Kamanda Siro naye ujiandae kutolewa kafara kwa sakata la Lisu. Ngoja mzoga uvunde zaudi utanikumbuka.

Sexless

JF-Expert Member
Mar 11, 2017
21,567
50,393
Sote leo tumeshuhudia leo kamanda Mambosasa akitolewa kafara kwa sakata la kutekwa kwa Mo Dewji. Anachokishangaa leo JPM akina Godbless Lema walikishangaa tangu siku ya kwanza mpk wakaitwa central. Ndiyo maana tunasema Mambosasa anatolewa kafara.

Tuachane na hilo tuje sasa kwa IGP siro. Kete ya mwisho ya serikali ya JPM kujiepusha na uvundo wa mzoga wa "sakata la kushambuliwa kwa Tundu Lisu" ni kumteua Prof. Kabudi kuwa waziri wa mambo ya nje.

Kama mmeisikiliza hotuba ya Prof huyu wakati akiapishwa kuitumikia wizara ya mambo ya nje ametamba kumshughulikia Lisu (japo hakumtaja kwa jina).

Mara baada ya kete hiyo kushindikana serikali ya JPM itaanza kutoa watu kafara. Siro ndiye kafara iliyo nona katika sakata hili. Namhakikishia kamanda Siro atapata tabu sana. Hakika hataamini!
 
Nadhani alishaelezea vizuri.
tapatalk_1540369072909.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zile kauli kuwa amri kutoka Juu ndio nani kwani huyo Juu? Maana zimesababisha Polisi kuvunja Sheria za Kazi bila umuhimu wowote ule... kwanini tusiishi kama nchi zilizoendelea haki kwanza na hakuna aliyejuu ya Sheria.. Kiongozi wako akikutuma uvunje sheria unam arrest tu... kwani anakuwa amejifukuzisha kazi tu.
 
Back
Top Bottom