Kama utiifu wa Jeshi hutegemea viongozi wa juu wa Majeshi, kina Samweli Doe waliweza kufanya mapinduzi?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,993
144,329
Hii dhana kuwa Jeshi linapokuwa na utii ni matokeo ya viongozi wa juu wa Jeshi huwa inanifanya nijiulize kama huo ndio ukweli, mtu kama Samweli Doe aliwezaje kuongoza mapinduzi ya kijeshi akiwa na cheo Sergeant?

Hata Idd Amini si alikuwa na cheo kidogo tu jeshini alipopindua serikali?

Labda swali liwe ni vipi wanajeshi wa ngazi za chini katika mataifa mbalimbali duniani huweza kufanikisha mapinduzi ya kijeshi huku wakubwa zao wakiwemo?
 
Huwa wanakuwa chambo tu ya mabosi zao ndio pindi tu inaposikika kuwa serikali imepinduliwa utaona kambi zote katika nchi husika zinaheshima bila reaction yeyote zaidi ya kuunga mkono mapinduzi.
 
Wale wenye vyeo vya chini hukutana kila mara na kazi wanafanya pamoja hivyo hata kupanga kitu ni rahisi sana kuliko wakubwa ambao wao kila mmoja na ofisi yake na sehemu mbali mbali.
 
Mipango hii mara nyingi huwa ina mkono wa Mzungu!!! kwa malengo yao mahususi kabisa wa maksudi hasa km huendani na mipango yao!!! mara nyingi km umekataa kutimiza malengo yao hasa hsa yenye faida kiuchumi!

au sababu za kiusalama zaidi!! dhidi ya mahasimu wa serikali husika mfano, Mreno hakuipenda Bongo ajili ya kumlea Samora na chama lake la FRELIMO lazima akutwange tu! au wamsaidiea mtu mmoja mzalendo kudhoofisha serikali yako! km Savimbi na Angola!

Na wanataka ukipata urais ufuate matakwa yao! ukikataa ndo wanakufanya km Saddam Hussein! au Hissen Habre wa Chad, au Idd Amini dada! Wa uganda huyu angekomaa na yale aliyoagizwa wala Bongo tusinge muweza!

Kamuzu Banda alikuwa na wasiwasi na Bongo baada ya kumtwanga Idd amini lkn alimtuma baba yangu pamoja na mkapa kumtuliza moyo!! na kweli kamoyo kakatulia tuli!

Wakati wa zamani nchi za africa zilikuwa na umoja dhdi ya vibaraka wote!! km alivyo fanywa savimbi! dhidi ya Augustino Neto! huyu hakutia pua nchi yeyote Africa!!

Baada ya sisi sote kuwa Huru sasa amebaki mkoloni anapigapiga mara leo pale kesho kule! mapinduzi yamepungua!! tatizo Bara la Africa linagombewa km Binti Mrembo mzuriiii sana, na wanaume! Lukuki na yeye hajui amchukue nani!!!

Akienda huku huyu na yule wanakasirika!! sasa lazima uwe na Bwana mmoja tu!! na ndo akupe hela na miti! na misaada usichukue kule!! km mfano ni Hissene Habre yeye alihamia USA kupata misaada huko, akamponda France weeeee!! kwani alikaa!!

mpaka juzi juzi kifo yule jamaa kimemkuta gerezani la ufaransa hakuijua Chad tena kiviile! Lazima Rais uwe macho hasa! usomi weka kando chunga maisha yako na ukitoka uraisini pia shida, unapaswa ujiangalie sana sababu utaishi kwa wasiwasi mno si unamuona nKurunzinza!! yuko wapi leo?? na siku ya kufa utaijua tu!

angalia yalo mkuta Binti wa Agustino Neto tena Rafiki yake aliye muamini hasa!!! .......... watu km Mnagagwa ni wachache sana na yule jamaa ataishi maisha marefu mnooo!! akifanya uhoko anakuwa km yalo mkuta Chiluba!! africans wengi wamejifunza kutoka kwa mchonga!
 
Back
Top Bottom