kibaravumba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 6,635
- 7,005
Najua wapo wengi wanajiuliza mustakabali wa kisiasa katika miaka mitano ijayo na kubaki wakiumia tu. Wanaumia kutokana na ukweli kwamba, nafasi karibu zote za uwakilishi wa kisiasa, zimechukuliwa na CCM.
Imefika muda tukubali tu kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.
Viongozi wa dini wengi wanakiunga mkono chama hiki. Wasanii wengi wanakiunga mkono chama hiki. Matajiri wengi wanakiunga mkono chama hiki.
Kina mama wengi wanakiunga mkono. Wasomi wengi wanakiunga mkono. Cha kushangaza zaidi wale maskini ndio wanaongoza kutoa dhihaka kwa wapinzani walioshindwa.
Nimebaki najiuliza hawa wapinzani ni nani? Ni watu wa aina gani? Wale wasomi wa tabia za binadamu niambieni, huenda kuna watu wamezaliwa wapinzani?Kama ndivyo tusaidieni maana kama upinzani ni tabia, basi naona kabisa si tabia nzuri. Haiwezekani hata Mungu awasuse.
Maana kupigwa ni wao, kuteswa ni wao, ikibidi kufa ni wao. Hii si ishara mbaya?
Kama kuna mtu ana elimu tafadhali,atuelimishe sie. Maana imeandikwa watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Mungu amewakataa watu wasio na maarifa. Kama ni dhambi kuwa mpinzani tuambieni,watu wengi hawapendi dhambi japo wanaitenda. Lakini ni vibaya sana kufanya kitu ukijua ni halali Kumbe si halali.
Au wasomi mmeshindwa pia kujua kwa nini kuna wapinzani?Au adui yetu "ujinga" bado ni tishio licha ya kuongezeka kwa vyuo vikuu?
Mwisho nitoe wito kuwa,inabidi tukubali kuwa Mungu amewapa kibali ccm. Pia nawaomba ccm, kuliko kuruhusu watu kuteswa, kupigwa mabomu, na hata risasi za moto kwa vile tu ni wapinzani, fanyeni jambo moja muhimu sana; Futeni sheria ya vyama vingi. Sasa mpo wengi bungeni hakuna mtu wa kuwazuia. Epusheni watu kuumizwa kwa kuwa wao ni wapinzani. Mungu atazidi kuwabariki
Imefika muda tukubali tu kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.
Viongozi wa dini wengi wanakiunga mkono chama hiki. Wasanii wengi wanakiunga mkono chama hiki. Matajiri wengi wanakiunga mkono chama hiki.
Kina mama wengi wanakiunga mkono. Wasomi wengi wanakiunga mkono. Cha kushangaza zaidi wale maskini ndio wanaongoza kutoa dhihaka kwa wapinzani walioshindwa.
Nimebaki najiuliza hawa wapinzani ni nani? Ni watu wa aina gani? Wale wasomi wa tabia za binadamu niambieni, huenda kuna watu wamezaliwa wapinzani?Kama ndivyo tusaidieni maana kama upinzani ni tabia, basi naona kabisa si tabia nzuri. Haiwezekani hata Mungu awasuse.
Maana kupigwa ni wao, kuteswa ni wao, ikibidi kufa ni wao. Hii si ishara mbaya?
Kama kuna mtu ana elimu tafadhali,atuelimishe sie. Maana imeandikwa watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Mungu amewakataa watu wasio na maarifa. Kama ni dhambi kuwa mpinzani tuambieni,watu wengi hawapendi dhambi japo wanaitenda. Lakini ni vibaya sana kufanya kitu ukijua ni halali Kumbe si halali.
Au wasomi mmeshindwa pia kujua kwa nini kuna wapinzani?Au adui yetu "ujinga" bado ni tishio licha ya kuongezeka kwa vyuo vikuu?
Mwisho nitoe wito kuwa,inabidi tukubali kuwa Mungu amewapa kibali ccm. Pia nawaomba ccm, kuliko kuruhusu watu kuteswa, kupigwa mabomu, na hata risasi za moto kwa vile tu ni wapinzani, fanyeni jambo moja muhimu sana; Futeni sheria ya vyama vingi. Sasa mpo wengi bungeni hakuna mtu wa kuwazuia. Epusheni watu kuumizwa kwa kuwa wao ni wapinzani. Mungu atazidi kuwabariki