mgt software
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 13,767
- 7,115
wana JF,
Mikakati ya kumpokea Tundu Lissu imeiva akiwa anarejea kutoka ughaibuni, kwa vile Lissu ni kipenzi cha wengi, hakuna haja ya kuvalia uniform kuonyesha kuwa wewe ni wa chama fulani, bali tunavaa kawaida sana nguo za nyumbani.
Kwa vile wenye mapenzi naye ni mchanganyiko wa vyama vyote Serikali iweke ulinzi apokelewe salamu tusije kutumia nguvu pasipostahili tukakuta tunawaumiza wapiga kura wetu au kuumiza wasio husika kama ndege atakayopanda inawezekana ikawa na watalii wa nchi mbalimbali, wasafiri wa aina nyingi, wafanyabiashara na wawekezaji.
Kamanda Sirro haya mapokezi usiyachukulie ya kisiasa, ni kwa mapenzi tu ya mtu kwani ikiingiza siasa, hata huko CHADEMA kuna maadui na mahasimu wake, hata CCM kuna maadui na mahasimu wake lakini pia kuna marafiki wake nje ya game, ndio maana kwenye familia yake , kuna ambao ni CCM kindakindaki lakini linapokuja suala la udugu vyama tunaweka pembeni.
Wengine wanakuja kumsagaa Lissu ni mzimu unaotembea au vipi, haiwezekani mtu akapigwa risasi 18 alafu akapona kirahisi hivi.
Kingine kwa kuwa mgombea huyu anaweza kupitishwa na chama kwa sasa angeachwa atulie aje kwa amani ili asiongezewe stress ili ajumuike na wenzie katika ushindani.
Mikakati ya kumpokea Tundu Lissu imeiva akiwa anarejea kutoka ughaibuni, kwa vile Lissu ni kipenzi cha wengi, hakuna haja ya kuvalia uniform kuonyesha kuwa wewe ni wa chama fulani, bali tunavaa kawaida sana nguo za nyumbani.
Kwa vile wenye mapenzi naye ni mchanganyiko wa vyama vyote Serikali iweke ulinzi apokelewe salamu tusije kutumia nguvu pasipostahili tukakuta tunawaumiza wapiga kura wetu au kuumiza wasio husika kama ndege atakayopanda inawezekana ikawa na watalii wa nchi mbalimbali, wasafiri wa aina nyingi, wafanyabiashara na wawekezaji.
Kamanda Sirro haya mapokezi usiyachukulie ya kisiasa, ni kwa mapenzi tu ya mtu kwani ikiingiza siasa, hata huko CHADEMA kuna maadui na mahasimu wake, hata CCM kuna maadui na mahasimu wake lakini pia kuna marafiki wake nje ya game, ndio maana kwenye familia yake , kuna ambao ni CCM kindakindaki lakini linapokuja suala la udugu vyama tunaweka pembeni.
Wengine wanakuja kumsagaa Lissu ni mzimu unaotembea au vipi, haiwezekani mtu akapigwa risasi 18 alafu akapona kirahisi hivi.
Kingine kwa kuwa mgombea huyu anaweza kupitishwa na chama kwa sasa angeachwa atulie aje kwa amani ili asiongezewe stress ili ajumuike na wenzie katika ushindani.