Kama uongozi wa juu wa Taifa ungeruhusu Vyama vya Upinzani kuendelea na shughuli zao za Siasa tangu Mwaka 2015 basi haya ya leo yasingelikuwepo

Habari za Mchana Wanajukwaa?

Kama kichwa cha habari kinavyoeleza hapo juu.

Kwa mwaka huu kampeni kwa vyama vya upinzani imekuwa rahisi kwa sababu ya MKULU kuzuia siasa tangu 2015.

Wanachofanya upinzani ni kuanika mambo mabaya ya Uongozi uliopo madarakani kisha kupendekeza njia za kutatua mambo hayo.

Kama siasa kwa upinzani ingelikuwepo tangu 2015 basi Upinzani ungelizungumzia mambo hayo kabla ya kampeni ya sasa hivyo viongozi wa chama kilichopo madarakani au viongozi wa serikali kupata nafasi ya kufafanua vizuri kwa wananchi (yaani kujibu hoja za upinzani) kama ilivyokuwa katika awamu zilizopita.

Kwa sasa Chama kilichopo madarakani kina shughuli kubwa ya kufanya kampeni muda huohuo kujibu hoja za Upinzani wakati mwingine inapelekea kujibu hoja vibaya au kwa kutowaridhisha wananchi kutokana na hali halisi ya mahudhirio ya wananchi kwenye mikutano,umuhimu wa hoja husika,muda,hali ya kweli ya maisha ya wananchi n.k.

PENDEKEZO LANGU
Napendekeza kwa Chama Chochote kitakachoshika Dola Nchini Tanzania (Nchi ya Vyama Vingi) kiruhusu Siasa wakati wote kwa ajili ya kujibu hoja mbalimbali za Upinzani.

Nawasilisha.
Magugumaji alikuja na akili zake za Maganda ya Korosho akijua zinalipa hapa mjini, Sasa yuko hoi bin taaban akifanya Kampeni siku 2 analala siku 5
 
Walituaminisha kuwa kutokana na kuwaziba midomo wapinzani, kampeni za mwaka huu kwao CCM zingekuwa nyepesi sana, lakini mambo yamekuwa viceversa! Kuna taharuki, hawajuwi washike lipi , waache lipi! Walisema watajikita kwenye kutangaza na kuonyesha miradi sasa wameacha wanajibu tu hoja za wapinzani, je ilani yao iko wapi? Wepesi wa kampeni za ccm uko wapi? Ni hapa ndipo utajuwa kuwa hiki chama hakina maono, kinatupeleka gizani, ni wakati sasa tupate uwongozi mbadala wa kutuvusha tulipokwama!

Hoja za wapinzani za hakuna barabara, hakuna maji, hakuna watoto wanaolipiwa ada, hakuna ndege, hakuna kilimo kilicho ongezeka hakuna ongezeko la mikopo kwa wanafunzi, watu hawalipwi mishahara yao kwa wakati, hakuna hospitali zilizo jengwa ?

Kwa akili za kuvukia barabara, ni hoja zinazotakiwa kujibiwa?

Ogopa sana muongo na mpumbavu mwenye ujasiri.
 
Back
Top Bottom