Nkobe
JF-Expert Member
- Feb 17, 2013
- 2,162
- 3,162
Kuna wakati huwa nafikiria. Hivi serikali inayotokana na watu masikini inaweza kuhudumia watu wake kwa kiwango cha kutosha?, Prof Mkumbo alisema jamii ya wajinga uchagua viongozi wajinga. Vivyo hivyo naamini jamii ya watu masikini uzalisha serikali masikini maana kodi ya serikali inatokana na watu wake
Hivi ni asilimia ngapi ya Watanzania wana uwezo wa kusomesha watoto wao hata elimu ya chuo kikuu?, au ni asilimia ngapi wana uwezo wa kusomesha watoto wao hadi sekondari?, au ni asilimia ngapi ya Watanzania wana uwezo wa kujigharamia huduma ya Afya? Baada ya serikali kutangaza kuwa elimu ya msingi ni bure tumeshuhudia mafuriko ya watoto madarasani. Hi kwa kuwa wananchi wenyewe hawawezi kusomesha watoto wao, basi tusitegemee serikali itakuwa na uwezo huo.
Sasa najiuliza kama asilimia kubwa ya Watanzania hatuwezi kusomesha watoto wetu, je serikali itaweza? Hivyo sioni ajabu Serikali kushindwa kuwapa wanafunzi mikopo ya elimu ya juu
Hivi ni asilimia ngapi ya Watanzania wana uwezo wa kusomesha watoto wao hata elimu ya chuo kikuu?, au ni asilimia ngapi wana uwezo wa kusomesha watoto wao hadi sekondari?, au ni asilimia ngapi ya Watanzania wana uwezo wa kujigharamia huduma ya Afya? Baada ya serikali kutangaza kuwa elimu ya msingi ni bure tumeshuhudia mafuriko ya watoto madarasani. Hi kwa kuwa wananchi wenyewe hawawezi kusomesha watoto wao, basi tusitegemee serikali itakuwa na uwezo huo.
Sasa najiuliza kama asilimia kubwa ya Watanzania hatuwezi kusomesha watoto wetu, je serikali itaweza? Hivyo sioni ajabu Serikali kushindwa kuwapa wanafunzi mikopo ya elimu ya juu