Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
RPC mstaafu achaguliwa mwenyekiti CCM Arusha
Inamaanisha alikuwa na kadi toka akiwa polisi, then hawa na waliopo watatendaje haki kwa upinzani?
===
RPC mstaafu achaguliwa mwenyekiti CCM Arusha
Kwa ufupi
Aliyewahi kuwa Kamanda wa Polisi (RPC) amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuchukua nafasi ya Loota Sanare ambaye hivi karibuni aliteuliwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuchukua nafasi ya Dk Stephen Kebwe ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Arusha. Kamanda wa Polisi mstaafu nchini Tanzania, Zolothe Steven amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama tawala (CCM) Mkoa wa Arusha.
Zelothe amechaguliwa leo Jumanne Desemba 17, 2019 na wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa uchaguzi uliosimamiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphrey Polepole.
Akitangaza matokeo, Polepole amesema Zolethe amepata kura 468 dhidi ya kura 339 za waziri wa zamani wa mazingira, Dk Batilda Burian na Bakari Msangi amepata kura 42 kati ya kura zilizopigwa ni 850
Polepole amesema kura iliyoharibika ilikuwa moja huku kura halali zikiwa 849.
Zolothe anachukua nafasi ya Loota Sanare ambaye hivi karibuni aliteuliwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuchukua nafasi ya Dk Stephen Kebwe ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
RPC mstaafu achaguliwa mwenyekiti CCM Arusha
Inamaanisha alikuwa na kadi toka akiwa polisi, then hawa na waliopo watatendaje haki kwa upinzani?
===
RPC mstaafu achaguliwa mwenyekiti CCM Arusha
Kwa ufupi
Aliyewahi kuwa Kamanda wa Polisi (RPC) amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuchukua nafasi ya Loota Sanare ambaye hivi karibuni aliteuliwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuchukua nafasi ya Dk Stephen Kebwe ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Arusha. Kamanda wa Polisi mstaafu nchini Tanzania, Zolothe Steven amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama tawala (CCM) Mkoa wa Arusha.
Zelothe amechaguliwa leo Jumanne Desemba 17, 2019 na wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa uchaguzi uliosimamiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphrey Polepole.
Akitangaza matokeo, Polepole amesema Zolethe amepata kura 468 dhidi ya kura 339 za waziri wa zamani wa mazingira, Dk Batilda Burian na Bakari Msangi amepata kura 42 kati ya kura zilizopigwa ni 850
Polepole amesema kura iliyoharibika ilikuwa moja huku kura halali zikiwa 849.
Zolothe anachukua nafasi ya Loota Sanare ambaye hivi karibuni aliteuliwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuchukua nafasi ya Dk Stephen Kebwe ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
RPC mstaafu achaguliwa mwenyekiti CCM Arusha