Kama Warusi wanamhitaji Rais Putin kuongezewa muda, Tanzania tubadili Katiba ili Rais Magufuli aongozewe muda baada ya 2025

Alex Fredrick

JF-Expert Member
Jun 21, 2016
680
1,338
Majuzi tumeona vyombo vya habari ulimwenguni vimeripoti kuwa karibu 80 % ya Wananchi wa Urusi wanaunga mkono Rais Putin aongozewe muda zaidi wa kuongoza Taifa hilo.

Na sababu ya msingi ni moja tu kuwa Rais Putin ameipaisha sana Urusi kwenye medani karibu zote hasa zaidi Uchumi na imekuwa tisho kwa Nchi za Ulaya na Marekani.

Naamini sisi Watanzania mwaka 2025 baada ya Mh. Rais Magufuli kumaliza ngwe yake ya pili tuna kila sababu ya kumuongezea muda ili aendelee kutuongoza.

SGR, Stiglers pale Rufiji. Vituo vya afya karibu kila kijiji, Madawa kutoka Bajeti ya billion 34 mpka sasa billion 269, Elimu bure kutoka msingi mpka secondary, ununuzi wa ndege na kufufua Shirika la ATCL, Kubadilisha Sheria zote za madini na matokeo yake tayari tumeanza kuyaona mfano ACCACIA.

Huduma za Bima ya afya na sasa hivi Wizara ya Afya inaandaa muswada ili kila Mtanzania aweze kuwa na Bima ya afya. Nidhamu imerudi Serikali na Taasisi zote za mashirika ya umma sanjali na kuondoa wafanyakazi hewa ambao walikuwa wanaliingizia Taifa hasara kubwa.

Kwa haya na mengine yote kama Taifa tuna kila sababu ya kuendelea kumpa Mh Rais Magufuli ridhaa ya kutuongoza baada ya kumaliza kipindi chake 2025. Tuache dhana mfu kwamba Kiongozi akimaliza vipindi viwili hawezi kuendelea kwasababu ya Katiba wakati Katiba sio "MSAHAFU"

Tuomeona miongo ya hivi karibuni kwamba Viongozi wakimaliza vipindi vyao huku Taifa likiwa hoi kwenye medani za Uchumi na Ufisadi ukitamalaki kila eneo.

Tumuache Rais Magufuli andelea kuliongoza Taifa hili maana tumechezewa vya kutosha na tumebezwa vya kutosha na hata majirani zetu kwa miongo kadhaa kwamba tuna rasilimali za kila namna lakini hakuna maendeleo.

##JPM KIOO TUELEKEACHO

Alex Fredrick
 
Ndugu yangu mtoa mada usiifananishe Tanzania na Urusi sisi ni dunia ya mwisho na Urusi ni dunia ya kwanza! Magu needs to go after his last five years term!! Faida ni nyingi zaidi ya hasara, sababu mpaka anatoka wengine tutakuwa hatuna hata nguvu ya kutembea!! Magu ametubana mno uchumi wa mamilioni ya familia umeanguka. Usisahau pia nchi hii ina amani kwa kuwa Marais hupishana hapa sio Burundi ya Nkurunzinza, pia usisahau kukumbuka kuondokana na udini na ubinafsi sababu Magu ni lazima atoke aingie Rais mwislam ili kubalansi mambo, kulinda amani utulivu na mshikamano wa kitaifa!

Ona hapa chini nilivyojibu hoja ya Kafulila kuwa raia tufurahie nchi kuingia uchumi wa kati!

Sawa tunakubali kupitia makaratasi ya wazungu nchi yetu iko uchumi wa kati na hiyo ni one angle (economic growth model) ya kuangalia maendeleo ya uchumi ila hao hao wazungu wake Kafulila waje sasa wafanye utafiti wa angle ya pili inaitwa human development index inayoangalia maisha halisi ya watu , aina ya nyumba wanazoishi watu, idadi ya watu walalao katika chumba kimoja , virago wanavyolalia , upatikanaji na ujazo wa maji safi na salama ya kunywa, nguo wavaazo watu, kiwango cha furaha walichonacho raia, aina na kiwango cha chakula kwa kila raia , kiwango cha elimu cha raia walio wengi, uhuru wa habari, uhuru na haki za raia, utawala wa sheria nk!

