Ni miaka mingi kada ya uwalimu imekuwa ikidharauliwa kwa muda mrefu nchini kwetu. Hii imepelekea mwalimu kudharaulika sana ndani ya jamii japo amekuwa mtu muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu. Mshahara wa mwalimu umekuwa haukizi mahitaji ya mwalimu na hivyo kuwa mtu wa kukata tamaa sana kimaisha. Kutokana na mwalimu kukata tamaa kutokana na mazingiza ya kazi kuwa magumu imepelekea elimu ya Taifa kushuka kila siku huku viongozi wa taifa letu wakipigia chapuo idadi ya madarasa, na kuacha kuzungumzia ubora wa elimu nchini huku wakipeleka watoto wao nje ya nchi na kuwaacha watoto wa wakulima na wafugaji wa nchi wakiikosa haki yao ya kupata elimu bora. Kama waalimu wa nchi hii tunalo jukumu la kuitetea elimu ya taifa letu wenyewe na sio kutegemea chama cha waalimu CWT ambacho kimeonyesha dhahiri kuwa hakina nia ya dhati ya kurejesha heshima ya walimu nchini. Waalimu ili kufanikiwa katika hili tunatakiwa kupambana na maadui watatu wakubwa ambao ni:-1.WOGA 2.CHAMA CHA WALIMU TANZANIA (CWT) 3.SERIKALI. Tutafanikiwa endapo tutashirikiana sote kwa pamoja na kw3a umoja. Cha kufanya tunatakiwa kuwaunganisha waalimu wote nchini tuwe na kauli moja pasipo woga wala hofu.Ninahitaji kupata namba za simu kutoka waalimu pande zote za Tanzania ili tuunganishe nguvu ya pamoja kupigania maslahi na hadhi ya mwalimu nchini.Tukiungana kwa pamoja tunaweza. Nipatie namba yako kwenye inbox yangu ili tuwasiliane na tuunganishe nguvu. KWA PAMOJA BILA WOGA TUNAWEZA.