Kama umeshindwa kutimiliza ndoto zako, badili njia zako

Siasa Basi

JF-Expert Member
Jul 10, 2016
1,493
4,276
Watu waliofanikiwa ni kwamba wana mambo mawili tu usoni, "tabasamu na ukimya". Tabasamu linaweza tatua tatizo na ukimya waweza zuia tatizo.

Sukari na chumvi vyaweza kuchanganywa pamoja ila sisimizi ataacha chumvi na kuondoka na sukari. Chagua marafiki sahihi watakaokuongoza njia njema.

Kama umeshindwa kutimiliza ndoto zako, badili njia zako kamwe usibadili Mungu wako na kwenda kulikopotoka zaidi.

Kumbuka, Miti hubadilisha matawi na majani na sio mizizi. Hauwezi kufikia malengo yako kama utasimama na kurushia mawe kwa kila mbwa atakaekubwekea. Ziba masikio na songa mbele. Mwenda tezi na omo, marejeo ngamani.

Wanaokuchukia (haters) watakuona ukitembea kwenye maji na watasema ni kwa sababu hujui kuogelea. Na kama utacheza kwenye maji adui zako watakushutumu kwamba unawatimulia vumbi, vumbi na maji wapi na wapi jamani!

Weka lengo lako na kuishi maisha yako, kudili na kazi zako na kufanya kazi kwa mikono yako. Tambua huwezi ukamridhisha mwanadamu hata siku moja, ukifanya hili atasema bora ungalifanya lile.

Kumbuka, kamwe usicheze mieleka na Nguruwe. Wote mtachafuka, ila nguruwe atafurahia.

Kupoteza muda ni kubaya sana kuliko kupoteza pesa, pesa inatafutwa na kutumika ila muda unatumika na kamwe hautafutwi.

work, work, work, work, work!!!

Be Inspired and have a great day.
 
UJUMBE MZURI KATIKA MUDA MWAFAKA KABISA.JAMII FORUMS INAHITAJI WATU KAMA WEWE MKUU.UBARIKIWE SANA
 
Nimekuelewa vizur sana mungu akubariki sana.mara zote watu hasa walioajiriwa wanaishia kulalamika wewee na bila kujua muda sio rafiki tena
 
Back
Top Bottom