Kamanda Sirro,tafadhali litakafakari tena agizo lako kuhusu bodaboda

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,193
25,504
Tangu asubuhi ya leo kumekuwa kukiripotiwa kuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Simon Sirro ameagiza kuwa pikipiki ziishie saa tano usiku. Ndiyo kusema kuwa usafiri wa pikipiki utasita muda huo

Tunakubaliana kuwa ulinzi na usalama ni lengo kuu la kinchi huku Jeshi la Polisi wakilisimamia vyema lengo hilo. Tunakubaliana pia kuwa Jeshi la Polisi linafanya kazi ya kutukuka katika kulinda watu na mali zao. Ipo wazi kuwa Kamanda Sirro ametoa agizo lake kwakuwa ana sababu zake

Kwa kuzingatia mazingira ya jiji la Dar,pikipiki hazipaswi kupigwa marufuku kuanzia saa tano usiku. Yapo mabasi ya mikoani yanayowasili Dar hadi saa sita usiku. Pikipiki huwa msaada. Wapo wananchi wanaorejea makwao hadi kuanzia saa sita usiku. Pikipiki huwasaidia sana wananchi hao.

Tafadhali Kamanda Sirro,tafakari upya katazo lako. Kinachopaswa kufanyika ni kuimarisha ulinzi na utaratibu mzuri katika nia ya kuzuia pikipiki kutumika katika uhalifu.
 
Mama ndalichako aliwahi kutoa mtazamo wake juu ya wahitimu wa ngazi mbali mbali kuvaa majoho wakati wa mahafali, Siku chache baadaye 'Mtazamo' wake uligeuka sheria.

Awamu hii ya 5 unaposikia mtazamo wa 'Boss' wako juu ya jambo fulani inakupasa usihoji wala kushauri, inakupasa mara moja uuchukue kama sheria
 
Ha
Fata kauli yake usifuate magazeti.. Magazeti ya Tz sio km huyajuwi kwa kupindisha
Halafu Jenerali (Media na press guru), anayatetea kwa upotoshaji wa namna hii bila kuyakanya baadhi yanayoharibu tasnia ya habari.
 
Nimestushwa na katazo hilo nikizingatia muda ninaorudi nyumbani siku zote na ki ukweli sio mimi pekee Bali ni kundi la wananchi wengi(has a Dar),kwani Saa hizo 6,7 mpaka 8 za usiku ni watu wengi huwa wanarudi majumbani kwa usafiri Wa daladala na wengi wetu baada ya kushuka kwenye basi huwa kwa haraka tunarukia Pikipiki ambazo huingia njia ambazo in ndefu na zisizo na means yeyote ya usafiri nyakati hizo, hutufikisha mpaka kwenye mageti au nje ya nyumba zetu na tunaingia ndani tukiwa salama
Kwa katazo hili nahisi tutakua hatarini sana pindi tutapokua tukirudi nyumbani,ushauri kwa jeshi na hasa kamanda wetu Wa Dar aliangalie hili kwa mapana yake,usafiri huo unatuokoa kwa Massa 24,zaidi jeshi lichukulie waharifu wachache wanaotumia bodaboda kama changamoto mpya.
 
Kamanda embu licheki tena hili tangazo lako,,boda boda ni usafiri wetu mkubwa,,dar hakuna kulala,,embu check upya
 
Fata kauli yake usifuate magazeti.. Magazeti ya Tz sio km huyajuwi kwa kupindisha
Kauli yake inasafirishwa kupitia vyombo vya habari. Siyo askari wote wameusikia ushauri wake, wengine wataugeuza kuwa sheria. Inafaa sasa aje na kauli nyingine ya kugeuza huo ushauri ili bodaboda waendelee kutoa huduma
 
Asifikiri wote tunakaa hapo tu karibu na oysterbay polisi na wote tuna usafiri!! Ajipime kama alifanya utafiti kwenye kauli yake
 
magazeti mkuu achana nayo, kwa sasa kunamstari mwembamba sana unaotofautisha magazeti rasmi na magazeti ya udaku. ni afadhali Taarifa ya habari kuliko magazeti
Business first, taifa baadae

Mkuu sipingi hilo la udhaifu wa magazeti lakini hili la kamanda Sirro lisipopingwa usishangae kuwa ni sheria isiyo rasmi. Ni wangapi wasiojua utendaji wa polisi unaotegemea hisia zao bila kuangalia uhalisia? Yeye Kamanda Sirro anashauri kuanzia saa 5 ili kutokomeza uhalifu lakini yeye anapata usafiri wa bure na kwake ana mlinzi hivyo hajui sisi wengine tunasafiri vipi. Waandae utaratibu mzuri wa kupambana na uhalifu na sio kuzuia bodaboda kuanzia saa 5.
 
Wasifanye kazi tu kwa hoja kubwa moja,wanauliwa wengi hawa dereva wa bodaboda n kuibiwa pikipiki zao usiku.
Lkn nao boda boda wezi wanaibia watu wenye pochi au simu wanazitembea nazo mikononi
 
Hata kama ni ushauri ametoa ushauri feki kweli kweli kwa jiji kama la DSM ambalo ni 24hrs live City,
 
Kesho kutwa uhalifu ukifanyika sana kwa magari tutegemee Sirro atapiga marufuku matumizi ya magari mida ya usiku.
 
Hii kauli imenishangaza sana, jeshi letu inabidi liwe bunifu kulinda raia sio kila siku kutoa mazuio tu, lazima tupambane muda wa kazi uwe 24/7 nchi hii ili kukuza uchumi lakini kila uchao wao wanafikiria kumaliza kila shughuli saa 6 usiku. Wabadilike tunaenda mbele haturudi nyuma, wafikirie mbinu za kisasa zaidi, hili katazo ni baya sana kiuchumi.
 
Back
Top Bottom