Huyu Kafulila hana njaa asikurupuke alete wazungu waje sasa kutafiti na kuona familia ngapi kwasasa bongo zinamudu japo mlo mmoja kwa siku na kuvaa viatu badala ya yeboyebo?! familia ngapi zinamudu kulipia japo vipimo tu mmojawapo anapoumwa? ni familia ngapi zinamudu kununua uniforms za shule za watoto? ni familia ngapi zinamudu kulipa nauli na kusafiri kutembelea ndugu , kuhudhuria harusi na kuhudhuria mazishi? ni familia ngapi bongo kwasasa zinaweza kuweka akiba ya pesa benki ? ni chache tu mojawapo ni familia yake yeye!!

Jibu kuu ni kuwa uchumi huu wa kati utaonekana kwa zile familia za wafanyakazi wa formal sector tu ambao ni less than 10%, ikimaanisha mamilioni ya raia tuliobakia wote tuko hoi tumegeuka maskini hohehahe sababu sote tuko na self employments kwenye informal sector isiyo na mzunguko wa pesa uliokatwa na sera za sasa za matumizi ya pesa za umma!!

Kwa sasa zaidi ya watu millioni 50 bongo wameangukia kuwa familia maskini sababu hawana tena reliable income na hawako kwenye formal sector ambayo ni only 8% according to the website ya ofisi ya takwimu, zaidi ya 90% ya raia katika utawala huu wa Magu wako pembezoni kwenye small scale kilimo uvuvi na biashara na wanategemea kuishi kwa mzunguko wa pesa ambao umekata kabisa kwasasa sababu serikali inachukua kodi kubwa na kulipa wageni wanaojenga miundombinu kama waarabu na wachina na ambao hupeleka kwao hizo pesa!! Mzunguko wa pesa pia umekata sababu pesa zingine nyingi zikinunua moja kwa moja vitu mf pesa yote iliyolipia ndege zetu ilitoka kwenye mzunguko huu huu na imeacha maumivu ya kutisha kwenye uchumi wa walalahoi!!shimo ililoacha halijazibwa!!

Kwa upande mwingine pia kutokana na lawama za wafadhili kwa kudorora hali ya usalama kwa wapigania demokrasia nchini basi ukichanganya na athari za COVID19 ufadhili umekata sana kwa serikali na kukata kabisa kwa NGO hivyo kupunguza mno pesa zilizokuwepo katika mzunguko hasa wakati wa Mkwere wazungu walimwaga pesa nyingi mno ya ufadhili ambayo waliifurahia pia kuona iliishia kwenye matumbo ya watu na si kuendeleza nchi!! kukata kwa misaada
ya wafadhili kumeleta hali ngumu mno kwasasa bongo pesa hakuna, njaa ni kali mno kwasasa kwa mamilioni ya watu!! watu wana hasira si kitoto!!

Ingekuwa nchi hii haina magari ya washawasha , matumizi ya mabomu ya machozi, na matumizi ya nguvu na FFU wanaopiga watu kwa sifa, ingekuwa nchi hii ina utawala wa sheria na kuruhusu freedom of opinion, expression and assembly, ingekuwa nchi hii iko katika bara jingine na sio Afrika bara la giza , ingekuwa nchi hii ina mamilioni ya watu walio na civic education ya kutosha , ingekuwa nchi hii ina watu walioshiba vizuri chakula na kuweza kutulia na kuwaza mambo yao na si wale wanaohangaika kila kukicha eti kutafuta japo mlo mmoja tu kwa siku , ingekuwa nchi hii haina raia waoga, ingekuwa nchi hii ina kina ZZK mia tu basi muda huu kwa jinsi watu wanavyoteseka kusingekalika kwa maandamano yasiyoisha ya kupinga hali ngumu na kuitaka serikali iondoke madarakani!!sie tulie huku Geita mitaani tunaona watu wengi wanashindia uji na karanga!!

