Kama unaogopa hasara, baki na hela zako

Asante ..... umeeleweka ila kuweka fedha zote kwenye biashara tena kipindi hiki yataka moyo ila mimi nitaanza kujifunza baada ya awamu hii kuisha
 
Mkuu inabidi ulute nyuzi zingine ambazo zinafundisha maswala ya ujasriamali ili watu wajifunze kabla ya kuingia kwenye biashara.
Inaonekana una mawazo mazuri
 
Sikia....

Mzee Mengi alikuwa na gazeti linaitwa ALASIRI. Halikuleta faida. Gazeti la Dar Leo vile vile. Ushindani wa magazeti mengine ulikuwa mkali. Wasomaji wakabadilika. Internet zikaingia nk.
Akaachana nayo. Afu wewe eti unataka ufundishwe biashara ambayo hutaki kupoteza hela. Kaa na hela zako tu kwa kweli.

Hivi unadhani Novida imeenda wapi. Kama Coca Cola wanakosa soko la bidhaa yao wewe je? Lakini CocaCola wamefilisika? Mengi amefilisika? No.

Okay, tufanye hivi, ule ukumbi wa Sinema pale Mwenge ITV ulikufa kifo cha fasta. Competition. Century Cinemax ilileta upinzani. Wenye mradi wakajifunza.

Kuna matajiri wengi tu walipoteza sana pesa. Mabasi ya Scandinavia yapo tena? Kuna maduka mengi tu Kariakoo yamefungwa kipindi hiki.
Ni kawaida kwenye ulimwengu wa biashara. Si uliona Landmark Hotel Ubungo ilibadilishwa ikawa hostel. Umeona jinsi ambavyo tayari amerejea na kuwa hoteli ya kisasa zaidi. Alishajifunza. Sijui unaelewa?

Dar Village hapo Rose Garden Kijitonyama haijajengwa hadi leo. Mradi wa mabilioni uliingia mdudu miaka zaidi ya 8 sasa. Wewe unataka utakachoanza nacho kisife. Hela zako hutaki zipotee. Aisee you're not an entrepreneur. Kaa tu na hela zako. Bora ukazinywee soda tu au kula nyama choma kama unataka. Umekuwa mtu wa kutaka mafanikio yasiyo na changamoto yoyote. Ndo maana unasubiri ukiambiwa aisee biashara ya Matikiti inalipa hatari huyo umo. Ukiambiwa mayai ya kware yanalipa huyo. Hutaki kutulia kwanza ujifunze.

Hakuna biashara isiyolipa. Ila kuna akili zisizo za kibiashara ambazo lazima kuzibadili zijue biashara faida na hasara ni kawaida kabisa. Wanasema SOMETIMES YOU WIN AND SOMETIMES YOU LEARN.

Sasa wewe hutaki kulearn utafikaje kwenye mafanikio kibiashara?

Trump mwenyewe alifilisika kabisa. NIL. Zero. Rock bottom. Licha ya kuanza kwa mtaji mkubwa. Kama haupo tayari kukosekana pesa basi kazinunulie nguo mpya sikukuu zikifika uvae.

Na hiyo ndo maana kuna matajiri wachache. Wenye moyo wa UTHUBUTU katika jamii huwa ni wachache tu.

If you're afraid to lose money NEVER INVEST. Baki na hela zako.
You have made my day
 
Biashara 400 zinakufa kila mwezi na 400 zinazaliwa
Ni kuwa na dedication tu na back-up ya kujitosheleza
 
Kuna watu wanajua sana kuwashauri wenzao kuhusu biashara. Ye mwenyewe anakula kwa mshukaji....

Anaandika kitabu kizuri chenye cha "How to make money" halafu anaomba pesa kwa wengine..
 
Biashara ni mchakato....hebu jiulize waliojenga viwanda mfano cement n.k unadhani baada ya muda gani wataanza kupata faida?unaweza kuta baada ya miaka 5,10 n.k kwa hiyo cha muhimu ni uvumilivu.
 
Tushirikishe biashara yako tujifunze sorry
Mawazo mazuri sana,tuyafanyie kazi ili tujikwamue kiuchumi...binafsi yamenipa faraja kwasababu hiyo safari niliianza tangu mwaka jana, namshukuru Allah ( S.W ) nimesahau kusubiri mshahara wa mwisho wa mwezi.
biashara
 
Back
Top Bottom