GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,385
- 108,450
Mmekuwa ni Marafiki zangu wakubwa na wazuri tu japo Mimi ni Shabiki mkubwa na mzuri wa Chama Tawala Chama Cha Mapinduzi ( CCM ) na sijawahi kufikiria na sidhani kama hata huko mbele itakuja kutokea Mimi GENTAMYCINE nikawa ama Mpinzani au Mwanaharakati japo ninapenda mno na sana uwepo wa Siasa za Kidemokrasia na Upinzani hapa Tanzania.
Kuna tatizo moja nimeanza kuliona linaanza kuota ' mizizi ' hapa Tanzania na kuna muda nilidhani labda ulikuwa ni upepo tu wa muda lakini baadae hili tatizo litatoweka lakini naona sasa hilo tatizo ndiyo limegeuzwa kama mkakati ( strategy ) na ' turufu ' ya Kisiasa ya Wapinzani dhidi ya ' Hasimu ' Wao Mkuu Chama Tawala cha Mapinduzi.
Ni kujidanganya tu na kupotoka kwa Chama cha Siasa au Mwanasiasa wa Tanzania kudhani kwamba ataitoa CCM ' Madarakani ' kwa kila Siku tu Kuvizia ' mabaya ' yake au ' makosa ' yake pekee ndipo yatumike kama njia Kuu ya Kuishtaki kwa Wananchi wa Tanzania.
Nilisema huko nyuma na leo narudia tena kuwa Wapinzani nchini Tanzania mtaeleweka na Wananchi kama tu mtajijenga katika misingi ya Siasa za Kuheshimiana, Siasa za Kujenga Umoja, Siasa za Ushirikiano na Siasa za Mama Tanzania Kwanza huku mkiweka maslahi yenu kwa Tanzania na kuondokana na dhana Kubwa mliyo nayo sasa ya kuwa ' Wachonganishi ' na Watu mnaopenda / mnaotaka kupata ' Public Sympathy ' pekee.
Kuna nchi kadhaa za Afrika naona mnaweza pia mkajifunza katika hili kama vile Zambia, Afrika Kusini na Ghana na kwa huko ng'ambo ( Ulaya ) hadi Marekani pia mna mengi sana ya Kujifunza. Najitahidi sana kufuatilia Siasa za nchi kadhaa hapa Barani Kwetu Afrika na huko Ulaya pamoja na Marekani ila naona kama Siasa ambazo zinafanywa na Wapinzani wa Tanzania ni za ' Kipekee ' kabisa ambazo hazina tija wala mantiki sana sana naona ni za Kujitafutia / Kujizidishia tu matatizo kama mengine ambayo tumeanza sasa kuyaona na yanayowagharimu.
Bado naamini kwamba bila Upinzani Imara chama Changu ' pendwa ' cha CCM hakiwezi kuwa imara na mahiri hivyo nitumie tu fursa hii kuwaomba Wapinzani nchini Tanzania hebu tulieni, jipangeni upya kwani bado hamjachelewa, tengenezeni ' mkakati ' mzuri tu na wa Kistaarabu wa kuweza ' Kupambana ' au ' Kushindana ' Kisera na Chama cha Mapinduzi ili basi muweze kujijengea imani kwa Wananchi na ikiwezekana Siku moja nanyi mje kupewa ' Mamlaka ' na muitawale hii nchi na mtupeleke huko ambako mnataka kutupeleka katika mafanikio.
Nawapenda sana na mno na ndiyo maana sijawa ' Mnafiki ' Kwenu na nimeona leo niwaambieni tu huu ukweli hapa hapa.
Nawasilisha.
Kuna tatizo moja nimeanza kuliona linaanza kuota ' mizizi ' hapa Tanzania na kuna muda nilidhani labda ulikuwa ni upepo tu wa muda lakini baadae hili tatizo litatoweka lakini naona sasa hilo tatizo ndiyo limegeuzwa kama mkakati ( strategy ) na ' turufu ' ya Kisiasa ya Wapinzani dhidi ya ' Hasimu ' Wao Mkuu Chama Tawala cha Mapinduzi.
Ni kujidanganya tu na kupotoka kwa Chama cha Siasa au Mwanasiasa wa Tanzania kudhani kwamba ataitoa CCM ' Madarakani ' kwa kila Siku tu Kuvizia ' mabaya ' yake au ' makosa ' yake pekee ndipo yatumike kama njia Kuu ya Kuishtaki kwa Wananchi wa Tanzania.
Nilisema huko nyuma na leo narudia tena kuwa Wapinzani nchini Tanzania mtaeleweka na Wananchi kama tu mtajijenga katika misingi ya Siasa za Kuheshimiana, Siasa za Kujenga Umoja, Siasa za Ushirikiano na Siasa za Mama Tanzania Kwanza huku mkiweka maslahi yenu kwa Tanzania na kuondokana na dhana Kubwa mliyo nayo sasa ya kuwa ' Wachonganishi ' na Watu mnaopenda / mnaotaka kupata ' Public Sympathy ' pekee.
Kuna nchi kadhaa za Afrika naona mnaweza pia mkajifunza katika hili kama vile Zambia, Afrika Kusini na Ghana na kwa huko ng'ambo ( Ulaya ) hadi Marekani pia mna mengi sana ya Kujifunza. Najitahidi sana kufuatilia Siasa za nchi kadhaa hapa Barani Kwetu Afrika na huko Ulaya pamoja na Marekani ila naona kama Siasa ambazo zinafanywa na Wapinzani wa Tanzania ni za ' Kipekee ' kabisa ambazo hazina tija wala mantiki sana sana naona ni za Kujitafutia / Kujizidishia tu matatizo kama mengine ambayo tumeanza sasa kuyaona na yanayowagharimu.
Bado naamini kwamba bila Upinzani Imara chama Changu ' pendwa ' cha CCM hakiwezi kuwa imara na mahiri hivyo nitumie tu fursa hii kuwaomba Wapinzani nchini Tanzania hebu tulieni, jipangeni upya kwani bado hamjachelewa, tengenezeni ' mkakati ' mzuri tu na wa Kistaarabu wa kuweza ' Kupambana ' au ' Kushindana ' Kisera na Chama cha Mapinduzi ili basi muweze kujijengea imani kwa Wananchi na ikiwezekana Siku moja nanyi mje kupewa ' Mamlaka ' na muitawale hii nchi na mtupeleke huko ambako mnataka kutupeleka katika mafanikio.
Nawapenda sana na mno na ndiyo maana sijawa ' Mnafiki ' Kwenu na nimeona leo niwaambieni tu huu ukweli hapa hapa.
Nawasilisha.