Kafulila ana mahali pa kupata mlo unaotokana na kodi za wanyonge ni vigumu kwake kujua ni kwa kiwango gani mamilioni ya raia wanateseka kwa njaa na magonjwa na kukosa hata nguo za kutokea, Kafulila anapaswa kujua mtaani hakuna sherehe na uchumi wa kati hauna maana yoyote kwasasa kwa mamilioni ya watanzania wanaoshindia mlo mmoja tena si balanced! Kafulila ajue sasa we have a fake economy in Magu era, pole mno zaidi kwa wabongo maskini waishio mijini tuliozoea cash sababu serikali inatoa pesa kwenye mzunguko kupitia kodi kisha inapeleka kwa makandarasi wanaozitoa nje pesa hizo. katika miaka mitano ijayo ya Magu kila kitambi kitakwisha na kila goti litapigwa!!

Kwa mujibu wa Nape nilimsikia mwenyewe akiongea bungeni huku swahiba yake Mr Februari yuko pembeni akichekelea ni kuwa Mkulu hatimizi ilani ya sisiem waliyoitengeneza wao na waliyomtuma ilani ya sisiem ya sasa inayotaka maisha ya raia kuboreshwa , watu wawe na afya, chakula, nguo na furaha! leo hii kila mtu asie na kazi ya mshahara bila aibu amejaa utapeli ili kujinusuru yeye na familia yake na ukosefu wa chakula kutokana na hali ngumu!!hivi sasa kila mtu hasa wasanii wanalitaka bunge kwa njia yoyote ili kujinusuru na ukata kwakuwa pesa zimebaki kwenye siasa tu manake biashara hazitoki tena pesa hakuna mtaani!!

Kwa sasa serikali imeweka ilani kapuni haijali tena maisha ya watu walioiweka madarakani inaangalia kujenga miundombinu tu, ila ukweli familia nyingi bongo zimeingia kwenye umaskini wa kutisha baada ya kufeli biashara zao kutokana na kulipa kodi kubwa na wateja hamna sababu serikali inaondoa pesa kwenye mzunguko kulipa foreign contractors and brokers!

Kutokana na ukali wa askari wa bongo na uoga wa asili na dharau za watanzania watakubali kuteseka kwa miaka mingine mitano ya Mkulu na amani itadumu raia wakimsubiri Mkulu amalize miaka yake mitano ya mwisho wamtukane na kumzomea popote atakapoenda iwapo miradi ya kimkakati haitakamilika!!

Mimi ni shabiki kindakindaki wa Mkulu na namshauri ili uchumi huo wa kati utufikie mitaani basi katika ngwe ya pili ya lala salama Magu needs to be mkali times two, apunguze wapinzani bungeni times two, aondoe mikutano ya siasa times two, awabane kina DJ Makengeza na ZZK times two (wawe na kesi za uchochezi times two), apunguze na kulibana baraza la mawaziri times two, atumbue wazembe times two sababu kawatisha raia kuigopa serikali, kawabana raia kwenye maisha sasa ni muhimu kusimamia kibabe miradi mikubwa ya kimkakati adeal na mawaziri perpendicular ahakikishe miradi yote mikubwa imekamilika kabla ya wakati basi raia wema wa bongo watasahau shida za miaka yote na Mkulu atachukua CREDITS zote na kila atakapopita raia watamwimbia nyimbo na mapambio!! Mkulu atakuwa shujaa and the best President of Tanzania of all times na lazima tumuandike kwenye vitabu vya shule kama mfano wa uongozi bora kwa nchi masikini.
 
Mnatuchosha na hizi mada zenu. Kiufupi tu huyu wa kwenu hana hizo sifa unazotaka kutuaminisha.
 
Hakuna tatizo, hata Tanzania tunaeza kufanya hivo, lakini swali ni kwamba kura hizo zitapigwa kwa uwazi na haki? Kukiwa na tume huru ya uchaguzi haki itatendeka.
 
Majuzi tumeona vyombo vya habari ulimwenguni vimeripoti kuwa karibu 80 % ya Wananchi wa Urusi wanaunga mkono Rais Putin aongozewe muda zaidi wa kuongoza Taifa hilo.

Na sababu ya msingi ni moja tu kuwa Rais Putin ameipaisha sana Urusi kwenye medani karibu zote hasa zaidi Uchumi na imekuwa tisho kwa Nchi za Ulaya na Marekani.

Naamini sisi Watanzania mwaka 2025 baada ya Mh. JPM kumaliza ngwe yake ya pili tuna kila sababu ya kumuongezea muda ili aendelee kutuongoza.

SGR, Stiglers pale Rufiji. Vituo vya afya karibu kila kijiji, Madawa kutoka Bajeti ya billion 34 mpka sasa billion 269, Elimu bure kutoka msingi mpka secondary, ununuzi wa ndege na kufufua Shirika la ATCL, Kubadilisha Sheria zote za madini na matokeo yake tayari tumeanza kuyaona mfano ACCACIA.

Huduma za Bima ya afya na sasa hivi Wizara ya Afya inaandaa muswada ili kila Mtanzania aweze kuwa na Bima ya afya. Nidhamu imerudi Serikali na Taasisi zote za mashirika ya umma sanjali na kuondoa wafanyakazi hewa ambao walikuwa wanaliingizia Taifa hasara kubwa.

Kwa haya na mengine yote kama Taifa tuna kila sababu ya kuendelea kumpa Mh Rais Magufuli ridhaa ya kutuongoza baada ya kumaliza kipindi chake 2025. Tuache dhana mfu kwamba Kiongozi akimaliza vipindi viwili hawezi kuendelea kwasababu ya Katiba wakati Katiba sio "MSAHAFU"

Tuomeona miongo ya hivi karibuni kwamba Viongozi wakimaliza vipindi vyao huku Taifa likiwa hoi kwenye medani za Uchumi na Ufisadi ukitamalaki kila eneo.

Tumuache JPM andelea kuliongoza Taifa hili maana tumechezewa vya kutosha na tumebezwa vya kutosha na hata majirani zetu kwa miongo kadhaa kwamba tuna rasilimali za kila namna lakini hakuna maendeleo.

##JPM KIOO TUELEKEACHO

Alex Fredrick
Ila jamani, wengine mna mawazo mabaya sana !!!. Kwa lipi hasa ?!.

Fanya mema uende zako usingoje shukrani.
 
100% naunga mkono hoja, tena hakuna haja hata ya kubadili katiba ni kupoteza muda na pesa tu. Rais akitamka ni sheria na katiba yenyewe hiyo. Mbona kuzuia mikutano ya siasa alitamka tu ikawa!

Hata kufanya uchaguzi ni matumizi mabaya ya pesa. Hivi kwanini asitamke tu kuanzia August 2020 yeye ndiye rais wa maisha?

Tunampenda rais wetu mtukufu . Hapa Kazi tu!
 
TANZANIA HATUJAFIKIA HATUA HIYO,

Tanzania utamaduni wetu ni miaka 10 so hakutakua na haja yeyote ya kuongeza Muda kwa Mhe. Rais, yeye atafanya kwa wakati wake atatupisha na kuingia mwingine kwani wenye vipaji zaidi ya Mhe. Rais wapo wengi sana ndani na nje ya CCM.
Tunamhitaji Magufuli mwisho 2025 kisha aache kwa Mtanzania mwingine ili naye atuonyeshe makeke yake.
 
Majuzi tumeona vyombo vya habari ulimwenguni vimeripoti kuwa karibu 80 % ya Wananchi wa Urusi wanaunga mkono Rais Putin aongozewe muda zaidi wa kuongoza Taifa hilo.

Na sababu ya msingi ni moja tu kuwa Rais Putin ameipaisha sana Urusi kwenye medani karibu zote hasa zaidi Uchumi na imekuwa tisho kwa Nchi za Ulaya na Marekani.

Naamini sisi Watanzania mwaka 2025 baada ya Mh. Rais Magufuli kumaliza ngwe yake ya pili tuna kila sababu ya kumuongezea muda ili aendelee kutuongoza.

SGR, Stiglers pale Rufiji. Vituo vya afya karibu kila kijiji, Madawa kutoka Bajeti ya billion 34 mpka sasa billion 269, Elimu bure kutoka msingi mpka secondary, ununuzi wa ndege na kufufua Shirika la ATCL, Kubadilisha Sheria zote za madini na matokeo yake tayari tumeanza kuyaona mfano ACCACIA.

Huduma za Bima ya afya na sasa hivi Wizara ya Afya inaandaa muswada ili kila Mtanzania aweze kuwa na Bima ya afya. Nidhamu imerudi Serikali na Taasisi zote za mashirika ya umma sanjali na kuondoa wafanyakazi hewa ambao walikuwa wanaliingizia Taifa hasara kubwa.

Kwa haya na mengine yote kama Taifa tuna kila sababu ya kuendelea kumpa Mh Rais Magufuli ridhaa ya kutuongoza baada ya kumaliza kipindi chake 2025. Tuache dhana mfu kwamba Kiongozi akimaliza vipindi viwili hawezi kuendelea kwasababu ya Katiba wakati Katiba sio "MSAHAFU"

Tuomeona miongo ya hivi karibuni kwamba Viongozi wakimaliza vipindi vyao huku Taifa likiwa hoi kwenye medani za Uchumi na Ufisadi ukitamalaki kila eneo.

Tumuache Rais Magufuli andelea kuliongoza Taifa hili maana tumechezewa vya kutosha na tumebezwa vya kutosha na hata majirani zetu kwa miongo kadhaa kwamba tuna rasilimali za kila namna lakini hakuna maendeleo.

##JPM KIOO TUELEKEACHO

Alex Fredrick
Najua una wasiwasi wa kupoteza kawilaya kako baada ya jpm kustaafu,, amini nakwamnia jpm atakutumbua wewe mara tu atakapofanikiwa kushinda uchaguzi wa 2020.
 
Awe hata wa maisha, lakini kuishi kuna mwisho Tanzania itabaki
 
Ifiƙe mahali tuongelee mamɓo ƴa msingi tumechoshwa na nƴimɓo hii dailƴ😠😡 nasema hivi miaƙa mi5 haitoshi ƙumpima mtu wa ƙutuongoza milele mwamɓieni aƙaze na ahaƙiƙishe hiƴo miraɗi inaleta maenɗeleo enɗelevu ƙwa wananchi sio ƙila siƙu tƴamɓiwe FAIƊA TUTAZIONA MƁELENI iƙiwa watu wanaziɗi ƙuwa masiƙini wa ƙupinɗuƙia sio ƙwa masiƙini sio ƙwa tajiri wote ƙilio ƙimoja mpaƙa lini😕😕😕
 
Majuzi tumeona vyombo vya habari ulimwenguni vimeripoti kuwa karibu 80 % ya Wananchi wa Urusi wanaunga mkono Rais Putin aongozewe muda zaidi wa kuongoza Taifa hilo.

Na sababu ya msingi ni moja tu kuwa Rais Putin ameipaisha sana Urusi kwenye medani karibu zote hasa zaidi Uchumi na imekuwa tisho kwa Nchi za Ulaya na Marekani.

Naamini sisi Watanzania mwaka 2025 baada ya Mh. Rais Magufuli kumaliza ngwe yake ya pili tuna kila sababu ya kumuongezea muda ili aendelee kutuongoza.

SGR, Stiglers pale Rufiji. Vituo vya afya karibu kila kijiji, Madawa kutoka Bajeti ya billion 34 mpka sasa billion 269, Elimu bure kutoka msingi mpka secondary, ununuzi wa ndege na kufufua Shirika la ATCL, Kubadilisha Sheria zote za madini na matokeo yake tayari tumeanza kuyaona mfano ACCACIA.

Huduma za Bima ya afya na sasa hivi Wizara ya Afya inaandaa muswada ili kila Mtanzania aweze kuwa na Bima ya afya. Nidhamu imerudi Serikali na Taasisi zote za mashirika ya umma sanjali na kuondoa wafanyakazi hewa ambao walikuwa wanaliingizia Taifa hasara kubwa.

Kwa haya na mengine yote kama Taifa tuna kila sababu ya kuendelea kumpa Mh Rais Magufuli ridhaa ya kutuongoza baada ya kumaliza kipindi chake 2025. Tuache dhana mfu kwamba Kiongozi akimaliza vipindi viwili hawezi kuendelea kwasababu ya Katiba wakati Katiba sio "MSAHAFU"

Tuomeona miongo ya hivi karibuni kwamba Viongozi wakimaliza vipindi vyao huku Taifa likiwa hoi kwenye medani za Uchumi na Ufisadi ukitamalaki kila eneo.

Tumuache Rais Magufuli andelea kuliongoza Taifa hili maana tumechezewa vya kutosha na tumebezwa vya kutosha na hata majirani zetu kwa miongo kadhaa kwamba tuna rasilimali za kila namna lakini hakuna maendeleo.

##JPM KIOO TUELEKEACHO

Alex Fredrick
Hofu yako wewe na wenye mawazo kama wewe ni njaa utakayoipata pindi Magufuli atakapomaliza muda wake. Hayo sijui SGR, Stiggler ni geresha tu
 
Majuzi tumeona vyombo vya habari ulimwenguni vimeripoti kuwa karibu 80 % ya Wananchi wa Urusi wanaunga mkono Rais Putin aongozewe muda zaidi wa kuongoza Taifa hilo.

Na sababu ya msingi ni moja tu kuwa Rais Putin ameipaisha sana Urusi kwenye medani karibu zote hasa zaidi Uchumi na imekuwa tisho kwa Nchi za Ulaya na Marekani.

Naamini sisi Watanzania mwaka 2025 baada ya Mh. Rais Magufuli kumaliza ngwe yake ya pili tuna kila sababu ya kumuongezea muda ili aendelee kutuongoza.

SGR, Stiglers pale Rufiji. Vituo vya afya karibu kila kijiji, Madawa kutoka Bajeti ya billion 34 mpka sasa billion 269, Elimu bure kutoka msingi mpka secondary, ununuzi wa ndege na kufufua Shirika la ATCL, Kubadilisha Sheria zote za madini na matokeo yake tayari tumeanza kuyaona mfano ACCACIA.

Huduma za Bima ya afya na sasa hivi Wizara ya Afya inaandaa muswada ili kila Mtanzania aweze kuwa na Bima ya afya. Nidhamu imerudi Serikali na Taasisi zote za mashirika ya umma sanjali na kuondoa wafanyakazi hewa ambao walikuwa wanaliingizia Taifa hasara kubwa.

Kwa haya na mengine yote kama Taifa tuna kila sababu ya kuendelea kumpa Mh Rais Magufuli ridhaa ya kutuongoza baada ya kumaliza kipindi chake 2025. Tuache dhana mfu kwamba Kiongozi akimaliza vipindi viwili hawezi kuendelea kwasababu ya Katiba wakati Katiba sio "MSAHAFU"

Tuomeona miongo ya hivi karibuni kwamba Viongozi wakimaliza vipindi vyao huku Taifa likiwa hoi kwenye medani za Uchumi na Ufisadi ukitamalaki kila eneo.

