Kama ulinunua Gari kabla ya Kujenga nyumba ya kuishi, hili la kulipa kodi ya jengo kwa njia ya LUKU, Halikuhusu, Kaa Kimya

Chee4

Member
May 17, 2021
35
125
DAda zangu wa mjini nawapa angalizo, Kama boyfriend wako aliwahi kukuambia kajenga nyumba kijijini kwao ambayo hujawahi kuiona, halafu leo kwa namna yoyote ile umemsikia au umemshudia akilalamika kuhusu kulipa kodi ya majengo kwa LUKU, achana nae, hana nyumba huyo. ALIKUDANGANYA. Kwanini nasema hivi;

Kodi ya Majengo sio kodi mpya, ipo tangu kitambo, mafaza wengi wameshalipa na hawajawahi kulalamika, wengi wanaopiga leo ni wapangaji, HAKUNA mwenye nyumba anaweza kulalamikia Serikali wakati mfumo huu mpya unamrahisishia kero za ulipaji kodi, kutoka Kwenda kupanga foleni Halmashauri siku nzima, hadi kulipa kwa Simu akiwa anakula Katles nyumbani kwake, easy tu yaan.

Inawezekana maneno haya 'kodi ya majengo' ni MSAMIATI mpya kwa vijana wengi waliokimbilia magari na iphone mjini kabla ya kujenga nyumba zao, nashangaa hawa mabrazamen wanatoa wapi ujasiri wa kujadili jambo lisilowahusu, Hili la kulipa Kodi kwa njia ya Luku linatuhusu sisi wakina baba wenye nyumba mjini, nyie wapangaji KAENI KIMYA. Haliwahusu. Nyie ni mamidoman tu.

Kama mnataka kujadili basi njooni tujadili changamoto zake, ambazo kimsingi ni mbili tu, ya kwanza ni Nyumba nyingi wapangaji ndio wanalipa LUKU, sasa kama kodi itakatwa kwenye Luku hatuoni kama wapangaji ndio watakuwa wakilipa Kodi za majengo badala ya wenye nyumba? Changamoto ya pili ni Je kwa nyumba moja yenye wapangaji watatu na luku 3, Kila mpangaji (kila Luku) atalipa kodi ya jengo?

Kwa kuwasadia, hizi changamoto ni ndogo mno ukilinganisha na faida za huu mfumo mpya, Kuhusu nani atalipa Kodi, wewe Mpangaji kubaliana na mwenye nyumba wako, mkatanaje, unaweza ukamkakata elfu 6 ambayo ni kodi ya jengo ya miezi sita, wakati unamlipa hela yake au vyovyote mtakavyokubaliana. kama mwenye nyumba wako hakubali utaratibu wa kumkata kwenye kodi yake, hama kwenye hiyo nyumba, huyo ni TAPELI.

Kuhusu Nyumba moja yenye Luku 3, mwenye nyumba atachagua Luku ipi iwe inalipa kodi ya jengo ya nyumba yake yote (nzima), hamtalipa wote, mpangaji mwenye Luku itakayochaguliwa na mwenye nyumba ndio atakayekubaliana na mwenye nyumba utaratibu wa ulipaji, kama ni kukatana kwenye kodi au vinginevyo.

Sasa mlikuwa tunalalamika nini? Hata kama mna stress za kodi za nyumba mlizopanga, muwe mnatafakari kabla ya kutoa maoni yetu, ANYWAY, siwalaumu sana, siku mkijenga zenu, mtaelewa.

Ahsante TRA, Ahsante TANESCO na Ahsante kubwa kwa Serikali kwa kuturahisishia sisi wenye Nyumba ulipaji wa Kodi ya Majengo, Hakuna kupanga foleni tena.
 
... hivi yale manamba yaliyobandikwa kwenye mageti kutambua nyumba nchi nzima hayana maana tena? Tulivyopelekeshana sijui serikali za mitaa kupata anwani za makazi nguvu yote ile ni zero?

Hii nchi kwa vituko tuko vizuri. No plan, no what akikurupuka mwenye mamlaka akitaka iwe inakuwa but unsustainable! Yale yale ya usajili wa sim cards yet matapeli wanaendelea kusumbua! Why?

Nchi hii tunakosea wapi? Ardhi, watu, siasa safi, uongozi bora Mwl aliwahi kutuasa ndio pillars za maendeleo. Kuna mahali tunakosea katika hayo.
 
Mama anaupiga mwingi kama Okwi...

Mitano tena kwa mama tafazali
 
Roho inaniuma sana sijaamia hata naambiwa nianze kulipia.
Hivi kuna kodi ya pango (nyumba)na kodi ya ardhi (kiwanja au shamba au eneo)ni hiyo hiyo au ni 2 tofauti.?
 
Ukweli mchungu hkuna mwenye nyumba ailalamikie 12000/- eti mwenye ghorofa Lake ailalamikie 50000/ muda mwingne tuwe wazalendo tu.
 
Mama anaupiga mwingi kama Okwi...

Mitano tena kwa mama tafazali
Si wewe ulikuwa unademka humu ukifurahia kwamba sasa chama kimetoka mikononi mwa washamba na kimerudi kwa wenye nacho?

Na bado, wenye nacho ndio hao sasa wanataka chao!

Hapo bado bidhaa za vyakula hazijapanda, mbona maji mtaita mma!
 
