Kama ulishawahi kukwea hii treni sema neno...

Zeni2017

JF-Expert Member
Apr 27, 2017
1,247
532
cfc4ebae86bd5a644fa2059bb391866b.jpg


Watoto wa miaka ya 90 hamtaelewa kitu. Tushukuru Magufuli ana mpango wa kuleta treni mpya. Nchi ikikosa treni ni afadhali tu irudi kwenye stone age (zama za kutumia mawe)
 
Sasa uwe daraja la tatu kajamba nani hiyo ilikuwa inaitwa. Hivi walikuwa wanalipa wale? Au Nyerere aliwafadhili?
 
Nashindwa kusema kwa sauti, labda niseme tu kimoyomoyo.... yeaah
nachokumbuka zaidi toka enzi zile huu ukiwa ndio usafiri wetu ni Saranda
 
Kuna likizo moja wanafunzi tulijaza behewa kuna jamaa alikuwa na box likapasuka. Vilitoka vijiko vingi sana vya zamani alichekesha ila mpaka leo sijui vijiko vile alivitoa wapi na alikusudia kwenda kuvifanyia nini.
 
Hii Kitu ina historia historia kubwa maishani mwangu... Salute Garimoshi aka jongooo
 
Baada ya kumaliza likizo ya form one (nyumban Shinyanga alipozaliwa Kanumba, Noorah mzee wa Icecream, Johari muigizaji, Andrew Chenge na Hayati Bob Makani)

Basi nikamuomba dingi nauli ya treni (ilikua 5000 kutoka Shinyanga mpaka Tabora).
Khaaa dingi akasema hana hela, nisubiri next week. Nikaona ananizingua.
Mfukoni nilikua na 3500.

Nikasema mi Mboyzia bana (waliosoma Tabora Boys alikosoma J.K.Nyerere, Samuel Sitta, Mukandara, Zitto Kabwe, Joshua Nassari) wanajua nini maana ya neno Mboyzia.

Basi nilikua na hamu ya kuwahi Boys kwenda kuwaonea ma form nyoya wapya, usiku ule nikatoroka home na begi langu.
Huyooo mpaka stesheni. Ngoma tano usiku Gogo la kutoka Mwanza hili hapa.

Bila ajizi, kama mshale vile nikadandia behewa limeandikwa herufi F ubavuni (kwa chaki).

Kufika maeneo ya Tinde Tiitii akapita kukagua tiket.
Mboyzia nikatoa 3500 Mfukoni na excuse kibao juu, nawahi shule, baba kafariki, sina msaada.

Kubabake yule Tiitii alikua bandidu kishenz.
Akanikomalia dogo ongeza hiyo jero, umeificha sio??? La sivyo nakushusha.

Ebana eeeeh...
Kufika stesheni ya Bukene nikashushwa kweli... Niliangua kilio pale usiku wa saa nane (mpaka Makamasi) Tiitii akanihurumia, kabla Gogo halijapiga kipenga akaniambia "Panda dogo kuna wachawi hapa, siku nyingine usirudie"

Sitosahau kwa kweli.
Mtumishi Mcharo
 
Raha ya hii kitu uzamie. Wale maaskari wakifika mnapishana nao chooni.
 
mnawaonea sana hawa waliozaliwa 90 nakumbuka 2006 na 2008 treni ilikuwepo na ilikua muhimu sana kwa abiria hivyo watoto wa 90 wengi waliipanda sana. Acheni kujidai wa ushuani. Watoto waliozaliwa 2000 hawa ndo wa kusema hawaijui adha ya treni
 
Hukuwa mjanja mi kuna wakati nilikuwa ña wakwepa na lala uvunguniau ikisimama nashuka naenda behewa ambalo titii ameisha kagua. Vivyo hivyo kwenye meli. Ila hii ya Magu usijaribu kudandia ina kasi ya ajabu
 
Baada ya kumaliza likizo ya form one (nyumban Shinyanga alipozaliwa Kanumba, Noorah mzee wa Icecream, Johari muigizaji, Andrew Chenge na Hayati Bob Makani)

Basi nikamuomba dingi nauli ya treni (ilikua 5000 kutoka Shinyanga mpaka Tabora).
Khaaa dingi akasema hana hela, nisubiri next week. Nikaona ananizingua.
Mfukoni nilikua na 3500.

Nikasema mi Mboyzia bana (waliosoma Tabora Boys alikosoma J.K.Nyerere, Samuel Sitta, Mukandara, Zitto Kabwe, Joshua Nassari) wanajua nini maana ya neno Mboyzia.

Basi nilikua na hamu ya kuwahi Boys kwenda kuwaonea ma form nyoya wapya, usiku ule nikatoroka home na begi langu.
Huyooo mpaka stesheni. Ngoma tano usiku Gogo la kutoka Mwanza hili hapa.

Bila ajizi, kama mshale vile nikadandia behewa limeandikwa herufi F ubavuni (kwa chaki).

Kufika maeneo ya Tinde Tiitii akapita kukagua tiket.
Mboyzia nikatoa 3500 Mfukoni na excuse kibao juu, nawahi shule, baba kafariki, sina msaada.

Kubabake yule Tiitii alikua bandidu kishenz.
Akanikomalia dogo ongeza hiyo jero, umeificha sio??? La sivyo nakushusha.

Ebana eeeeh...
Kufika stesheni ya Bukene nikashushwa kweli... Niliangua kilio pale usiku wa saa nane (mpaka Makamasi) Tiitii akanihurumia, kabla Gogo halijapiga kipenga akaniambia "Panda dogo kuna wachawi hapa, siku nyingine usirudie"

Sitosahau kwa kweli.
Mtumishi Mcharo
Hmmnn!

We Padri mhuni' uko parokia gani! ??
 
Back
Top Bottom