Kama una aibu unaweza kujifunika, lakini lazima issue iongelewe!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779

KILA LA KHERI KWENYE MAONGEZI
Kama una aibu unaweza kujifunika, lakini lazima issue iongelewe! Sex ni somo au kitu ambacho ni exciting duniani, hata hivyo ni kitu kigumu sana na husumbua sana kujadili na hii inatokea mara nyingi kwa wale walio kwenye ndoa.

Mwanaume na ujanja wake wote kuna wakati hujikuta ananywea kuongelea suala la sex au kumshirikisha mke mpenzi nini wafanye ili wanapokuwa mwili mmoja kuwa na kuridhika kwa kila mmoja.
Pia wapo wanawake huogopa kuongea bayana na wazi kile wanahitaji kwa mume au mahusiano na kwa kuwa kuna stima kubwa kwa mwanamke kuwa passive kwenye ndoa matokeo kila mmoja anakula jiwe na wote huishia kuumia na kuugulia wakati wanandoa wengine duniani wanaongea na kuweka sawa mambo yao chumbani bila woga.

Kawaida unavyochelewa au kuacha kuongelea issue hii ya sex kwenye kuta nne za chumba chenu ndivyo inazidi kuwa ngumu zaidi na huzidi kuwapa disconnection ya feeling kwenu wawili.

Jambo la msingi ni kufanya haya Yafuatayo:-
Omba Mungu akupe hekima na busara ili uweze kujadiliana na mume wako au mke wako kwa upendo na wazi issue hii, wewe unadhani uliondoka kwa wazazi wako kuja kwake ili iweje kama si kupata mtu ambaye atakupa hitaji la mwili wako.
Hii issue ni muhimu kuijadilia kama mnavyojadili mipango mingine ya familia kama fedha na miradi.

Tafuta muda ambao wewe na mwenzi wako mnaweza kukaa chini na kujadili, tafuta sehemu ambayo imetulia na hamuwezi kusumbuliwa na kitu chochote.

Muhakikishie kwamba unampenda na onesha msingi wa upendo ulio nao kwake, elezea hisia zako halisi na kwamba kuna kitu ambacho hukipati katika maisha ya ndoa, na kwamba ungependa muongelee na ukipate.

Hatua kubwa na ya msingi ni kwa wote kukubali kwamba kuna tatizo.
Ukweli ni kwamba ukiona unashindwa kuongelea issue za sex kwenye ndoa, maana yake mnashindwa kuongelea mambo mengi ya msingi.
Pia kuongelea suala la sex ndani ya ndoa huweza kuwaweka karibu zaidi na wanawake hupenda sana hii topic kwani huonesha mwanaume anajali.

Tegemea kupata solution na uwe positive kwani unaweza kushinda tatizo lolote kwa kumtegemea Mungu


Wafilipi 4:13.
 
Kuongea tu mpaka kujifunika!! Basi kazi.

hilo tu wengine bila giza ajachoboa nguo zake........
 
Back
Top Bottom