Si wewe ulikuwa unademka humu ukifurahia kwamba sasa chama kimetoka mikononi mwa washamba na kimerudi kwa wenye nacho?

Na bado, wenye nacho ndio hao sasa wanataka chao!

Hapo bado bidhaa za vyakula hazijapanda, mbona maji mtaita mma!
Na wewe utayaitaje maji? Au ccm hamkatwi kodi na tozo?
 
Nikiwa nimefunga Solar system itakuwa hii kodi hainihusu mjengoni?
 
DAda zangu wa mjini nawapa angalizo, Kama boyfriend wako aliwahi kukuambia kajenga nyumba kijijini kwao ambayo hujawahi kuiona, halafu leo kwa namna yoyote ile umemsikia au umemshudia akilalamika kuhusu kulipa kodi ya majengo kwa LUKU, achana nae, hana nyumba huyo. ALIKUDANGANYA. Kwanini nasema hivi;

Kodi ya Majengo sio kodi mpya, ipo tangu kitambo, mafaza wengi wameshalipa na hawajawahi kulalamika, wengi wanaopiga leo ni wapangaji, HAKUNA mwenye nyumba anaweza kulalamikia Serikali wakati mfumo huu mpya unamrahisishia kero za ulipaji kodi, kutoka Kwenda kupanga foleni Halmashauri siku nzima, hadi kulipa kwa Simu akiwa anakula Katles nyumbani kwake, easy tu yaan.

Inawezekana maneno haya 'kodi ya majengo' ni MSAMIATI mpya kwa vijana wengi waliokimbilia magari na iphone mjini kabla ya kujenga nyumba zao, nashangaa hawa mabrazamen wanatoa wapi ujasiri wa kujadili jambo lisilowahusu, Hili la kulipa Kodi kwa njia ya Luku linatuhusu sisi wakina baba wenye nyumba mjini, nyie wapangaji KAENI KIMYA. Haliwahusu. Nyie ni mamidoman tu.

Kama mnataka kujadili basi njooni tujadili changamoto zake, ambazo kimsingi ni mbili tu, ya kwanza ni Nyumba nyingi wapangaji ndio wanalipa LUKU, sasa kama kodi itakatwa kwenye Luku hatuoni kama wapangaji ndio watakuwa wakilipa Kodi za majengo badala ya wenye nyumba? Changamoto ya pili ni Je kwa nyumba moja yenye wapangaji watatu na luku 3, Kila mpangaji (kila Luku) atalipa kodi ya jengo?

Kwa kuwasadia, hizi changamoto ni ndogo mno ukilinganisha na faida za huu mfumo mpya, Kuhusu nani atalipa Kodi, wewe Mpangaji kubaliana na mwenye nyumba wako, mkatanaje, unaweza ukamkakata elfu 6 ambayo ni kodi ya jengo ya miezi sita, wakati unamlipa hela yake au vyovyote mtakavyokubaliana. kama mwenye nyumba wako hakubali utaratibu wa kumkata kwenye kodi yake, hama kwenye hiyo nyumba, huyo ni TAPELI.

Kuhusu Nyumba moja yenye Luku 3, mwenye nyumba atachagua Luku ipi iwe inalipa kodi ya jengo ya nyumba yake yote (nzima), hamtalipa wote, mpangaji mwenye Luku itakayochaguliwa na mwenye nyumba ndio atakayekubaliana na mwenye nyumba utaratibu wa ulipaji, kama ni kukatana kwenye kodi au vinginevyo.

Sasa mlikuwa tunalalamika nini? Hata kama mna stress za kodi za nyumba mlizopanga, muwe mnatafakari kabla ya kutoa maoni yetu, ANYWAY, siwalaumu sana, siku mkijenga zenu, mtaelewa.

Ahsante TRA, Ahsante TANESCO na Ahsante kubwa kwa Serikali kwa kuturahisishia sisi wenye Nyumba ulipaji wa Kodi ya Majengo, Hakuna kupanga foleni tena.
Kodi ya jengo tulikuwa tunalipia kupitia mtandao sasa unaposema foleni sikuelewi, inanihakikishia hauna nyumba.
 
Nikiwa nimefunga Solar system itakuwa hii kodi hainihusu mjengoni?
Wasio na umeme wataendelea kulipa kwa mtindo wa zamani yaani mtaendelea kupanga foleni halmashauri na kulipa kwa mkupuo yaani 10000 na unapewa risiti.
 
Mkuu mbona kama unawafokea wasio na nyumba? hapa mjini lazima uanze kama mpangaji......baadaye mdogo mdogo ndo unamiliki mjengo. Kama vipi wenye nyumba wachangie hiyo buku 12 kwenye luku ya wapangaji ili ilipe kodi ya jengo........halafu ndugu mtoa mada hujatueleza uhalali wa wakazi wa vijijini kulipa kodi ya jengo ikiwa nyumba zao ni duni, yaani full suti na makazi yao hayajarasimishwa......
 
Si wewe ulikuwa unademka humu ukifurahia kwamba sasa chama kimetoka mikononi mwa washamba na kimerudi kwa wenye nacho?

Na bado, wenye nacho ndio hao sasa wanataka chao!

Hapo bado bidhaa za vyakula hazijapanda, mbona maji mtaita mma!
Mama anaupiga mwingi....

Tuacheni tudemke na mama yetu...

Kazi iendelee...
 
Back
Top Bottom