Nigendako
JF-Expert Member
- Dec 1, 2017
- 23,297
- 122,384
HahahRafiki yangu alikuwa
amesinzia tukiwa darasani,
nikachukua simu yake
nikabadilisha alivyosave
namba yangu nikasave "lovely
dad" (ndivyo alivyokuwa
amesave jina la baba yake
mzazi)
Nikamtumia SMS "mwanangu
nimeshinda millioni 100 toka
BIKO, na sasa hivi tutakuwa
na maisha mazuri. Acha
shule njoo tupange tutafanya
biashara gani"
Rafiki yangu baada ya
kusoma sms akanyanyuka na
kukusanya kila kilicho chake
akaanza kuondoka.
Alipofika mlangoni mwalimu
akamuuliza unaenda wapi
bila kuomba ruhusa?
Akageuka akamwonyesha
mwalimu kidole cha kati,
akaachia mfyonzo mkali kisha
akasepa.
Sasa hivi ananisaka kinyama,
nani anajua sehemu nzuri ya
kujifichia