Kama una stress pitia hapa, usiache kutupia na wewe maneno yako

Jeshini bana! Eti afande anakwita jina we ni kuitika neno afande, hata ukiulizwa jina unatakiwa utaje jina lako kisha umalizie na neno afande! Sasa kuna dogo (askari) anaitwa Mboya kalizua huko
Afande: We askari unaitwa nani?
Askari (dogo): Naitwa Mboya
Afande:
Unaitwa nani? (kwa ukali)
Askari (dogo): Naitwa Mbooya Mboo ya Afande!
Afande: Huna adabu!


"Cᵒᵃᶜᵏʳᵒᵃᶜʰ ⁿᵘʰ ᵇᵘˢˢⁱⁿᵉˢˢ ⁱⁿⁿᵃ ᶠᵒʷˡ ᶠⁱᵍʰT"
 
Ni
Okay, kumbe unaielewa hali yako!
Karibu..

Niliwahi kusikia kuwa maji na mafuta havichangamani, na pia mafuta huwa yanaelea juu ya maji... Basi jana mimi nikaamua kupaka mafuta mengi tu miguuni kisha nikaingia baharini ili niweze kutembea juu ya maji maana nilihisi ningeelea na kuweza kufanya chochote.
Sikumbuki nini kilitokea lakini nilijikuta nimelala mchangani watu wakiwa wamenizunguka huku wakisema niwashukuru sana wavuvi. Nadhani watakuwa wamenipa samaki wa bure.
Nice
 
Kuna vijimisemo vifupi vimeibuka huku kwenye mitandao kwa sasa, yaani ni burudani tupu.

Ukivisoma mwisho lazima ubaki mdomo wazi au ucheke, baadhi ya niliyokutana nayo naweka hapa, pia karibuni kwa wenye zaidi tuburudike pamoja.
Tuanze na hivi:-

1. Leo kidogo nipigwe na mwanamke baada ya lifti kusimama, wakati tupo kwenye lifti Nilikua nayaangalia maziwa yake akasema "Bonyeza moja" mimi si nikalibonyeza yaani hadi sasa bado najiuuliza nilipokosea?

2.Hivi utajisikieje utakaposikia rafiki yako wa karibu hajaja kwenye mazishi yako? Nadhani mimi sitamwongelesha tena!
nafikiri nakaribia kupona

3.Nimenunua chips ili nile. Kwa bahati mbaya mtoto wa mama mwingine amekaa karibu na mimi akaanza kuzililia. Imebidi nivae earphones. Napenda watoto, ila utoto ndio sipendi.

4.Jana nimepita njia ya mkato makaburini, warembo wawili wakawa wananikimbilia wanatetemeka eti tunaogopa kupita peke yetu na mimi nikawajibu hata mimi nilivyokuwa hai nilikuwa naogopa sana. Wakazimia.

Sipendagi kufatwa fatwa.
 
Juzi nilipomsikia Mkuu wa mkoa Dar Es Salaam akisema biashara ziwe kwa mfumo wa take away nilifurahi sana kwa vile itapunguza misongamano. Lakini naona hii kauli bado kuna sehemu hawaizingatii! Jana nimezunguka sana usiku maeneo ya Sokota, Kona bar, Sinza, Kimboka, Batoto, wameshindwa kuniwekea ile bidhaa kwenye take away!

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"
 
Basi utaondoka na stress..!

Stress ni nini??
Stress ni pale umeenda kijijini kwa bibi ako huku umebeba jeans zako tano zile ja mtindo wa kuchanika (chanika jeans) sasa siku ukazifua ukazianika ukaenda zako kutembea ile unarudi jioni unakuta bibi yako kazianua afu kazishona zote!


Future
kmmk na lakumfanya huna kajiongeza zake😄
 
Vyoo vya uswazi noma sana unaingia chooni kufanya mambo yako Halafu by the time unajikaza mzigo utoke Unaona mlangoni pameandikwa


"UNGEKUWA UNAJIKAZA HIVYO MAISHANI UNGESHANUNUA PRADO"

Sent using myLG leon
Choo hadi kiandikwe hivyo unajua kabisa hayo maeneo ni maeneo ya namna ya watu hao hao ,( Wahuni )
 
Ndugu zangu niko njia panda

“Shemeji yeenu wa zamaaanii, leo kanikumbuka kasema anataka kuja kulala kwangu,

Aisee kila nikifikiria ujio wake lazima mie nioge, nguvu zinaniishia.

Kunakoelekea naikataa hii ofa, yaani mie nioge leo, makaveli mie nioge na baridi hili




Sent using Jamii Forums mobile app
Usioge, nipaje sanitaiza alafu subiri kiporo kije
 
Yaani bangi nilovuta leo ovyo sana! Nimeandika note flani hivi kwenye simu yangu, tatizo limekuja kila nikisave najibiwa Note saved nimefanya kama mara 10 hivi...jibu ni hili hilo....nahisi simu yangu itakuwa mbovu

ᵀʰᵉ ᶠⁱʳˢᵗ ʳᵘˡᵉ ᵒᶠ ʷᵃʳ ᵃⁿᵈ ᵇᵘˢˢⁱⁿᵉˢˢ ⁱˢ "ᴷⁿᵒʷ ʸᵒᵘʳ ᵉⁿᵉᵐʸ ᵇᵉᵗᵗᵉʳ"
Tatizo unakula bangi zilizo komaa sana
 
Back
Top Bottom