Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
LIVE: Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM Lazaro Mambosasa anazungumza kuhusu kilichotokea juzi Segerea wakati Freeman Mbowe akisubiriwa kutoka gerezani
=====
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA UMMA.
KUKAMATWA KWA WAFUASI WA CHADEMA 27 KWA TUHUMA ZA KUFANYA FUJO KATIKA GEREZA LA MAHABUSU SEGEREA.
Mnamo tarehe 13.03.2020 majira ya saa 07:00 mchana Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam lilipokea taarifa kutoka kwa maofisa wa Gereza la Mahabusu Segerea kuwa kuna kundi la wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) likiongozwa na wabumbe wawili ambao ni Halima James Mdee, Ester Amos Bulaya na Meya wa Ubungo Boniface Jacob limekusanyika katika geti la kuingilia gerezani hapo huku likiandamana na kufanya fujo kutaka kuingia kwa nguvu ndani ya gereza kwa lengo la kwenda kumtoa mwenyekiti wa chama chao Mhe.Freeman Mbowe.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum baada ya kupokea taarifa hizo lilituma askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) na askari wa kituo cha Polisi Stakishari na ambapo walipofika eneo hilo waliwakuta askari magereza wakiwa wanaendelea kuwadhibiti wanachama hao na ndipo Polisi walipowakamata watuhumiwa 27.
Baada ya watuhumiwa hao kukamatwa askari wa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na askari wa Jeshi la magereza waliwachukua na kuwapeleka kituo cha Polisi Stakishari kwa mahojiano na baada ya mahojiano watuhumiwa wote 27 walidhaminiwa kwa mujibu wa sheria na watafikishwa mahakamani hivi karibuni kwani upelelezi wa shauri hili umeishakamilika.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatoa onyo kali kwa kikundi chochote cha siasa,dini,au mtu yeyote kuacha kabisa kuchezea maeneo nyeti kama magereza,makambi ya Majeshi yote au maeneo yoyote ambayo ni nyeti kwa taifa.
Hivyo atakayejaribu kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.
WATU 03 WAPOTEZA MAISHA KWA AJARI YA BARABARANI.
Mnamo tarehe 15.03.2020 majira ya 04:30 alfajiri huko barabara ya kawawa mataa ya veta gari namba T 530 DNW aina ya EICHER daladala linalofanya safari za Mbangara- Makumbusho likitokea Mbagala kuelekea Makumbusho liligongana na gari la kubebea nyama lenye namba T 744 DET lililokuwa likitokea Tazara kuelekea katikati ya Jiji na kusababisha vifo vya watu watatu ambao ni wanaume wawili na mwanamke moja na kusababisha majeruhi ya watu nane.
Chanzo cha ajari ni daladala kutaka kuwahi kupita kwenye taa nyekundu.
LAZARO MAMBOSAS– SACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM.
15/03/2020
=====
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA UMMA.
KUKAMATWA KWA WAFUASI WA CHADEMA 27 KWA TUHUMA ZA KUFANYA FUJO KATIKA GEREZA LA MAHABUSU SEGEREA.
Mnamo tarehe 13.03.2020 majira ya saa 07:00 mchana Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam lilipokea taarifa kutoka kwa maofisa wa Gereza la Mahabusu Segerea kuwa kuna kundi la wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) likiongozwa na wabumbe wawili ambao ni Halima James Mdee, Ester Amos Bulaya na Meya wa Ubungo Boniface Jacob limekusanyika katika geti la kuingilia gerezani hapo huku likiandamana na kufanya fujo kutaka kuingia kwa nguvu ndani ya gereza kwa lengo la kwenda kumtoa mwenyekiti wa chama chao Mhe.Freeman Mbowe.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum baada ya kupokea taarifa hizo lilituma askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) na askari wa kituo cha Polisi Stakishari na ambapo walipofika eneo hilo waliwakuta askari magereza wakiwa wanaendelea kuwadhibiti wanachama hao na ndipo Polisi walipowakamata watuhumiwa 27.
Baada ya watuhumiwa hao kukamatwa askari wa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na askari wa Jeshi la magereza waliwachukua na kuwapeleka kituo cha Polisi Stakishari kwa mahojiano na baada ya mahojiano watuhumiwa wote 27 walidhaminiwa kwa mujibu wa sheria na watafikishwa mahakamani hivi karibuni kwani upelelezi wa shauri hili umeishakamilika.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatoa onyo kali kwa kikundi chochote cha siasa,dini,au mtu yeyote kuacha kabisa kuchezea maeneo nyeti kama magereza,makambi ya Majeshi yote au maeneo yoyote ambayo ni nyeti kwa taifa.
Hivyo atakayejaribu kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.
WATU 03 WAPOTEZA MAISHA KWA AJARI YA BARABARANI.
Mnamo tarehe 15.03.2020 majira ya 04:30 alfajiri huko barabara ya kawawa mataa ya veta gari namba T 530 DNW aina ya EICHER daladala linalofanya safari za Mbangara- Makumbusho likitokea Mbagala kuelekea Makumbusho liligongana na gari la kubebea nyama lenye namba T 744 DET lililokuwa likitokea Tazara kuelekea katikati ya Jiji na kusababisha vifo vya watu watatu ambao ni wanaume wawili na mwanamke moja na kusababisha majeruhi ya watu nane.
Chanzo cha ajari ni daladala kutaka kuwahi kupita kwenye taa nyekundu.
LAZARO MAMBOSAS– SACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM.
15/03/2020