kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,991
- 17,888
Kamanda wa IRGC: Uingereza na Marekani zitajuta kwa kuizuilia meli ya mafuta ya Iran
Jul 12, 2019 02:26 UTC
Naibu Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) ameonya kuwa, Uingereza na Marekani zitajuta kutokana na hatua ya London ya kusimamisha na kuzuilia meli ya mafuta ya Iran katika Lango Bahari la Jabal Tariq (Gibraltar).
Admeri Ali Fadavi alisema hayo jana Alkhamisi katika mkoa wa Isfahan, katikati ya Iran na kuongeza kuwa, "Kitendo chao (Uingereza na Marekani) cha kuzuia meli ya mafuta ya Iran ni cha kipuuzi na karibuni hivi watajuta na kuomba msamaha."
Ameeleza bayana kuwa, hatua ya kuzuia meli ya mafuta ya Iran ni ukiukaji wa kanuni na sheria za kimataifa na kamwe kitendo hicho hakitapita hivi hivi bila kupewa jibu mwafaka.
Naibu Kamanda wa SEPAH amesisitiza kuwa, maadui hawana ujasiri na uthubutu wa kufyatua japo risasi moja dhidi ya Iran na wenyewe wamekiri mara kadhaa kuwa njama zao dhidi ya taifa hili zimegonga mwamba.
Katika kuhalalisha hatua yake hiyo ya Alkhamisi ya wiki iliyopita, Uingereza ilidai kwamba inaiuzuilia meli hiyo ya mafuta ya Iran kwa kuwa imekiuka vikwazo vya Marekani na vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Syria vilivyowekwa mwaka 2011. London ilidai kuwa meli hiyo ya mafuta ilikuwa inaelekea Syria.
Hata hivyo, Brigedia Jenerali Amir Hatami, Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hivi karibuni aliashiria hatua hiyo ya askari wa Jeshi la Wanamaji la Uingereza ya kuisimamisha meli ya mafuta ya Iran katika Lango Bahari la Jabal al Tariq (Gibraltar) na kueleza bayana kuwa, Tehran kamwe haitafumbia macho uharamia huo wa London.
Tags
IRAN MAREKANI UINGEREZA
Jul 12, 2019 02:26 UTC
Naibu Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) ameonya kuwa, Uingereza na Marekani zitajuta kutokana na hatua ya London ya kusimamisha na kuzuilia meli ya mafuta ya Iran katika Lango Bahari la Jabal Tariq (Gibraltar).
Admeri Ali Fadavi alisema hayo jana Alkhamisi katika mkoa wa Isfahan, katikati ya Iran na kuongeza kuwa, "Kitendo chao (Uingereza na Marekani) cha kuzuia meli ya mafuta ya Iran ni cha kipuuzi na karibuni hivi watajuta na kuomba msamaha."
Ameeleza bayana kuwa, hatua ya kuzuia meli ya mafuta ya Iran ni ukiukaji wa kanuni na sheria za kimataifa na kamwe kitendo hicho hakitapita hivi hivi bila kupewa jibu mwafaka.
Naibu Kamanda wa SEPAH amesisitiza kuwa, maadui hawana ujasiri na uthubutu wa kufyatua japo risasi moja dhidi ya Iran na wenyewe wamekiri mara kadhaa kuwa njama zao dhidi ya taifa hili zimegonga mwamba.
Katika kuhalalisha hatua yake hiyo ya Alkhamisi ya wiki iliyopita, Uingereza ilidai kwamba inaiuzuilia meli hiyo ya mafuta ya Iran kwa kuwa imekiuka vikwazo vya Marekani na vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Syria vilivyowekwa mwaka 2011. London ilidai kuwa meli hiyo ya mafuta ilikuwa inaelekea Syria.
Hata hivyo, Brigedia Jenerali Amir Hatami, Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hivi karibuni aliashiria hatua hiyo ya askari wa Jeshi la Wanamaji la Uingereza ya kuisimamisha meli ya mafuta ya Iran katika Lango Bahari la Jabal al Tariq (Gibraltar) na kueleza bayana kuwa, Tehran kamwe haitafumbia macho uharamia huo wa London.
Tags
IRAN MAREKANI UINGEREZA