishi kule katani kw audiwani na halmashahuri kwa wabunge na pia tallying center kwa uraisi, kiukwlei kwneye majumuishi hasa ya uraisi ilikuw angumu sana kuthibitisha kuw akura zinazojumlishw ani sahihi, maana unakuta tume inaingiza kura za jimbo A, lakini upinzani hawana karatasi yao ya kuonyesha idadi ya kura kwenye kituo A. wakati ilipaswa tme wakubaliane na wasimamizi wa upinzani ndipo kura zitangazwe.

kuongzea pia kuna ishi za wasimamizi wa upinzani kwenye vituo mpaka majumuisho, kiukweli hakuna na waliopo walikuwa hawana uwezo wa kusimamia ipasavyo sabau ziukiwa ni nyingi moja wapo kubwa posho kwa wasimamizi hawa haikuwepo.

kwenye majimbo ambayo wapinzani walisimamia kura kuanzia vituoni mpaka majumuishio walishinda na hawakuibiwa.
 
Leo hii nimeamua kupitia baadhi ya Ibara za katiba Inayopendekezwa na mojawapo ni Ibara ya 218(1) inayohusu Kamati ya Uteuzi ambayo itakuwa na wajibu wa kupokea na kuchambua maombi ya watu wanaomba kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

Kamati hii ya uteuzi,kwa mujibu wa Katiba Inayopendekezwa,itakuwa na wajibu ya kuteua Mwenyekit wa Tume Huru ya Uchaguzi,Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wengine saba wa Tume hii ya uchaguzi.

Wafuatao ndio watu watakuwa wajumbe wa Kamati hiyo ya uteuzi
na ambao ndio watachambua maombi ya watu wanaotaka kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi na kisha kuwasilisha majina ya wajumbe watakaochaguliwa kwa Raisi kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.

1.Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ndie atakuwa mwenyekiti wa kamati ya uteuzi

2 Jaji Mkuu wa Zanzibar ambae atakuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi.

3.Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano

4.Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi

5.Jaji Kiongozi

6.Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Na pia kutakuwa na katibu wa kamati hii ya uteuzi ambae atakuwa ni Mkurugenzi wa Tume ya Huru ya Uchaguzi(mteule wa Raisi).

Sasa wadau hata kama leo hii Raisi ataamua kura ya maoni iitishwe kupitisha Katiba Inayopendekezwa na Katiba hiyo ikapita,Katiba Mpya itakayopatikana itaweza kutupatia Tume Huru ya Uchaguzi iwapo hao waheshimiwa hapo juu ndio watahusika kutupatia wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi?

Sitashangaa siku moja tukawa na katiba Mpya na kisha tukawa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba Mpya, lakini mwisho wa siku tukafuata nyayo za jirani zetu Kenya.

Africa ni shiida kwakweli!!
Umenena vyema, ila usisome ibara moja ukakomaa nayo kama mlokole, katiba ili uielewe lazima uisome yote kwa kuhusianisha ibara mbalimbali.

Maana yangu ni kua, wakati hilo litapotimia, hata hao wajumbe watakua sio wateule wa Rais tena, na wao watakua wamepitia mchakato huru wenye kuzingatia vigezo stahiki kuwapata. Sasa kwakua ni watu huru hawatakua na shinikizo lolote.

Kwa uelewa angalia namna ya kumpata Jaji Mkuu, Jaji Kiongozi, Spika na hao wengine katika ibara za katiba hio pendekezwa.
 
Wakati Tume huru inadaiwa kupitia Katiba Mpya, turekebishe pia Katiba za Vyama vyetu vya Siasa ambazo zinaruhusu Mwenyekiti wa Chama kuwa Mmoja huyo huyo kwa miaka zaidi ya 20 na mgombea Urais kuwa huyo huyo 1995, 2000, 2005, 2010, 2015 na bila shaka 2020 watakuwa hao hao.

Tume Huru mi naona ni Mtazamo tu, Tuangalie sheria, kanuni na Taratibu za chaguzi zetu na muihukumu Tume kupitia Ibara za Katiba na Vifungu na Kanuni za Kisheria zilokiukwa na sio vinginevyo, Kenya IEBC ni TUME huru na ODINGA alishiriki kikamilifu kuhakikisha wajumbe na watendaji wa Tume hiyo ni huru ,Kushindwa tu Uchaguzi tayari Tume sio huru
na hivi niulize kwanza Bunge letu lina Wabunge wa upinzani, hivi hawa Uchaguzi wao wao ulisimamiwa na Tume ipi.
na pia turudi kwenye teuzi za vyama vyetu kwenye Wabunge na Madiwani wanawake Viti Maalumu kuna malalamiko kibao so 'Kamati za Uchaguzi' za vyama vyetu nazo sio huru

kabla hujatoa boriti kwenye jicho la mwenzako angalia kwanza kibanzi kwenye jicho lako
Sasa we ushaingiza siasa, upinzani Mara ccm, hapa tunajadili kuhusu TUME, hivi kwanini mnapenda kutoa watu kwenye reli, mnafaidika nin? Inasikitisha sana
 
Umenena vyema, ila usisome ibara moja ukakomaa nayo kama mlokole, katiba ili uielewe lazima uisome yote kwa kuhusianisha ibara mbalimbali.

Maana yangu ni kua, wakati hilo litapotimia, hata hao wajumbe watakua sio wateule wa Rais tena, na wao watakua wamepitia mchakato huru wenye kuzingatia vigezo stahiki kuwapata. Sasa kwakua ni watu huru hawatakua na shinikizo lolote.

Kwa uelewa angalia namna ya kumpata Jaji Mkuu, Jaji Kiongozi, Spika na hao wengine katika ibara za katiba hio pendekezwa.
Tume ya utmishi ya Mahakama ikishafanya uteuzi wa hao ulioataja inapeleka majina kwa Raisi ili afanye uteuzi wa mwisho.

Soma vizuri katiba inayopendekezwa utaona hilo nalokwambia.
 
Back
Top Bottom