Kama umeshindwa kuwa na demokrasia kwenye chama, utawezaje kuwa na demokrasia kwenye nchi?

Emc2

JF-Expert Member
Sep 26, 2011
16,808
16,831
Nawasalimia wadau wa JF.

Kuna baadhi ya vyama vya siasa hapa nchini kwetu, mwenyekiti ni kama mfalme. Tangu aingie madarakani hana mpango wa kupisha wengine waweze kuongoza chama.

Na kuna vyama tangu vijulikane katibu mkuu wake ni yule yule tu. Miongo zaidi ya miwili bado yupo kwenye kiti hicho, huku akidai kugombea kuongoza nchi.

Kama kiongozi huyo ameshindwa kuleta demokrasia ndani ya chama chake je, ni halali kumwamini kiongozi huyo na chama chake?

Viongozi hao wameonekana wakijaribu na kuweza kuwafumba midomo wengine wenye nia ya kugombea kiasa cha kuwaita wasaliti na kuwaundia zengwe zito na wanabaki kuwa makabwela.

Zengwe zito linaloleta ukabwela linafanya wenye kung'amua mambo na kuwaona hao watu kama hawajajiandaa au wanataka kuwa wafalme ndani ya chama.

Ni vyema kutoa boliti kwenye jicho kabla ya kukatoa ka kibanzi kwenye jicho la wengine.
 
Nawasalimia wadau wa JF.

Kuna baadhi ya vyama vya siasa hapa nchini kwetu, mwenyekiti ni kama mfalme. Tangu aingie madarakani hana mpango wa kupisha wengine waweze kuongoza chama.

Na kuna vyama tangu vijulikane katibu mkuu wake ni yule yule tu. Miongo zaidi ya miwili bado yupo kwenye kiti hicho, huku akidai kugombea kuongoza nchi.

Kama kiongozi huyo ameshindwa kuleta demokrasia ndani ya chama chake je, ni halali kumwamini kiongozi huyo na chama chake?

Viongozi hao wameonekana wakijaribu na kuweza kuwafumba midomo wengine wenye nia ya kugombea kiasa cha kuwaita wasaliti na kuwaundia zengwe zito na wanabaki kuwa makabwela.

Zengwe zito linaloleta ukabwela linafanya wenye kung'amua mambo na kuwaona hao watu kama hawajajiandaa au wanataka kuwa wafalme ndani ya chama.

Ni vyema kutoa boliti kwenye jicho kabla ya kukatoa ka kibanzi kwenye jicho la wengine.


Kuna chama hata kishindwe uchaguzi kwa kura kinalazimisha kwa nguvu kubaki madarakani kwa madai kuwa vyama vingine vikiongoza kutatokea vurugu na kutumia vyombo vya dola kupora ushindi kwa mabavu
 
Kuna chama hata kishindwe uchaguzi kwa kura kinalazimisha kwa nguvu kubaki madarakani kwa madai kuwa vyama vingine vikiongoza kutatokea vurugu na kutumia vyombo vya dola kupora ushindi kwa mabavu
Je, mwenyekiti anaye kaa kwenye uongozi zaidi ya miongo miwili yupo tofauti na mfalme wa chama?
 
Je chama kinachokaa madarakani kwa nguvu kina tofauti na utawala wa kidikteta na kifalme?
Swali dogo tu. Unataka kufananisha mtu mmoja na chama kilichoshinda kwa kupigiwa kura na jamaa mmoja ambaye hataki hata wanachama kupiga kura?
 
Swali dogo tu. Unataka kufananisha mtu mmoja na chama kilichoshinda kwa kupigiwa kura na jamaa mmoja ambaye hataki hata wanachama kupiga kura?


Nobody can understand your question can rewrite it?
 
Ukitumia akili yako vyema....na kujitoa kwenye koti la mahaba....unagundua kuwa katika nchi hii...hakuna wapinzani ambao tunawatazamia kutuletea neema...bali ni magenge ya wapiga dili...wanaolilia fursa ya kuiba rasilimali za umma kupitia uongozi......

CCM kumeoza na huko Upinzani ndio kunatoa funza kabisa......
 
Swali dogo tu. Unataka kufananisha mtu mmoja na chama kilichoshinda kwa kupigiwa kura na jamaa mmoja ambaye hataki hata wanachama kupiga kura?

Huwa nashangazwa sana na watu wanaojiita wapinzani wa nchi hii.....wanaojitanabaisha kuwa ni watetezi wa demokrasia...ili hali mioyoni mwao wanajijua kuwa ni maadui wa demokrasia.....

Wanapigania uhuru wa kutoa maoni na kujieleza hali ya kuwa wao wenyewe hawaheshimu wala si wavumilivu wa maoni ya wengine.....

Utawagundua hata humu...kupitia matusi yao kwa watu walio na mtazamo tofauti na wa kwao.....
 
Ukitumia akili yako vyema....na kujitoa kwenye koti la mahaba....unagundua kuwa katika nchi hii...hakuna wapinzani ambao tunawatazamia kutuletea neema...bali ni magenge ya wapiga dili...wanaolilia fursa ya kuiba rasilimali za umma kupitia uongozi......

