Kaka mwisho
JF-Expert Member
- Dec 19, 2011
- 402
- 167
Ndugu zangu kuna watu wanapenda sana kufanya shughuli za ziada kama kilimo na ufugaji lakini tatizo wanakuwa hawana muda wa kusimamia kutokana na majukumu ya kazi zao za kiofisi kwa walio ajiriwa. Nategemea kuanza kilimo cha tikiti maji mkuranga mwezi wa pili na baadae taanzisha mradi wa kuku wa kienyeji na baadae wa kisasa na mbuzi. Kwahiyo kwa yoyote ambaye anapenda kufanya hizi shughuli lakni hana muda wa kutosha kutokana na majukumu ya kikazi naomba tuwasiliane kwa pm ili tujadili jinsi ya kushirikiana kwa hili na kuonana kabsa ili kutambuana vizuri. Nawakaribisha wadau wote wanaopenda kulima na kufuga mkuranga.