grandMullah23m
JF-Expert Member
- Mar 9, 2017
- 234
- 310
Mkuu... Sasa kwa kijana kama mimi nitaanzaje na kamtaji kenyewe laki tatu... Kuna kutoka hapo kwel auUmeandika vizuri na umeeleweka ukiona mtu anauliza swali huyo Hana nia na hawezi mikiki mikiki ya hyo kazi sababu umeandika vitu muhimu na umenyoosha.
Binafsi nishafanya Ila ilkua n nguruwe mnadani unatakiwa uwe mjanja na mshapu Ila door to door n nzuri muhimu uwe unajua kwa macho kuwa huyu ukimuangalia hakosi KG kadhaa hvyo unakata hata 7kg ndo unaongea Bei na mnunuzi.
Changamoto ya Door to door unatakiwa ujue kuishi na watu ukikuta watu wanakula ugali wa mdama na dagaa wa kuchemsha unga usilete swaga, Kuna muda inabidi ulale hukohuko bush kwa wenyeji Kama n kulala chini lala Kama n kwenye ngozi lala faida yake utakuja kuiona baadae.
Ukiingia Kijiji unakutana na mjanja wao Sasa wewe kuwa mjanja zaidi yake wengi wanaongea kilugha hvyo jifunze kujua maneno muhimu kwenye Biashara yako katika sehemu unayokwenda kutafuta mifugo.
Jifunze kumsoma mtu usoni pindi mnaposalimiana tuu au akiongea maneno matatu hii itakusaidia kupata kwabei nafuu.
Vijana tupambane usisubiri mpaka ufike 1million ndo uanze Anza na hicho hicho ulichonacho Kama una Nia inakutoa bila shida hata Kama n laki moja we Anza na pale inapowezekana.