Idd Ninga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 5,136
- 4,298
ASANTE KWA KUNILIZA.
1.Nilijua nimefika,nawe utanituliuza
Wakufa na kunizika,leo tena waniliza
Mdomo naufunika,wala sitokuuliza
Asante kwa kuniliza,nakuombea baraka.
2.Japo chozi lanitoka,maumivu napuuza
Mbali nawe naondoka,nakwacha dada muuza
Nenda kunako endeka,nibaki najiuguza
Asante kwa kuniliza,machozi nitayafuta.
3.Mapenzi yameanguka,shetani kayakatiza
Moyoni ninafunguka,sitoweza kulipiza
Mabaya yakaja zuka,tena yakupitiliza
Asante kwa kuniliza,nakiri nimepigika.
4.Kwako nimejeruhika,kupona bado nawaza
Dawa inahitajika,nitanywa kujiliwaza
Moyoni nimevunjika,sana umenishangaza
Asante kwa kuniliza,na mola atakulipa.
5.Tamati tumeshafika,penzi umeliunguza
Penzi limevurugika,tumeshindwa kulikuza
Leo tunatawanyika,tamaa umetukuza
Asante kwa kuniliza,na fimbo umenichapa.
SHAIRI-ASANTE KWA KUNILIZA.
MTUNZI-Idd Ninga,Tengeru Arusha.
+255624010160.
iddyallyninga@gmail.com
1.Nilijua nimefika,nawe utanituliuza
Wakufa na kunizika,leo tena waniliza
Mdomo naufunika,wala sitokuuliza
Asante kwa kuniliza,nakuombea baraka.
2.Japo chozi lanitoka,maumivu napuuza
Mbali nawe naondoka,nakwacha dada muuza
Nenda kunako endeka,nibaki najiuguza
Asante kwa kuniliza,machozi nitayafuta.
3.Mapenzi yameanguka,shetani kayakatiza
Moyoni ninafunguka,sitoweza kulipiza
Mabaya yakaja zuka,tena yakupitiliza
Asante kwa kuniliza,nakiri nimepigika.
4.Kwako nimejeruhika,kupona bado nawaza
Dawa inahitajika,nitanywa kujiliwaza
Moyoni nimevunjika,sana umenishangaza
Asante kwa kuniliza,na mola atakulipa.
5.Tamati tumeshafika,penzi umeliunguza
Penzi limevurugika,tumeshindwa kulikuza
Leo tunatawanyika,tamaa umetukuza
Asante kwa kuniliza,na fimbo umenichapa.
SHAIRI-ASANTE KWA KUNILIZA.
MTUNZI-Idd Ninga,Tengeru Arusha.
+255624010160.
iddyallyninga@gmail.com