Una mpenzi wako unayempenda sana na unamtimizia kila kitu na umekaa naye takribani miaka kama mitano hivi . Halafu ilitokea amekwenda shule kusoma na ukamsaidia kwa hali na mali na jinsi ulivyoweza. Cha kushangaza shule kuna mambo mengi inatokea wanasoma na kijana mwingine ambaye wanakuwa karibu sana naye kila ukiulizia na umeanza kuhisi mahusiano kati yao. Mpenzi wako anakwambia kuwa usiwe na wasiwasi siwezi kutembea na mtu kama yule mie. Shule inamalizika ukiwa unamsaidia kwa kila kitu . Inapita muda mawasiliano yanaendelea na inakuja kufikia huyu bwana wanatengana mwingine anahamia mikoani na mwingine anabaki.Huyu bwana nakuja mkutanoni dar na hawajaonana , Huku huyu mpenzi wangu angundua kuwa huyu bwana alikuja na anamwambia umekuja bila kuonana , maana yake nini lakini. Baada ya hapo ujumbe kama huu unatumwa Nimekumiss sana mpenzi wangu kutoka kwa mwanaume akitaja na jina la mpenzi wangu na mwanamke anajibu , wewe tu umeni tupa kabisa, na jamaa anasema nikija nitakutafuta hata usiku , ni wewe tu. Na mara kwa mara anakuwa anampigia simu ukimwuuliza anasema ni mawasiliano tu. Kwa kuwa mtu unampenda , unaamini. Ila hii ya kutembelewa hata usiku ni kali na imeniweka mahali patata. Kumpenda nampenda na nimeweka kweli pendo kwake mbele . Sasa hii inanikatisha tamaa kabisa.
Je nishaurini jamani , huyu dada nampenda na natarajia ndoa na yeye , huyu bwana ana mke na watoto wake . Sasa waungwana nipeni jawabu hapo sielewi.
Je nishaurini jamani , huyu dada nampenda na natarajia ndoa na yeye , huyu bwana ana mke na watoto wake . Sasa waungwana nipeni jawabu hapo sielewi.