Kamarada Amos Makalla tafadhali Wewe ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na wala si Mkuu wa Mkoa wa CCM Dar es Salaam

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,865
Katika Mtu ambaye GENTAMYCINE nimepanga nisiwe namsema ( namsiliba ) hapa JamiiForums kutokana na kuwa ni Mdau wangu mkubwa wa Miziki ya Congo DR ( Misebene ), Mwana Simba SC Mwenzangu na Mtoto wa Mjin vile vile ni Wewe Amos Makalla ( Mkuu wa Mkoa mpya wa Dar es Salaam )

Pacha ( Mdau ) Amos Makalla nimesikitika sana na Taarifa niliyoiona katika Mitandao mbalimbali ( japo bado naithibitisha ) kuwa umesema kuwa kila baada ya Miezi Mitatu utakuwa unakutana na Wazee wa CCM ili uchote Uzoefu wao na Wakufunde zaidi.

Tafadhali sana Pacha ( Mdau ) Amos Makalla kwa hili utaharibu na Mimi GENTAMYCINE kwa Heshima na Taadhima nakuomba libadilishe na badala yake kutana tu na Wazee wote bila kuweka Itikadi ya Siasa uliyonayo hasa ukiwa ni mwana CCM Mwenzangu.

Pacha ( Mdau ) Amos Makalla Wewe ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na siyo Mkuu wa Mkoa wa CCM Dar es Salaam na nimeshtuka mno kuona Mtu kama Wewe umekuja na wazo la ' Kiubaguzi ' na la ' Kipuuzi ' pia kama hili ambalo binafsi pia bila Urafiki wala Kukuonea Aibu niseme tu kuwa limenikwaza zaidi.

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere huko nyuma alipenda sana Kukutana na Wazee mbalimbali na hakuwahi ' Kuwabagua ' kwa namna yoyote ile hali ambayo iliwautia Wazee wengi bila kujali tofauti zao za Kiitikadi, Kiukabila na Kidini Kujumuika nae na kumpa Mawazo ( Ushauri ) ambao ndiyo ulikuwa Chachu ya kumfanya atuongoze vyema kama Taifa na Watanzania mpaka leo hii tunamkumbuka na hata wakati mwingine Kumlilia.

Pacha ( Mdau ) Amos Makalla nani alikuambia kuwa Wazee wa Vyama vya Upinzani waliopo hapa Mkoani Dar es Salaam hawana Mawazo mazuri ya Kukushauri tena huenda hata ya Kuwazidi hao Wazee wa CCM ambao Wewe unawaona ni bora Kwako kwa Sisi tunawajua kuwa wengi wao ni Wanafiki watupu na wakija Kukutana nawe sana sana watakachokuwa Wanakushauri ni Umbea, Majungu, Uzandiki na kukuonyesha aina mpya ya Waganga wa Kienyeji ili uende ' Ukajigange ' zaidi kusudi ' Mama ' asiwaze kabisa ama Kukuhamisha na Kukutumbua.

Usianze vibaya mapema yote hii Pacha.
 
Heading tu ya hii mada! Ajitafakari
😅 😅😅 Makalla ubunge tu wa Mvomero, ulimshinda, hebu tulione picha la uRC mkoa wa fitina za kina fudenge.

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Ameanza na mguu was kushoto! Hata dumu hapa dar. Inawezekana ndiyo maana hata magu alimtema Ana kaujinga flani.
Mkuu ndio ameanza na mguu wa kushoto, ila kwa dini zetu una dua yake. Tusubili tuone. YAJAYO YANAFURAHISHA. Vipi kuhusu wamachinga, vibanda vyao bado vipo? maana muda umeshapita!
 
Merci mingi Genta ..mdau wa BCBG asikie hiyo na asome Alama za Nyakati...
Amos Makalla ni mwana Wenge BCBG Mwenzangu na mpenda Misebene ya Kikongo sijui ni nini tena kimemkumba hadi anataka kuanza vibaya hivi. Naanza kuhisi huenda ameanza ' Kurogwa ' na wanaokitaka hicho Cheo kwani ukiwa RC wa Dar ni ' Ulaji ' mtupu tu

Namwomba aubadilishe huo Utaratibu aliouandaa badala yake akutane na Wazee wote tu bila Kujali Political Affiliations zao. Itamjenga na Kumsaidia zaidi hasa katika kupata Ushirikiano wa Kimaendeleo kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
 
Amos Makalla ni mwana Wenge BCBG Mwenzangu na mpenda Misebene ya Kikongo sijui ni nini tena kimemkumba hadi anataka kuanza vibaya hivi. Naanza kuhisi huenda ameanza ' Kurogwa ' na wanaokitaka hicho Cheo kwani ukiwa RC wa Dar ni ' Ulaji ' mtupu tu

Namwomba aubadilishe huo Utaratibu aliouandaa badala yake akutane na Wazee wote tu bila Kujali Political Affiliations zao. Itamjenga na Kumsaidia zaidi hasa katika kupata Ushirikiano wa Kimaendeleo kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
Na Wenge BCBG MEGA CLAN hatunaga ubaguzi Werrasonian na Jibeniaqe yote ni Famili moya...

Makalla mtani wangu Ajitazame kama Mukulu Genta anavyo kushauri...
 
Mkuu RC Kwa Dar, wazee ni wote above 60 years tu, hamnaga zaidi. Usilete ubaguzi wowote wa elimu, dini wala ukabila! Wote ni wako. Inawezekana ukategemea wale ambao unawaamini watakupatia USHAURI BORA ikawa ndivyo sivyo.
 
Back
Top Bottom