Naomba kuzungumza na wenyeji wa jiji la Dar na viunga vyake hususan wafanya biashara. Ni hivi, ujambazi wa kutumia silaha umerejea kwa kasi sawa na maambukizi ya Corona.
Na ujambazi wa safari hii ni wa pekee. Yaani hata Shilingi 200,000/= inakutoa roho.
Tayari huko Segerea meneja wa Baa ameuawa kwa kupigwa risasi akifunga baa usiku akitakiwa kutoe hela za mauzo na alipozingua akatobolewa kwa risasi.
Huko Tabata mfanyabiashara wa bidhaa za jumla amefuatwa nyumbani kwake mara tu alipofika getini akaoneshwa "mguu wa kuku" akitakiwa kutoa hela na silaha. Hakuwa na silaha akatoa hela. Huko Chanika nako kuna tukio la namna hiyo. Hatujui leo wataenda wapi.
Chanzo: Ni kutoka ndani ya jeshi letu la Polisi kwa sharti la hifadhi ya jina.
My Take: Ni vizuri kila mmoja kuchukua tahadhari kushirikiana na Jeshi letu la Polisi. Ni vizuri Polisi wakaweka namba zao wazi ili mtu aonapo dalili za mtu asiyeeleweka kutoa taarifa ili wanaohisiwa kunyakuliwa kabla hawajafanya uharibifu mkubwa.
Polisi nao watoe elimu ya watu kumtambua mtu anayeweza kuwa ni jambazi ili wawahiwe. Hatuwezi kupangiwa muda wa kufanya kazi na kulala na majambazi. Tuwape Polisi ushirikiano.
Hofu yangu ni, isijekuwa ni "beep" ya yule Kamanda aliyeshushwa cheo na kupelekwa Dodoma kusoma magazeti sasa anakomoa. Nawaza kwa sauti.
Na ujambazi wa safari hii ni wa pekee. Yaani hata Shilingi 200,000/= inakutoa roho.
Tayari huko Segerea meneja wa Baa ameuawa kwa kupigwa risasi akifunga baa usiku akitakiwa kutoe hela za mauzo na alipozingua akatobolewa kwa risasi.
Huko Tabata mfanyabiashara wa bidhaa za jumla amefuatwa nyumbani kwake mara tu alipofika getini akaoneshwa "mguu wa kuku" akitakiwa kutoa hela na silaha. Hakuwa na silaha akatoa hela. Huko Chanika nako kuna tukio la namna hiyo. Hatujui leo wataenda wapi.
Chanzo: Ni kutoka ndani ya jeshi letu la Polisi kwa sharti la hifadhi ya jina.
My Take: Ni vizuri kila mmoja kuchukua tahadhari kushirikiana na Jeshi letu la Polisi. Ni vizuri Polisi wakaweka namba zao wazi ili mtu aonapo dalili za mtu asiyeeleweka kutoa taarifa ili wanaohisiwa kunyakuliwa kabla hawajafanya uharibifu mkubwa.
Polisi nao watoe elimu ya watu kumtambua mtu anayeweza kuwa ni jambazi ili wawahiwe. Hatuwezi kupangiwa muda wa kufanya kazi na kulala na majambazi. Tuwape Polisi ushirikiano.
Hofu yangu ni, isijekuwa ni "beep" ya yule Kamanda aliyeshushwa cheo na kupelekwa Dodoma kusoma magazeti sasa anakomoa. Nawaza kwa sauti.