Kama wenye VVU/AIDS wanasaidiwa na serikali na Albino je?

KIDUNDULIMA

JF-Expert Member
Aug 18, 2010
966
536
Ndugu zangu nimeuliza swali hili kuhusu namna ambavyo ndugu zetu Albino wanavyotendewa katika nchi yetu ya Tanzania. Tunajua wazi kuwa tatizo kubwa walilonalo wenzetu albino ni magonjwa ya ngozi ambayo yanaweza kutatuliwa na kupakaa mafuta maalumu ya ngozi. Na tukijua wazi kuwa wengi wa maalbino kipato chao ni cha chini kabisa hivyo hushindwa kumudu gharama za mafuta hayo. Cha kushangaza serikali imekaa kimya kuhusu tatizo lao wala hakuna agizo la kuhakikisha kuwa albino wanapatiwa mafuta hayo ili kuwaondolea mateso yatokanayo. Kama wenye VVU/AIDs wanasaidiwa na serikali kupunguza makali ya virusi kwanini albino nao wasisaidiwe?Je ni kwa vile hakuna albino ambaye ni waziri katika serikali wa kuweza kuwatetea? Maana mawaziri kibao tunao wenye VVU/AIDs hivyo kwao ni raisi kujipendelea kuliko kuwapendelea albino.

Tafadhari serikali saidieni albino nao ni watanzania.
 
Ndugu zangu nimeuliza swali hili kuhusu namna ambavyo ndugu zetu Albino wanavyotendewa katika nchi yetu ya Tanzania. Tunajua wazi kuwa tatizo kubwa walilonalo wenzetu albino ni magonjwa ya ngozi ambayo yanaweza kutatuliwa na kupakaa mafuta maalumu ya ngozi. Na tukijua wazi kuwa wengi wa maalbino kipato chao ni cha chini kabisa hivyo hushindwa kumudu gharama za mafuta hayo. Cha kushangaza serikali imekaa kimya kuhusu tatizo lao wala hakuna agizo la kuhakikisha kuwa albino wanapatiwa mafuta hayo ili kuwaondolea mateso yatokanayo. Kama wenye VVU/AIDs wanasaidiwa na serikali kupunguza makali ya virusi kwanini albino nao wasisaidiwe?Je ni kwa vile hakuna albino ambaye ni waziri katika serikali wa kuweza kuwatetea? Maana mawaziri kibao tunao wenye VVU/AIDs hivyo kwao ni raisi kujipendelea kuliko kuwapendelea albino.

Tafadhari serikali saidieni albino nao ni watanzania.


Unatakiwa ujiulize kwanza nani ni decision makers Tanzania. Kwanza angalia ni asilimia ngapi ya members wa cabinent ni HIV positive, na angalia ni asilimia ngapi ya members wa cabinet ni albino, angalia ni asilimia ngapi ya ya HIV positive people have access to centres of decion making, na ni asilimia ngapi ya Albino have that access. Jibu liko wazi. Kisiasa tunasema Albino ni wenzetu ni ndugu zetu, kivitendo tunawaonesha kuwa they are useless human beings, ndio maana tulianza kushughulikia mauaji ya Albino pale international media ilivyoanza kusema. pure and simple.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom