Kama Wanasiasa wa Upinzani nchini Tanzania wataendelea na ' Strategies ' zao za ' Kitoto ' hivi nitaanza kuwapuuza!

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,385
108,450
Mmekuwa ni Marafiki zangu wakubwa na wazuri tu japo Mimi ni Shabiki mkubwa na mzuri wa Chama Tawala Chama Cha Mapinduzi ( CCM ) na sijawahi kufikiria na sidhani kama hata huko mbele itakuja kutokea Mimi GENTAMYCINE nikawa ama Mpinzani au Mwanaharakati japo ninapenda mno na sana uwepo wa Siasa za Kidemokrasia na Upinzani hapa Tanzania.

Kuna tatizo moja nimeanza kuliona linaanza kuota ' mizizi ' hapa Tanzania na kuna muda nilidhani labda ulikuwa ni upepo tu wa muda lakini baadae hili tatizo litatoweka lakini naona sasa hilo tatizo ndiyo limegeuzwa kama mkakati ( strategy ) na ' turufu ' ya Kisiasa ya Wapinzani dhidi ya ' Hasimu ' Wao Mkuu Chama Tawala cha Mapinduzi.

Ni kujidanganya tu na kupotoka kwa Chama cha Siasa au Mwanasiasa wa Tanzania kudhani kwamba ataitoa CCM ' Madarakani ' kwa kila Siku tu Kuvizia ' mabaya ' yake au ' makosa ' yake pekee ndipo yatumike kama njia Kuu ya Kuishtaki kwa Wananchi wa Tanzania.

Nilisema huko nyuma na leo narudia tena kuwa Wapinzani nchini Tanzania mtaeleweka na Wananchi kama tu mtajijenga katika misingi ya Siasa za Kuheshimiana, Siasa za Kujenga Umoja, Siasa za Ushirikiano na Siasa za Mama Tanzania Kwanza huku mkiweka maslahi yenu kwa Tanzania na kuondokana na dhana Kubwa mliyo nayo sasa ya kuwa ' Wachonganishi ' na Watu mnaopenda / mnaotaka kupata ' Public Sympathy ' pekee.

Kuna nchi kadhaa za Afrika naona mnaweza pia mkajifunza katika hili kama vile Zambia, Afrika Kusini na Ghana na kwa huko ng'ambo ( Ulaya ) hadi Marekani pia mna mengi sana ya Kujifunza. Najitahidi sana kufuatilia Siasa za nchi kadhaa hapa Barani Kwetu Afrika na huko Ulaya pamoja na Marekani ila naona kama Siasa ambazo zinafanywa na Wapinzani wa Tanzania ni za ' Kipekee ' kabisa ambazo hazina tija wala mantiki sana sana naona ni za Kujitafutia / Kujizidishia tu matatizo kama mengine ambayo tumeanza sasa kuyaona na yanayowagharimu.

Bado naamini kwamba bila Upinzani Imara chama Changu ' pendwa ' cha CCM hakiwezi kuwa imara na mahiri hivyo nitumie tu fursa hii kuwaomba Wapinzani nchini Tanzania hebu tulieni, jipangeni upya kwani bado hamjachelewa, tengenezeni ' mkakati ' mzuri tu na wa Kistaarabu wa kuweza ' Kupambana ' au ' Kushindana ' Kisera na Chama cha Mapinduzi ili basi muweze kujijengea imani kwa Wananchi na ikiwezekana Siku moja nanyi mje kupewa ' Mamlaka ' na muitawale hii nchi na mtupeleke huko ambako mnataka kutupeleka katika mafanikio.

Nawapenda sana na mno na ndiyo maana sijawa ' Mnafiki ' Kwenu na nimeona leo niwaambieni tu huu ukweli hapa hapa.

Nawasilisha.
 
Sio kweli,wapinzani wanaaenda zaidi ya hapo na ukumbuke hivi sasa hata tu kufanya mikutano ya siasa wanadhibitiwa.

Kumbuka pia CHADEMA wamendaa sera mbadala, sera ambazo walipaswa kuzinadi kupitia mikutano ya hadhara,mikutano ambayo kwa sasa hairuhusiwi kwa kutumia dola.

Vile vile duniani kote sissa ni kama mchezo wa soka;ukifanya kosa, mwenzako analitumia kukupiga bao, hivyo kamwe wapinzani hawawezi kukaa kimya pale serikali inapofanya makosa na wakifanya hivyo,basi hata uwepo wao kama wapinzani utakuwa hauna maana.

Isitoshe, ni bora wapinzani wanaoibua hoja za kuisulubu CCM kuliko CCM hii ya sasa iliyojikita katika kununua mamluki wa kisiasa kutoka upinzani eti wakitegemea hio ndio njia sahihi ya kuua upinzani!

Kingine,unapoona CCM wanakuja na muswaada kandamizi wenye lengo la kutaka kuua upinzani,ujue teyari wanakiri hawawezi kushinda kwa hoja na wapinzani na kwamba 2020 hawana sera za kuwafanya wauzike kwa umma zaidi ya kuja na habari za kununua ndege, SGR, Stieglers Gorge na vitu vya aina hiyo mambo ambayo hayamgusu mwananchi moja kwa moja kama kiliomo, ajira, maji, masilahi bora ya watumishi, kodi rafiki kwa wafanyabiashara,n.k.
 
Polisi walipiga Risasi Akwilina leo mbowe yuko ndani heshima iko wapi, Kwanza kusema wewe ni CCM mada yako imekosa mashiko, unatetea chama chako, kwahiyo mnataka Wapinzani waungane kimawazo na CCM? upinzani utakuwa na maana gani,

CCM wengi hamjui maana ya upinzani, mpinzani wako mfano ukiweka mambo 100, ukafanya yote 100 na ukakosea 1, 99 yakawa vizuri, atakukosoa kwa hilohilo moja, jueni maana ya Upinzani hamta pata shida. kuteka watu, kupiga Risasi kote huko ni kutokujua upinzani maana yake nini, ikiwepo na mtoa mada.
 
Sio kweli maana wapinzani wanaaenda zaidi ya hapo na ukumbuke hivi sasa hata tu kufanya mikutano ya siasa wanadhibitiwa.

Kumbuka pia CHADEMA wameabdaa sera mbadala ambazo walipaswa kuzinadi kupitia mikutano ya hadhara,mikutano ambayo kwa sasa hairuhusiwi kwa kutumia dola.

Uko sahihi na nakubaliana nawe kwa 75% juu ya Hoja yako uliyoiwasilisha hapa ila nilidhani sasa baada ya nyie Wapinzani kuona mmebanwa hivi basi mngejipanda upya na mje Kivingine kuliko kila mara ' Kudandia dandia ' tu matukio ya Kisiasa na Kiutawala yanayofanywa na Chama Tawala ( CCM ) pamoja na Serikali yake kisha mnayatumia kama ' mitaji ' yenu mbele ya ' Wafuasi ' wenu kitu ambacho binafsi sioni kama kina Tija kivile na kitakuja kuwasaidieni kutaka kufika huko mnakokutaka.
 
Mbinu za kupambana na adui ziko nyingi..
Kumkalisha adui kama CCM hakutakiwi fair play lazima ucheze faulo nyingi hata ikiwezekana kuwashika kende ili wakae ni sawa tu.. Huwezi kuishinda CCM kwa kutumia Mbinu ushawishi na mbinu za hoja kali maana watanzania ambao ndio wapiga kura walio wengi bado vichwa haviko tayari..

Kama Naibu spika anacheza Nyegezi na linapita tu kimya kimya bila reaction ya wananchi unategemea unaweza kushawishi umati huu kwa hoja za kisomi?? Lazima ushambulie kwa kuvizia..
 
Polisi walipiga Risasi Akwilina leo mbowe yuko ndani heshima iko wapi, Kwanza kusema wewe ni CCM mada yako imekosa mashiko, unatetea chama chako, kwahiyo mnataka Wapinzani waungane kimawazo na CCM? upinzani utakuwa na maana gani,

CCM wengi hamjui maana ya upinzani, mpinzani wako mfano ukiweka mambo 100, ukafanya yote 100 na ukakosea 1, 99 yakawa vizuri, atakukosoa kwa hilohilo moja, jueni maana ya Upinzani hamta pata shida. kuteka watu, kupiga Risasi kote huko ni kutokujua upinzani maana yake nini, ikiwepo na mtoa mada.

Naomba tuijadili hii ' Mada ' Kisomi tafadhali na siyo Kutanguliza au Kutawaliwa na Hasira zetu za Vyama. Na sioni kama ni dhambi / kosa kwa Mimi GENTAMYCINE Kujinasibu / Kujitanabaisha kuwa ni Shabiki na Mpenzi mkubwa tena wa ' Kutukuka ' kabisa wa Chama Tawala cha Mapinduzi ( CCM )

Ninachojaribu kuwashaurini hapa ni kwamba badilikeni halafu sijawalazimisha bali nawashaurini tu kama Marafiki zangu wakubwa wa Kidemokrasia.
 
uki wapuuza wewe ita tusaidia namna gani bwana?

Wapinzani wa kweli na wanaojitambua kamwe wasingejibu hivi kwa ' Mhemko ' wa Kihasira / Kijazba. Hata hivyo siyo Kosa lako na nimekusamehe bure!
 
Ruhusuni mikutano ya siasa !
Mtu kwenda zindua kisima cha maji tu anakamatwa hapo kuna haki kweli!
Awamu hii siasa ya majukwani na kuzunguka nchi nzima wanafanya chichiem tu!

Ova
 
Naomba tuijadili hii ' Mada ' Kisomi tafadhali na siyo Kutanguliza au Kutawaliwa na Hasira zetu za Vyama. Na sioni kama ni dhambi / kosa kwa Mimi GENTAMYCINE Kujinasibu / Kujitanabaisha kuwa ni Shabiki na Mpenzi mkubwa tena wa ' Kutukuka ' kabisa wa Chama Tawala cha Mapinduzi ( CCM )

Ninachojaribu kuwashaurini hapa ni kwamba badilikeni halafu sijawalazimisha bali nawashaurini tu kama Marafiki zangu wakubwa wa Kidemokrasia.
Ulishadeclare interest kuwa wew mwanaccm hivyo umekosa moral and ideological authority!!!Ushaur wako kisiasa hauna mantıki hata kidogo,itakua ni maajabu mfuasi wa shetani anamshauriwafuasi wa malaika kubadili strategy ya kupambana naye!!!Itawahitaji common sense kujua wepesi wa ushauri huo hata hivyo haya yanabaki kuwa maoni binafsi amabayo hali ya kawaida yana ukakasi mkubwa kwa unao washauri.
Mwanasayansi nguri wa kisiasa ndugu Bentham mwaka 1980's kipindi cha vita baridi kati ya socialist na capitalist blocks alinena;Opponent in political context is a lost friend!!!
 
Hii taarifa na imfikie Zitto Zuberi Kabwe,Godbless Lema na wengineo wanaopinga kila kitu kinachofanywa na serikali
Ifikie mahala wapinzani uchwara jifunzeni kutoka Nchi za watu(mentioned above).acheni kuvizia vizia visuala kuweni na mipango.
Kuna haja kubwa ya kuwaomba ushauri nguli wa siasa za upinzani duniani wawape hoja za kulisaidia Taifa.bila hivyo mtabaki kusindikiza tawala na tawala
Mpinzani imara bado hajazaliwa hawa waliopo ni opportunities
 
Changamoto kubwa ninayoiona kwako ndugu G katika mada zako umekosa kitu kinaitwa" impersonification".Na hii ni pyschological problem ya hyper tension of knowing!!!Na watu wa namna hii ni too conservative hawataki kuamini kuwa kuna watu wanajua zaidi yao mwishi ufahamu wao unabaki kuwa stagnanted.
Ukipitia maandishi ya great philosophers wengi hutumia impersonification katika kufanya arquement,tafsir yake ni kwamba nao hujifunza kutoka kwa wengine na wengne watajifunza toka kwao,hivyo tuache tabia za jiwe na aliyejisemea ni jiwe hakukosea matendo yanaaksi dhana ya yabisi jiwe!!Haya ni maoni yangu binafsi
 
Vyama vya upinzani haviwezi kufanikiwa kupitia ushauri wa makada wa ccm... ni sawa na YANGA wategemee ushauri wa SIMBA ili kuchukua kombe
Wewe wasema lakini wenye macho matatu tunaona wapinzani walivyo dhaifu katika kila kitu hawana strategy ya kulisaidia Taifa bali kuliangamiza,jifikirie agenda kuu ya upinzani kwa miaka hiii mitano ilikuwa nini???kulazimisha makosa ili wakamatwe????
 
Ulishadeclare interest kuwa wew mwanaccm hivyo umekosa moral and ideological authority!!!Ushaur wako kisiasa hauna mantıki hata kidogo,itakua ni maajabu mfuasi wa shetani anamshauriwafuasi wa malaika kubadili strategy ya kupambana naye!!!Itawahitaji common sense kujua wepesi wa ushauri huo hata hivyo haya yanabaki kuwa maoni binafsi amabayo hali ya kawaida yana ukakasi mkubwa kwa unao washauri.
Mwanasayansi nguri wa kisiasa ndugu Bentham mwaka 1980's kipindi cha vita baridi kati ya socialist na capitalist blocks alinena;Opponent in political context is a lost friend!!!

Muasisi wa Chama Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alipokuwa anatoa mawazo yake kwa CHADEMA na bahati nzuri mara kwa mara hata wana CHADEMA wenyewe wamekuwa wakimpongeza kwa hilo na hata kuweka baadhi ya ' Clips ' zake Mitandaoni hadi katika Kurasa za Mitandao ya CHADEMA. Je hapa pia Nyerere alikosa hiyo Moral and Ideological authority kutoa mawazo yake kwa CHADEMA? Kama jibu ni hapana kwanini leo kwa GENTAMYCINE iwe ni ndiyo na ' nongwa ' Kwako / Kwenu?

Hivi kumbe leo hii Mwana Yanga hawezi kutoa ushauri wake mzuri tu kwa Klabu ya Simba na bado huo ushauri wake ukawa na Tija na Mafanikio kwa Klabu hiyo? Hivi Wazungu na Vyama vyao vya Kisiasa tena huku wakiwa wamekomaa kabisa Kidemokrasia kama wangekuwa hawataki kupokea Mawazo ya Wapinzani Wao leo hii wangeendelea Kisiasa hadi Kimaendeleo hivi? Ni mara ngapi Rais mstaafu wa Marekani Obama alikuwa akichukua / akipokea mawazo ya Chama ' Pinzani ' cha Republicans na bado akawa anayatumia? Je uliwahi kuona mahala popote wana Democrats wanamsema au wanamzuia asiwasikilize?

Kuna Watu hapa Jamvini ni Wapumbavu / Mapopoma sijapata kuona. Ninapokuwa ' nawadharau ' na kuwaambieni hamna ' akili ' msiwe mnabisha kwani huwa sikosei na namaanisha hasa / kweli.
 
Kifupi Leo G umeaandika upuuzi!o!omba mods waotuoe hivi kuna siasa za kistarabu kweli hapa Tanzania mtu anaogopa hata wanachi kusikiliza bunge kwa kigezo kisicho na maaana ili hali yeye anakuwa live hata akinunua mapapai!juzi kasema kuna wabunge wanne wa ccm wanapinga hoja za serikali kwa hyo yy hataki kukosolewa!kazi
 
Uko sahihi na nakubaliana nawe kwa 75% juu ya Hoja yako uliyoiwasilisha hapa ila nilidhani sasa baada ya nyie Wapinzani kuona mmebanwa hivi basi mngejipanda upya na mje Kivingine kuliko kila mara ' Kudandia dandia ' tu matukio ya Kisiasa na Kiutawala yanayofanywa na Chama Tawala ( CCM ) pamoja na Serikali yake kisha mnayatumia kama ' mitaji ' yenu mbele ya ' Wafuasi ' wenu kitu ambacho binafsi sioni kama kina Tija kivile na kitakuja kuwasaidieni kutaka kufika huko mnakokutaka.
Hebu shauri kipi wafanye maana binafsi naona wapo in a right track ndiyo maana wanaswekwa ndani ovyo ovyo, wangekuwa vibogoyo mngekuwa mnawacheka tu mlivyowaweka mfukoni
 
CHADEMA hatutaki mapopoma yaliyotukuka kama wewe,kaa huko huko kwa wajinga wenzako CCM,kwanza umenifanya nitapike kusema eti unampenda nyoka CCM.

Kajifunze ' Matusi ' mapya ya Kunitukana hasa ukizingatia ya kwamba hapa ndiyo Makao Makuu yake na kama umeishiwa nayo sema haraka sana nikuazime yaliyopo katika ' Hazina ' yangu. Na kwa ' Ukomavu ' wangu wa ' Matusi ' bado sijaona ' Tusi ' lolote ulilonitukana hapa sana sana ndiyo nimezidi Kukupuuza kama siyo Kukudharau pia.
 
Back
Top Bottom