Bonde la Baraka
JF-Expert Member
- Sep 22, 2016
- 4,580
- 7,938
Kijana mhitimu wa Shahada, stashahada au astashahada hajui Kiswahili fasaha, cha ajabu wengine chuo kikuu wamesoma Shahada ya Elimu na Lugha. Ukipitia kurasa zao Facebook au instagram utaona wameandika hovyohovyo halafu utamsikia anamlaumu Magufuli.
Unataka uwe mwalimu ukawafundishe upumbavu watoto wetu?. Sisi tuliozaliwa kijijini zamani mwalimu wa shule ya msingi alikuwa anatufundisha kuandika au kuongea Kiswahili fasaha sasa kijana mwenye shahada anaandika hovyo tutegemee nini?.
Maneno kama ucku, xmas, xaxa,p, yap yanatokaje kichwani mwa msomi? Kijana wa leo anayetafuta nafasi ofisini huandika Juwa badala ya jua, anaandika ninajuwa badala ya ninajua, huandika kura badala ya kula, huandika ntakuja badala ya nitakuja, barabara huandika balabala, cm badala ya simu, bahalini badala ya baharini.
Msomi hajui kutenganisha kati ya maneno haya; Nipo na niko, hicho na hiko aya na haya. Msomi eti anaandika iko badala ya hiko, uko badala ya huko. Mtu anashindwa kutofautisha neno kwenda na kuondoka.
Analazimisha neno liandikwe kwa kifupi bila kujali miiko ya lugha husika. Kijana mmoja alikuwa katibu wa kikundi hivyo ndiye aliyepaswa kuandika risala, ile risala nilipoipitia nilikutana na makosa mengi mpaka nilishangaa inakuwaje mtu aliyesoma HKL aandike kipumbavu namna ile!
Risala kaandika lisala
Waalikwa kaandika waarikwa na makosa mengine mengi niliyaona.
Vijana wengi hawajui kuandika wasifu(C.V) mzuri na badala yake huhariri C.V walizoziweka watu mtandaoni.
Barua za maombi ya kazi nyingi ni za hovyo , ashukuriwe Mungu maafisa Utumishi wanasoma kichwa tu. Wangesoma neno moja hadi jingine wangekuwa wanacheka sana.
Unataka uwe mwalimu ukawafundishe upumbavu watoto wetu?. Sisi tuliozaliwa kijijini zamani mwalimu wa shule ya msingi alikuwa anatufundisha kuandika au kuongea Kiswahili fasaha sasa kijana mwenye shahada anaandika hovyo tutegemee nini?.
Maneno kama ucku, xmas, xaxa,p, yap yanatokaje kichwani mwa msomi? Kijana wa leo anayetafuta nafasi ofisini huandika Juwa badala ya jua, anaandika ninajuwa badala ya ninajua, huandika kura badala ya kula, huandika ntakuja badala ya nitakuja, barabara huandika balabala, cm badala ya simu, bahalini badala ya baharini.
Msomi hajui kutenganisha kati ya maneno haya; Nipo na niko, hicho na hiko aya na haya. Msomi eti anaandika iko badala ya hiko, uko badala ya huko. Mtu anashindwa kutofautisha neno kwenda na kuondoka.
Analazimisha neno liandikwe kwa kifupi bila kujali miiko ya lugha husika. Kijana mmoja alikuwa katibu wa kikundi hivyo ndiye aliyepaswa kuandika risala, ile risala nilipoipitia nilikutana na makosa mengi mpaka nilishangaa inakuwaje mtu aliyesoma HKL aandike kipumbavu namna ile!
Risala kaandika lisala
Waalikwa kaandika waarikwa na makosa mengine mengi niliyaona.
Vijana wengi hawajui kuandika wasifu(C.V) mzuri na badala yake huhariri C.V walizoziweka watu mtandaoni.
Barua za maombi ya kazi nyingi ni za hovyo , ashukuriwe Mungu maafisa Utumishi wanasoma kichwa tu. Wangesoma neno moja hadi jingine wangekuwa wanacheka sana.