GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,468
- 108,621
1. USHIRIKINA
Tambueni ya kwamba katika Mechi hiyo (hii) Yanga SC ndiyo Mwenyeji na hakuna asiyejua kuwa Timu hizi Mbili (Vilabu hivi Vikubwa viwili ) ni 'Mabingwa' wa 'Ushirikina / Ndumbaism' na hata kwa 99% Matokeo ya Mechi zao huamuliwa na 'Majini' tupu na siyo Makocha, Wachezaji au Waamuzi. Yanga SC 'walishachungulia' na Kuona kuna 'Dhahama' ilikuwa inaenda Kuwaangukia. Na hata Kinujumu (Kiutabiri) tarehe ya 18 Oktoba imekaa vibaya. Wale 'Wabobezi' wa Kamati za 'Shirki' najua hapa mtanielewa sana.
2. KUMLINDIA HESHIMA KOCHA MPYA CEDRIC KAZE
Mara baada ya Yanga SC kuweza 'Kuchungulia' katika Bakuli la 'Kiushirikina' kwa Babu na Kugundua ya kwamba hiyo tarehe 18 Oktoba kuna 'Gharika' lilikuwa linaenda 'Kuwaangukia' wakaona kuwa pia 'ingemchafua' sana Kocha wao mpya Mburundi Cedric Kaze ambaye siyo 'Siri' kwa aina ya CV yake tu na uwezo wake kama angekuja na Kushuhudia Kipigo cha 'Shalubela' ambacho Klabu yake ya Yanga ingekipata kutoka kwa Simba SC basi ingemshusha mno 'Hadhi' yake. Kumbukeni Yanga SC ndiyo Mwenyeji kabisa.
3. HOFU YA KISIASA NDANI YA VILABU HIVI VIWILI
Japo haiwekwi / haijawekwa Wazi kivile na inajaribu 'Kuzimwa' Kimya Kimya inajulikana kuwa Klabu ya Yanga ina 'Vinasaba' vyote vya 'Kimahusiano' na Chama Tawala na Kikongwe nchini cha CCM na Klabu ya Simba nayo ina 'Vinasaba' vya mbali kidogo na Chama 'Maarufu' cha Upinzani cha CHADEMA. Hivyo kama 'Matokeo' ya 'Derby' hiyo yangeenda vibaya kwa Yanga SC yenye Jezi za Rangi ya CCM za Kijani na Njano huenda 'ingeathiri' hata upande wa CCM na katika Kipindi hiki muhimu cha Kampeni. Na kuna taarifa za chini chini nimedokezwa kuwa kuna Viongozi 'Waandamizi' vya Vyama hivi 'Hasimu' Kisiasa wangeenda Mpirani.
4. UIMARA WA SIMBA SC AMBAO UNAONEKANA KUWA TISHIO KWA WADHAMINI WAKUU WA YANGA GSM
Hili halina 'Ubishi' labda ni kwa Mpumbavu (Popoma) tu pekee kujua ya kwamba Klabu ya Simba inacheza Mpira mkubwa (mwingi) na inauwezo wa 'Kukufunga' muda wowote ule kwakuwa ni Timu ambayo hata 'Chemistry' yake Uwanjani 'imeshakubali' na inashinda Magoli mengi huku ikiwa inacheza Mpira wa 'Kuburudisha' vile vile. Kwaku Yanga SC ni Mwenyeji na ipo chini ya Mdhamini GSM mwenye 'Ushawishi' mkubwa ndani ya Uongozi wa Klabu hivyo kwa 'Kukwepa' aibu kwani 'Injinia' Hersi 'ameshawaaminisha' wana Yanga SC endapo angefungwa Mashabiki na wana Yanga wasingemwelewa.
5. MPANGO WA SIRI WA YANGA JUU YA KUWAOMBA WACHEZAJI WA TIMU PINZANI WAWAUMIZE WA SIMBA KUTOKAMILIKA
Kama ukibahatika Kukutana na Viongozi wa juu kabisa (Waandamizi) wa Yanga SC tena 'Chobingo' kabisa utasikia wanakiri wazi wazi kuwa Simba SC ina Wachezaji wengi 'Talented' na wenye uwezo wa Kuamua 'Matokeo' muda wowote ule. Yanga SC wameogopa kwakuwa ule Mpango wao wa 'Siri' wa Kuwaomba Wachezaji wa Timu Pinzani zinazocheza na Simba SC 'Wawaumize' Wachezaji 'Muhimu' wa Simba SC 'Kutokamilika' na mpaka hivi leo wote ni wazima. Na kupitia hapa hapa tu niwaonye Simba SC wawe 'Makini' kwani huu Mpango 'Ovu' dhidi ya Wachezaji 'Mafundi' Kuumizwa bado upo pale pale.
6. MAJERUHI NDANI YA KIKOSI CHA KWANZA CHA YANGA SC
Najua kuwa hili Yanga SC 'wanaficha' ila Sisi Watu wa Mpira akina GENTAMYCINE tunajua kuwa mpaka jana kuna Wachezaji kama Wanne au Watano tena Waandamizi na wapo katika 'First Eleven' ya Yanga SC ni 'Majeruhi' na kwamba huenda hayo 'Majeraha' yao yakaja Kupona ndani ya Wiki kama Mbili zijazo hivyo Yanga SC ingeenda Kukutana na Simba SC hiyo tarehe 18 Oktoba huenda safari hii si tu kwamba 'wangefungwa' Goli nyingi lakini pia 'wangeaibika' mno na 'Klabuni' Kusingekalika tena. Kumbukeni Mechi hii Yanga SC ndiyo Mwenyeji hivyo lazima aingie akiwa 'amejidhatiti' kabisa na GSM iendelee Kuaminika.
7. KUTAKA KUJIPANGA ZAIDI KIMAPATO HASA KATIKA MCHEZO (MECHI) HIYO
Baada ya Klabu ya Yanga kuona kuwa kuna 'tatizo' kubwa hasa upande wa Ukataji wa Tiketi Uwanjani ambalo Klabu ya Simba ni 'Wahanga' wakubwa katika hili hasa katika Michezo yake Miwili iliyocheza Uwanja wa Mkapa hii 'imewashtua' zaidi Yanga SC na kuona ya kwamba ipo haja Kwanza 'Kujipanga' nalo mapema ili kuweza kujua 'Mfumo' wake mzima ili basi Siku hiyo ya Mechi waweze Kujipatia Pesa nyingi za 'Kimapato' tofauti na ilivyozoeleka huko nyuma. Na katika hili najua hata Bodi ya Ligi na TFF nao wanashirikiana na Yanga SC kwani Yanga Kuvuna' Pesa nyingi ndiyo hata TFF nao 'inavuna' Pesa nyingi vile vile tu.
HITIMISHO
Hakuna mahalo popote pale ambapo Mimi GENTAMYCINE nimekulazimisha ukubaliane kwa hiki nilichokiandika hapa ila Mimi nakikubali na kukiamini kwakuwa nipo katika Soka hili la Bongo lenye 'Fitina' na 'Kisununu' kwa muda mrefu na hata Mimi vile vile nimeshawahi kutumika katika 'Umafia' Mmoja dhidi ya Mechi ya Simba na Yanga ile ambayo Yanga 'ilikufa' Bao / Goli Tano (5) leo kwa Mkapa ila zamani kwa Mchina. Na nina 'Imani' kuwa hata Mwenyezi Mungu 'amenisaheme' kwa 'Kufuru' niliyoifanya.
Wale 'Masokolokwinyo' ambao mnapenda mno 'Kuchukua' haya 'Mabandiko' yangu hapa JamiiForums na kuyaweka huko katika sijui 'Viblogu' vyenu au 'Mitandao' yenu ya 'Kihabari' tafadhalini mkiikopi hii (na wala siwazuii) ila nipeni tu 'Credit' yangu au 'Acknowledgement' yangu kuwa mmeitoa katika huu Mtandao wangu 'pendwa' wa JamiiForums na kwa 'Member' Mimi mwenye GENTAMYCINE. Na huu ndiyo Ustaarabu hasa kwa 'Intellectuals' popote pale duniani. Nadhani hapa nimeelewaka.
Tambueni ya kwamba katika Mechi hiyo (hii) Yanga SC ndiyo Mwenyeji na hakuna asiyejua kuwa Timu hizi Mbili (Vilabu hivi Vikubwa viwili ) ni 'Mabingwa' wa 'Ushirikina / Ndumbaism' na hata kwa 99% Matokeo ya Mechi zao huamuliwa na 'Majini' tupu na siyo Makocha, Wachezaji au Waamuzi. Yanga SC 'walishachungulia' na Kuona kuna 'Dhahama' ilikuwa inaenda Kuwaangukia. Na hata Kinujumu (Kiutabiri) tarehe ya 18 Oktoba imekaa vibaya. Wale 'Wabobezi' wa Kamati za 'Shirki' najua hapa mtanielewa sana.
2. KUMLINDIA HESHIMA KOCHA MPYA CEDRIC KAZE
Mara baada ya Yanga SC kuweza 'Kuchungulia' katika Bakuli la 'Kiushirikina' kwa Babu na Kugundua ya kwamba hiyo tarehe 18 Oktoba kuna 'Gharika' lilikuwa linaenda 'Kuwaangukia' wakaona kuwa pia 'ingemchafua' sana Kocha wao mpya Mburundi Cedric Kaze ambaye siyo 'Siri' kwa aina ya CV yake tu na uwezo wake kama angekuja na Kushuhudia Kipigo cha 'Shalubela' ambacho Klabu yake ya Yanga ingekipata kutoka kwa Simba SC basi ingemshusha mno 'Hadhi' yake. Kumbukeni Yanga SC ndiyo Mwenyeji kabisa.
3. HOFU YA KISIASA NDANI YA VILABU HIVI VIWILI
Japo haiwekwi / haijawekwa Wazi kivile na inajaribu 'Kuzimwa' Kimya Kimya inajulikana kuwa Klabu ya Yanga ina 'Vinasaba' vyote vya 'Kimahusiano' na Chama Tawala na Kikongwe nchini cha CCM na Klabu ya Simba nayo ina 'Vinasaba' vya mbali kidogo na Chama 'Maarufu' cha Upinzani cha CHADEMA. Hivyo kama 'Matokeo' ya 'Derby' hiyo yangeenda vibaya kwa Yanga SC yenye Jezi za Rangi ya CCM za Kijani na Njano huenda 'ingeathiri' hata upande wa CCM na katika Kipindi hiki muhimu cha Kampeni. Na kuna taarifa za chini chini nimedokezwa kuwa kuna Viongozi 'Waandamizi' vya Vyama hivi 'Hasimu' Kisiasa wangeenda Mpirani.
4. UIMARA WA SIMBA SC AMBAO UNAONEKANA KUWA TISHIO KWA WADHAMINI WAKUU WA YANGA GSM
Hili halina 'Ubishi' labda ni kwa Mpumbavu (Popoma) tu pekee kujua ya kwamba Klabu ya Simba inacheza Mpira mkubwa (mwingi) na inauwezo wa 'Kukufunga' muda wowote ule kwakuwa ni Timu ambayo hata 'Chemistry' yake Uwanjani 'imeshakubali' na inashinda Magoli mengi huku ikiwa inacheza Mpira wa 'Kuburudisha' vile vile. Kwaku Yanga SC ni Mwenyeji na ipo chini ya Mdhamini GSM mwenye 'Ushawishi' mkubwa ndani ya Uongozi wa Klabu hivyo kwa 'Kukwepa' aibu kwani 'Injinia' Hersi 'ameshawaaminisha' wana Yanga SC endapo angefungwa Mashabiki na wana Yanga wasingemwelewa.
5. MPANGO WA SIRI WA YANGA JUU YA KUWAOMBA WACHEZAJI WA TIMU PINZANI WAWAUMIZE WA SIMBA KUTOKAMILIKA
Kama ukibahatika Kukutana na Viongozi wa juu kabisa (Waandamizi) wa Yanga SC tena 'Chobingo' kabisa utasikia wanakiri wazi wazi kuwa Simba SC ina Wachezaji wengi 'Talented' na wenye uwezo wa Kuamua 'Matokeo' muda wowote ule. Yanga SC wameogopa kwakuwa ule Mpango wao wa 'Siri' wa Kuwaomba Wachezaji wa Timu Pinzani zinazocheza na Simba SC 'Wawaumize' Wachezaji 'Muhimu' wa Simba SC 'Kutokamilika' na mpaka hivi leo wote ni wazima. Na kupitia hapa hapa tu niwaonye Simba SC wawe 'Makini' kwani huu Mpango 'Ovu' dhidi ya Wachezaji 'Mafundi' Kuumizwa bado upo pale pale.
6. MAJERUHI NDANI YA KIKOSI CHA KWANZA CHA YANGA SC
Najua kuwa hili Yanga SC 'wanaficha' ila Sisi Watu wa Mpira akina GENTAMYCINE tunajua kuwa mpaka jana kuna Wachezaji kama Wanne au Watano tena Waandamizi na wapo katika 'First Eleven' ya Yanga SC ni 'Majeruhi' na kwamba huenda hayo 'Majeraha' yao yakaja Kupona ndani ya Wiki kama Mbili zijazo hivyo Yanga SC ingeenda Kukutana na Simba SC hiyo tarehe 18 Oktoba huenda safari hii si tu kwamba 'wangefungwa' Goli nyingi lakini pia 'wangeaibika' mno na 'Klabuni' Kusingekalika tena. Kumbukeni Mechi hii Yanga SC ndiyo Mwenyeji hivyo lazima aingie akiwa 'amejidhatiti' kabisa na GSM iendelee Kuaminika.
7. KUTAKA KUJIPANGA ZAIDI KIMAPATO HASA KATIKA MCHEZO (MECHI) HIYO
Baada ya Klabu ya Yanga kuona kuwa kuna 'tatizo' kubwa hasa upande wa Ukataji wa Tiketi Uwanjani ambalo Klabu ya Simba ni 'Wahanga' wakubwa katika hili hasa katika Michezo yake Miwili iliyocheza Uwanja wa Mkapa hii 'imewashtua' zaidi Yanga SC na kuona ya kwamba ipo haja Kwanza 'Kujipanga' nalo mapema ili kuweza kujua 'Mfumo' wake mzima ili basi Siku hiyo ya Mechi waweze Kujipatia Pesa nyingi za 'Kimapato' tofauti na ilivyozoeleka huko nyuma. Na katika hili najua hata Bodi ya Ligi na TFF nao wanashirikiana na Yanga SC kwani Yanga Kuvuna' Pesa nyingi ndiyo hata TFF nao 'inavuna' Pesa nyingi vile vile tu.
HITIMISHO
Hakuna mahalo popote pale ambapo Mimi GENTAMYCINE nimekulazimisha ukubaliane kwa hiki nilichokiandika hapa ila Mimi nakikubali na kukiamini kwakuwa nipo katika Soka hili la Bongo lenye 'Fitina' na 'Kisununu' kwa muda mrefu na hata Mimi vile vile nimeshawahi kutumika katika 'Umafia' Mmoja dhidi ya Mechi ya Simba na Yanga ile ambayo Yanga 'ilikufa' Bao / Goli Tano (5) leo kwa Mkapa ila zamani kwa Mchina. Na nina 'Imani' kuwa hata Mwenyezi Mungu 'amenisaheme' kwa 'Kufuru' niliyoifanya.
Wale 'Masokolokwinyo' ambao mnapenda mno 'Kuchukua' haya 'Mabandiko' yangu hapa JamiiForums na kuyaweka huko katika sijui 'Viblogu' vyenu au 'Mitandao' yenu ya 'Kihabari' tafadhalini mkiikopi hii (na wala siwazuii) ila nipeni tu 'Credit' yangu au 'Acknowledgement' yangu kuwa mmeitoa katika huu Mtandao wangu 'pendwa' wa JamiiForums na kwa 'Member' Mimi mwenye GENTAMYCINE. Na huu ndiyo Ustaarabu hasa kwa 'Intellectuals' popote pale duniani. Nadhani hapa nimeelewaka.