Jiwe mzee wa tbc1liveMange atamkubali Magufuli na kumuomba msamaha...muda ni msema kweli
Usemayo ni kweli mkuu, mange akitoa kero flani unaona inatatuliwa, watu wanatoa kero zao bungeni, hazitatuliwi,Kumbe hawa watu hawaendi mbele bila ya Mange.
Kumbe watanzania wanatakiwa wawe wanaipongeza serikali haha hahah haha hahah kumbe ukipongeza unapongezwa ukukosoa unapotezwa Hahaha Hahaha sasa wampe cheo basiKamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa amempongeza Mtanzania anayeishi Marekani, Mange Kimambi kwa maelezo kuwa ameipongeza Serikali.
Mambosasa ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Mei 11,2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari na kumpongeza Mange ambaye alikuwa Kinara wa kushawishi watu kuandamana Aprili 26, 2018 katika maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Kamanda huyo amesema Watanzania wanatakiwa kufikia mahali wachague watu wa kuwashabikia.
"Aprili 26 wananchi wa Kanda yangu walipuuza uhamasishaji wake katika mitandao ya kijamii, sasa Mange huyo huyo anaipongeza Serikali", amesema.
Amesema kwa kuwa ameipongeza Serikali nao wanampongeza kwa kuwa sasa amerudi kundini.
"Nampongeza kwa kuwa amerudi kundini alikuwa anapotosha na Watanzania walipopuuza na yeye ameamua kurudi na kuipongeza Serikali", amesema Mambosasa
Kuhusu watuhumiwa waliokamatwa wakihusishwa na maandamano ya Aprili 26, Mambosasa amesema walioshukiwa kufanya waliojiwa na kupata dhamana.
Chanzo: Mwananchi
Au Big Ghabari bila picha au clip ni sawa na kumfunga ng'ombe kwa ulimbo
Nani Mange au Mambosasa?Hv huyu yupo serious