Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Kamanda Nzowa wa kikosi cha kuzuia madawa ya kulevya amejitokeza na kumtaja Mch. Kuchupu Denis Okechuku wa kanisa moja la 'kiroho' lililopo maeneo ya Kinondoni Biafra, kuwa ni mmoja wa wachungaji wanaotuhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya. Amesema akiwa pamoja na watu wengine mchungaji huyo alikamatwa na kilo 81 za cocaine mapema mwaka huu, na kuwa katika pile ya watuhumiwa wa matukio mbalimbali ya madawa ya kulevya, wapo pia viongozi wengine kadhaa wa kidini, ambao watatajwa baadae.
Source; Channel ten (Kipindi cha Baragumu leo asubuhi)
Source; Channel ten (Kipindi cha Baragumu leo asubuhi)