Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,986
- 144,313
Leo hii nimeamua kupitia baadhi ya Ibara za katiba Inayopendekezwa na mojawapo ni Ibara ya 218(1) inayohusu Kamati ya Uteuzi ambayo itakuwa na wajibu wa kupokea na kuchambua maombi ya watu wanaomba kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.
Kamati hii ya uteuzi,kwa mujibu wa Katiba Inayopendekezwa,itakuwa na wajibu ya kuteua Mwenyekit wa Tume Huru ya Uchaguzi,Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wengine saba wa Tume hii ya uchaguzi.
Wafuatao ndio watu watakuwa wajumbe wa Kamati hiyo ya uteuzi
na ambao ndio watachambua maombi ya watu wanaotaka kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi na kisha kuwasilisha majina ya wajumbe watakaochaguliwa kwa Raisi kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.
1.Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ndie atakuwa mwenyekiti wa kamati ya uteuzi
2 Jaji Mkuu wa Zanzibar ambae atakuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi.
3.Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano
4.Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi
5.Jaji Kiongozi
6.Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma
Na pia kutakuwa na katibu wa kamati hii ya uteuzi ambae atakuwa ni Mkurugenzi wa Tume ya Huru ya Uchaguzi(mteule wa Raisi).
Sasa wadau hata kama leo hii Raisi ataamua kura ya maoni iitishwe kupitisha Katiba Inayopendekezwa na Katiba hiyo ikapita,Katiba Mpya itakayopatikana itaweza kutupatia Tume Huru ya Uchaguzi iwapo hao waheshimiwa hapo juu ndio watahusika kutupatia wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi?
Sitashangaa siku moja tukawa na katiba Mpya na kisha tukawa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba Mpya, lakini mwisho wa siku tukafuata nyayo za jirani zetu Kenya.
Africa ni shiida kwakweli!!
Kamati hii ya uteuzi,kwa mujibu wa Katiba Inayopendekezwa,itakuwa na wajibu ya kuteua Mwenyekit wa Tume Huru ya Uchaguzi,Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wengine saba wa Tume hii ya uchaguzi.
Wafuatao ndio watu watakuwa wajumbe wa Kamati hiyo ya uteuzi
na ambao ndio watachambua maombi ya watu wanaotaka kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi na kisha kuwasilisha majina ya wajumbe watakaochaguliwa kwa Raisi kwa ajili ya uteuzi wa mwisho.
1.Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ndie atakuwa mwenyekiti wa kamati ya uteuzi
2 Jaji Mkuu wa Zanzibar ambae atakuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi.
3.Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano
4.Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi
5.Jaji Kiongozi
6.Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma
Na pia kutakuwa na katibu wa kamati hii ya uteuzi ambae atakuwa ni Mkurugenzi wa Tume ya Huru ya Uchaguzi(mteule wa Raisi).
Sasa wadau hata kama leo hii Raisi ataamua kura ya maoni iitishwe kupitisha Katiba Inayopendekezwa na Katiba hiyo ikapita,Katiba Mpya itakayopatikana itaweza kutupatia Tume Huru ya Uchaguzi iwapo hao waheshimiwa hapo juu ndio watahusika kutupatia wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi?
Sitashangaa siku moja tukawa na katiba Mpya na kisha tukawa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa mujibu wa Katiba Mpya, lakini mwisho wa siku tukafuata nyayo za jirani zetu Kenya.
Africa ni shiida kwakweli!!