Tumuache Rais Magufuli andelea kuliongoza Taifa hili maana tumechezewa vya kutosha na tumebezwa vya kutosha na hata majirani zetu kwa miongo kadhaa kwamba tuna rasilimali za kila namna lakini hakuna maendeleo.

##JPM KIOO TUELEKEACHO

Alex Fredrick
Stupid fella.
 
Tutaandamana nchi nzima kama Rais hotoongezewa muda mpaka 2030.patachimbika.
Viva Maguli.
 
Tutaandamana nchi nzima kama Rais hotoongezewa muda mpaka 2030.patachimbika.
Viva Maguli.
Mkuu mtu anapokosea fikra hukosea pia katika maandishi, ona umeandika ‘Viva Maguli’ badala ya ‘Viva Magufuli’

naona umetangaza vita mapema na waislamu!! muda utakapofika yakiibuka mapigano usiwatangulize mbele wengine!!
 
Katika nchi za wazungu wenye akili za Kiafrika(Watanzania) mojawapo ni Warusi. Na jamaa ana wapeleka kama atakavyo. Zamani nilikuwa najua kuwa hakuna wazungu wajinga.
Majuzi tumeona vyombo vya habari ulimwenguni vimeripoti kuwa karibu 80 % ya Wananchi wa Urusi wanaunga mkono Rais Putin aongozewe muda zaidi wa kuongoza Taifa hilo.

Na sababu ya msingi ni moja tu kuwa Rais Putin ameipaisha sana Urusi kwenye medani karibu zote hasa zaidi Uchumi na imekuwa tisho kwa Nchi za Ulaya na Marekani.

Naamini sisi Watanzania mwaka 2025 baada ya Mh. Rais Magufuli kumaliza ngwe yake ya pili tuna kila sababu ya kumuongezea muda ili aendelee kutuongoza.

SGR, Stiglers pale Rufiji. Vituo vya afya karibu kila kijiji, Madawa kutoka Bajeti ya billion 34 mpka sasa billion 269, Elimu bure kutoka msingi mpka secondary, ununuzi wa ndege na kufufua Shirika la ATCL, Kubadilisha Sheria zote za madini na matokeo yake tayari tumeanza kuyaona mfano ACCACIA.

Huduma za Bima ya afya na sasa hivi Wizara ya Afya inaandaa muswada ili kila Mtanzania aweze kuwa na Bima ya afya. Nidhamu imerudi Serikali na Taasisi zote za mashirika ya umma sanjali na kuondoa wafanyakazi hewa ambao walikuwa wanaliingizia Taifa hasara kubwa.

Kwa haya na mengine yote kama Taifa tuna kila sababu ya kuendelea kumpa Mh Rais Magufuli ridhaa ya kutuongoza baada ya kumaliza kipindi chake 2025. Tuache dhana mfu kwamba Kiongozi akimaliza vipindi viwili hawezi kuendelea kwasababu ya Katiba wakati Katiba sio "MSAHAFU"

Tuomeona miongo ya hivi karibuni kwamba Viongozi wakimaliza vipindi vyao huku Taifa likiwa hoi kwenye medani za Uchumi na Ufisadi ukitamalaki kila eneo.

Tumuache Rais Magufuli andelea kuliongoza Taifa hili maana tumechezewa vya kutosha na tumebezwa vya kutosha na hata majirani zetu kwa miongo kadhaa kwamba tuna rasilimali za kila namna lakini hakuna maendeleo.

##JPM KIOO TUELEKEACHO

Alex Fredrick
Umesema kweli aiseee!
Waafrika wanapenda sana matatizo ndio maana matatizo ya kila aina hukaa Afrika. Kubadilisha katiba ili mtu akae zaidi madarakani ni ujinga mkubwa tena mtu ambaye ni dikteta!
 
Back
Top Bottom