CCM kumeoza na huko Upinzani ndio kunatoa funza kabisa......
Umeongea la maana sana Mkuu. Kuna watu wanawaongopea wananchi eti wanataka kuleta ukombozi, huu ni uongo kabisa, kwani wao wanachogombea ni madaraka na siyo ukombozi.
 
Ya Ngoswe muachie...Fanya yako
Ndugu ni muhimu kuonesha kwa mifano tunayo yahubiri. Huwezi kuhubiri watu waache wizi wakati wewe ni jambazi. Ni lazima tuache siasa za kilaghai.
 
Ukitumia akili yako vyema....na kujitoa kwenye koti la mahaba....unagundua kuwa katika nchi hii...hakuna wapinzani ambao tunawatazamia kutuletea neema...bali ni magenge ya wapiga dili...wanaolilia fursa ya kuiba rasilimali za umma kupitia uongozi......

CCM kumeoza na huko Upinzani ndio kunatoa funza kabisa......
Kweli tupu.Na hiyo ndio sababu inayofanya CCM iendelee kuwa madarakani.Upinzani dhaifu.kila mtu anajua kuwa CCM haifai,lakini sasa unajiuliza,is there a better alternative?.vyama vyetu vimekaa kibiashara zaidi na sio katika mfumo wa kiharakati wenye lengo la kumkomboa mwananchi.Vyama vingi vimekuwa na harakati za kimatukio tu na kujali zaidi mambo ya kuwapa kiki kisiasa na sio kudili na matatizo ya wananchi.
Hatuhitaji wanasiasa wavyama vya upinzani wanaotuahidi mengi mazuri watakayofanya tukiwapa hatamu bali tunahitaji wanasiasa wanaoshiriki kikamilifu katika kuleta mabadiliko wanayoyahubiri majukwaani.
Hatuhitaji upinzani wa kuonekana kwenye press conferences na mikutano ya hadhara iliyojaa malalamiko tu na ukosoaji usiokuwa constructive.Tunahitaji wapinzani wanaofanya mobilization kwenye communities zao na kutumia influence na rasilimali walizonazo kuwaletea wafuasi na wananchi wao maendeleo.wapinzani wafanye investment kubwa ndani ya jamii zinazowazunguka zitakazotatua matatizo ya wananchi kama ajira n.k
Wajenge community centers,hospitali,viwanja vya michezo na mengineyo.Watuonyeshe kwa vitendo falsafa na ilani zao wanazozipigia debe.twataka shamba darasa ati.
Ukawa wakiamua kutumia ruzuku zao pamoja na michango na harambee kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya huduma za jamii na biashara sidhani kwamba watashindwa.tukisema tusubiri ccm itoke madarakani ndio maendeleo yaje nadhani itachukua miaka mia na zaidi kwa sheria zetu za uchaguzi zilizopo.
 
ukweli hatuna upinzani bali ni kikundi cha watu wachache wanaotumia upinzani ili kufikia malengo yao, wengi wameanzisha vyama kama NGO ndio maana unaona mpaka sasa pamoja na mahakama ya Afrika kuruhusu mgombea binafsi hakuna chama hata kimoja kinachoshinikiza serikali itekeleze hukumu ya mahakama kwani wanajua wakifanya hivyo ndio mwanzo wa vyama vingi kupotea ikiwamo ccm kwani wale wenye nia nzuri wanakaa pembeni kwa sababu hawawezi kuvumilia madudu yanayofanyika kwenye vyama vya siasa
 
Kwa mbaali naona kina Mfalme mbowe na mwenzie wa kulee wanavyotoa macho maana hao ndio hawataki kusikia mabadiliko,wanaamin wao ndio wao hakuna mwingine alaf wanakuja na madai ya democracy
 
Ukitumia akili yako vyema....na kujitoa kwenye koti la mahaba....unagundua kuwa katika nchi hii...hakuna wapinzani ambao tunawatazamia kutuletea neema...bali ni magenge ya wapiga dili...wanaolilia fursa ya kuiba rasilimali za umma kupitia uongozi......

CCM kumeoza na huko Upinzani ndio kunatoa funza kabisa......
word
 
Kwa nini tumung'unye maneno? Wapinzani Tanzania wanatakiwa wa step down kwa muda ili wawa achie wenye vision ya kweli wame prove ku fails ndani ya miaka zaidi ya ishirini na tano.
 
Huwa nashangazwa sana na watu wanaojiita wapinzani wa nchi hii.....wanaojitanabaisha kuwa ni watetezi wa demokrasia...ili hali mioyoni mwao wanajijua kuwa ni maadui wa demokrasia.....

Wanapigania uhuru wa kutoa maoni na kujieleza hali ya kuwa wao wenyewe hawaheshimu wala si wavumilivu wa maoni ya wengine.....

Utawagundua hata humu...kupitia matusi yao kwa watu walio na mtazamo tofauti na wa kwao.....
Aaah hii tabia ni mbaya sana...sasa wewe kuwaita wenzio wapinzani na kujitoa wewe wakati na wewe unawapinga hao ...Jitambue
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom